Sunday 29 June 2014

Fadhila za kusali Dhuhaa

Makala imeandaliwa na Raudhwah Islamic Group

Imesimuliwa na Abu-Hurayra -radhi za Allah ziwe juu yake- amesema:"Ameniusia Kipenzi changu(swalla Allahu alayhi wasallam) mambo matatu: Kufunga siku tatu kila mwezi,Rakaa mbili za Dhuha na kusali witri kabla ya kulala" Imepokelewa na Bukhari na Muslim na pia Mtume swalla Allahu alayhi wassalam alimuusia hayo hayo swahaba wake mwengine Abuu-Dardai radhia Allahu anhu katika hadityhi ilopokelewa na Imam Muslim na Abu-Daud

Ndugu zangu wa kiisalamu, sala ya dhuha ni sala yenye ujira mkubwa lakini ni katika swala ambazo zimesahaulika katika jamii ya kiislamu, na hata wengine hawajui kama kuna sunna hiyo, hii ni kutokana na kuwa na mishughuliko mingi ya kidunia kwani swala hii huswaliwa robo saa mara baada ya kuchomoza  jua mpaka kabla ya adhuhuri, hivyo watu huwa katika mishughuliko yao, na kusahau kusali sala hii, Anasimulia swahaba Abdullah bin Amr bin Aas -radhiallahu anhu kua mara moja maswahaba walirud katika vita hali ya kua wamepata ngawira nyngi na wamerudi katika muda mfupi sana, wakawa watu wanazungumzia kuhusu habari yao, Mtume akawauliza"Jee nikutajien kitu chenye thamani kuliko hata hizo ngawira na chenye kutosheleza muda? Maswahaba wakasema ndio. Akawaambia:Mwenye kutawadha akaelekea msikitini na kusali dhuhaa basi huyo kapata zaidi kuliko hata hizo ngawira" Imepokelewa na Imam Ahmad

Atakaeswali Dhuhaa kachukuliwa dhamana na Allah ya kusimamiwa mambo yake kwa siku ile kama anavyosema Mtume swallahu alayhi wassalam katika hadithi ilopokelewa na Uqba bin Amir radhia Allahu anhu kua "Amesema Allah kumwambia mwanadamu:Ewe mwanadamu nitosheleze mwanzo wa mchana kwa rakaa nne nami nitakutosheleza mwisho wa mchana" Imepokelewa na Imam Ahmad

swala ya dhuhaa ina rakaa mbili mpaka nane na muda wake ni robo saa baada ya kuchomoza jua na kabla ya adhuhuri , ina fadhila nyingi Allah atuwafikishe kuisali na atulipe ujira kamili
Wallahu a'alam.

Usisahau kusali DHUHA

3 comments: