Monday 6 October 2014

Faida za asali


Asali ni chakula kitamu. kinachotengenezwa na nyuki kwa kukusanya  nectar kutoka kwenye mauwa.Asali inaweza kaa miaka mingi sana bila kuharibika,asilimi kubwa ya wadudu waaribifu hawawezi kukua ndani ya asali kwani inakiasi kidogo sana cha maji  yaani 0.6(WATER ACTIVITY).Tone lolote la maji au mate linapoingia kwenye asali huongeza uwezakano wa kuaribika kwa asali hiyo na kufupisha maisha ya asali.Kwa ufupi naweza sema maji ni adui mkubwa wa asali.

Aina na ubora wa asali hutofautiana kutokana na aina ya nyuki walioitengeneza asali hiyo pomoja na aina ya maua ambayo nyuki wamenyonya nectar yake,rangi za asali pia hutofautiana kwa misingi hiyo hiyo.

Aina mbalimbali za asali.

Apa nchini Tanzania kuna aina kuu mbili za asali,asali ya nyuki wakubwa na asali ya nyuki wadogo.Asali ya nyuki wakubwa hupatikana kwa wingi zaidi kuliko ya nyuko wadogo,Lakini asali ya nyuki wadogo huuzwa bei ghali zaidi ya asali ya nyuki wakubwa kwani ilithibitika kwamba asali ya nyuki wadogo inatengenezwa kutoka kwenye nectar ya mauwa ambayo miti yake inausali wa dawa.Miti hiyo ni kama Mlonge,mwarubaini,rosella na mingine mingi.

Asali ni chakula kinachotumika kwa mambo mengi sana,unaweza itumia badala ya sukari kwenye vinywaji,kuipakaa kwenye mkate,na kuitumia kama kionjo kwenye vyakula mapishi mbali mbali,pia hutumika kutengeneza urembo wa aina mbalimbali kama mafuta na sabuni na vingine vingi,liakini zaidi ya yote asali hutumika kama dawa.

Ni vyema kujua kwamba asali mbichi(ambayo haijapitishwa kwenye moto)ni nzuri kuliko ile iliyopitishwa kwenye moto,Kwani pale asali inapopitishwa kwenye moto baadhi ya enzymes hufa na virutubisho vingine hupotea.Mara nyingi asali hupitishwa kwenye moto ili kuiyeyusha hasa pale inapotakiwa kuchujwa.

ASALI KAMA DAWA

Asali kama dawa inaweza kutibu matatizo mbalimbali,kumbuka tu tunaongelea asali ambayo haijachanganywa na kitu chochote.

For skin rashes, burns and abrasions.
Apply a small amount of raw honey lightly over the affected area; may cover with a dressing or a dusting of cornstarch to reduce any stickiness.

The ultimate moisturizer.
Smooth a small amount of raw honey lightly over the skin; easily remove later with splashes of cold water or comfortable warm water. Leaves skin baby soft.

As a bath and antibacterial soap.
Wash with raw honey straight from the jar and enjoy sparkling clean skin. Facial blemishes and acne caused by cosmetics or allergies will clear up quickly using a nightly treatment of RRH. A small amount needed.

For hair and scalp treatment.
Apply Really Raw Honey (with or without olive oil) to dry or damp hair about one half hour before washing–you’ll be amazed at your “crowning glory”.

For dental care and mouth sores.
Cleans teeth, mouth and dentures and stops bleeding gums. Canker sores, blisters and mouth ulcers respond to application of raw honey.

An astounding natural preservative.
Unprocessed honey found in ancient tombs was determined to be edible and was even used to preserve bodies. Keeps foods fresh and moist longer and retards spoilage.

For healing ulcers and burns
Also many years ago, a study by Robert Bloomfield, published in the Journal of the American Medical Association, reports “Applied every 2 to 3 days under a dry dressing, honey promotes healing of ulcers and burns better than any other local application. It can also be applied to other surface wounds, including cuts and abrasions…”

Honey has anti-cancer properties.
Recent studies by Gribel and Pashinskii indicated that honey possessed moderate antitumor and pronounced anti-metastatic effects in five different strains of rat and mouse tumors. Furthermore, honey potentiated the antitumor activity of chemotherapeutic drugs such as 5-fluorouracil and cyclophosphamide. — Gribel, N.V., and Pashinskii, V.G. Antitumor properties of honey. Vopr. Onkol., 36:704-709, 1990.

C.V. Rao at the American Health Foundation in Valhalla, New York found caffeic acids in propolis are inhibitors of colon cancers in animals. Other research shows hive products have the ability to prevent and halt the spread of malignant diseases. Earlier research by M.T. Huang also published in Cancer Research found caffeic acids effective in inhibiting skin cancer tumors in mice.

Ushauri
Ni  vyema ukawa na asali nyumbani kwa ajili ya matumizimbalimbali.Kwa matumizi ya asali kama dawa,nashauri asali mbichi ya nyuki wadogo.Najua ni ngumu kujua kama asali mbichi au imepitishwa kwenye moto,Hivyo nashauri utumie asali ya FANO 2010.

Asali za Fano 2010(Golden Lulu)

Asali za FANO 2010 zinapatika Thanks God supermarket,eneo la sinza madukani.nashauri asali hii kwani ndio asali ninayotumia na ninakuhakikishia kuwa ni asali mbichi,na zaidi ya yote niliwai tembelea workshop ya FANO 2010 na kuona jinsi wanavyochuja asali ,Ndio maana ninanguvu ya kushauri utumie asali hio

ONYO

Asali si nzuri kwa watoto wadogo wenye umri wa kati ya siku moja hadi miaka miwili,kwani wakati mwingine asali huwa na endospores wa bacterium  clostridium botulinum.Endospores hizo  zinaweza kubadilika kua aina ya bacteria wanatoa sumu.Bacteria hawa hushambulia utumbo mwembamba wa mtoto ambao haujakomaa  na hivyo  huweza msababishia mtoto kuumwa na  hata kifo.

Akina mama msikose chupa ya asali jikoni,kwani ajali za kuungua ni kawaida jikoni na asali ni dawa nzuri sana,Ukiungua kitu cha kwanza kabisa pakaa asali nyingi kwenye eneo uliloungua..

Nimalizie kwa kusema.Asali ikichanganywa na dawa zingine za asili au viungo fulani pia huwa dawa ya magojwa mengi zaidi.Naamini makala hii imekufumbua macho na kukufanya uithamini asali

Friday 26 September 2014

Uzushi Wa Unoadaiwa Ni Fadhila Za Siku Kumi Za Dhul-Hijjah


SWALI: 
 
Nimepokea e-mail iliyotumwa yenye kutaja fadhila za siku kumi kila siku kuwa ni jambo fulani limetokea na kadha kama inavyoeleza hapa chini. Je hii ipo dalili au ni katika uzushi?
 
Siku Kumi Bora

Mwenye-ezi mungu subhanahu wataala ameapa kwa masiku bora katika quraan takatifu sura 89 aya 1-2 isemayo : Mtume Muhammad ( S.A.W.) ametusimulia vilivyotendeka na umuhimu wa siku hizi kumi bora za mfungo tatu (DhulHijja); Rasula-llah atueleza sisi ummati wake  kuwa, mwenye kufunga siku hizo hupata fadhla kubwa mno,kwani kila   siku ina fadhila na kheri zake:

 SIKU YA KWANZA YA MFUNGO TATU Mtume (S.A.W.) asema kuwa - "Ni siku  ambayo Mwenye-ezi Mungu alimsamehe Nabii Adam (A.S.) kwa makosa  yake".Mwenye kufunga siku hiyo, Mwenye-ezi Mungu humsamehe madhambi  yake.   
 
 SIKU YA PILI YA MFUNGO TATUMtume(S.A.W.)asema kuwa:-"Ni siku  ambayo  Mwenye-ezi Mungu alikubali maombi ya Nabii Yunus (A.S.)  ya kumtoa  katika matumbo ya samaki".Mwenye kufunga siku hiyo,  ni kama  aliyefanya ibada ya mwaka mzima pasi na kufanya makosa.

   
 SIKU YA TATA MFUNGO TATU Mtume(S.A.W.)asema kuwa:-"Ni siku ambayo  Mwenye-ezi Mungu aliitikia Dua ya Nabii Zakariya (A.S.) yakumpata  mtoto".Mwenye kufunga siku hiyo, Mwenye-ezi Mungu huitikia dua  yake.

 
 SIKU YA NNE YA MFUNGO TATUMtume(S.A.W.)asema kuwa:-"Ni siku ambayo  alizaliwa Nabii Issa(A.S.)".Mwenye kufunga siku hiyo, Mwenye-ezi  Mungu humuondolea matatizo na umasikini.

 SIKU YA TANO MFUNGO TATU Mtume(S.A.W.)asema kuwa:-"Ni siku   alizaliwa  Nabii Musa(A.S) "Mwenye kufunga siku hiyo, Mwenye-ezi Mungu  humtakasa na unafiki na humuondolea adhabu za kabori.

 SIKU YA SITA MFUNGO TATU Mtume (S.A.W.)asema kuwa:-Ni siku ambayo  Mwenye-ezi Mungu alimfungulia Mtume wake (Muhammed (S.A.W.)  )kheri".Mwenye kufunga siko hiyo, Mwenye-ezi Mungu humuangalia kwa  jicho la huruma wala hapati adhabu siku ya kiyama.

 
 SIKU YA SABA YA MFUNGO TATU Mtume asema kuwa:-"Ni siku ambayo  Milango ya Jahannam(Moto)hufungwa na hayafunguliwi hadi masiku kumi  yatimie".Mwenye kufunga Mwenye-ezi Mungu humfungia Milango  thelathini ya mambo mazito na humfungulia Milango thelathini ya  mambo mepesi.

 SIKU YA NANE YA MFUNGO TATUMtume(S.A.W.)asema kuwa:-"Ni siku  iitwayo  Tar-wiya".Mwenye kufunga hupewa malipo ambayo hakuna ayajuwaye  isipokuwa Allah SWT.

 SIKU YA TISA YA MFUNGO TATUMtume(S.A.W.)asema kuwa:-"Ni siku  iitwayo  Arafat".Mwenye kufunga siku hiyo, hufutiwa makosa ya mwaka  uliopita, na utakao kuja.

 SIKU YA KUMI YA MFUNGO TATU:- Mtume(S.A.W.)asema kuwa:-"Ni siku ya  kuchinja Mnyama(itakuwa Iddi Kubwa), tone la kwanza la damu  litakapo tona Mwenye-ezi Mungu humsamehe dhambi zake na za jamaa  zake. Na mwenye kumpa chakula Masikini au akatowa sadaka siku hiyo,  Myenye-ezi Mungu atamfufua siku ya Kiyama kwa amali na mizani ya  uzito, thawabu zake zitashinda uzito wa Mlima Uhud".

  
PLEASE DO NOT FORGET TO ENLIGHTEN OTHER MUSLIMS BY FORWARDING THIS  MAIL

   
 
 
JIBU Kutoka alhidayah
 
Sifa zote njema Anastahiki Allaah Aliyetukuka Mola Mlezi wa walimwengu wote, Swalah na salamu zimshukie kipenzi chetu Mtume Muhammad (Swalla Allaahu 'alayhi wa  aalihi wasallam) na Swahaba zake (Radhiya Allaahu 'anhum) na watangu wema mpaka Siku ya Mwisho

 

Tunasikitika kwamba siku hizi fitna za kusambaza uzushi zimezidi kutokana na wepesi wa mawasiliano kupitia barua pepe (e-mail), simu za mkononi n.k. Jambo linaloshangaza ni kwamba Hadiyth zilizo Sahihi zimejaa tele lakini hizo hazisambazwi kama zinavyosambazwa za uzushi. Ni dhahiri kwamba wanaofanya hivyo ima hawajui tofauti ya mafunzo sahihi na yale potofu ima kwa uchache wa elimu, au kwa pupa tu za kutafuta thawabu kwa njia za mkato ndiko kunakowasababisha wao kueneza haya mambo yasiyo na dalili wala asili. Lakini wanaghafilika ndugu hao kutambua madhara yanayopatikana kutokana na hayo wanayoyaeneza kila mara.

Moja ya madhara makuu ni kupoteza mafundisho sahihi ya Dini yetu, na kueneza ya uongo na hivyo kutawala upotofu katika jamii ya Kiislam, Kwani kama wanavyosema wema waliotangulia, kuwa, bid’ah inavyoenea, ndio Sunnah hupotea.

Tumepekuwa vitabu mbalimbali vya Hadiyth vikubwa na mashuhuri na hakuna hata sehemu moja tuliyokuta kuna Hadiyth inayotaja Fadhila za masiku kumi ya Dhul-Hijjah kwa mtindo huo na kwa maelezo hayo! Vilevile Maulamaa waliowahi kukumbana na maelezo hayo, wamesema kuwa ni ‘Mawdhuw’ – yaani ya kutungwa na si ya kweli.

Kuna hatari vilevile ya watu kutumbukia katika maonyo na makemeo aliyoyatoa Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam):

((من كذب علي متعمدا فليتبوأ مقعده من النار)) متفق عليه

((Atakayeniongopea makusudi basi ajitayarishie makazi yake motoni))  [Al-Bukhaariy Na Muslim]

Ukiwa umeeneza mambo hayo na hali unajua kuwa si sahihi, basi tambua kuwa ushaingia katika walioelezwa ndani ya Hadiyth hiyo.

 

Na ikiwa una mazoea ya kueneza au kutuma kila unachopata ukidhani utapata thawabu kwa kufanya hivyo na hali huna uhakika nacho, au huna elimu ya jambo hilo kama ni sahihi au la, basi utakuwa pia una majukumu kwa kuwa Uislam umesisitiza sana elimu na umuhimu wa kuitafuta; hivyo kwanini ubakie katika ujinga na kutokufahamu unayotuma? Pia ikiwa hujui, ushaelezwa na Allaah (Subhaanahu wa Ta’ala) uulize wenye elimu na upambuzi, je, ulijaribu kufanya hayo kabla hujasambaza mambo hayo ya kutunga yenye kupotezea Waislam muda, juhudi, na hata ‘amali zao kwa kufanya yasiyo sahihi na yasiyo katika mafundisho ya Dini?

 

Na madhara mengine ni kwamba dhambi za mwenye kueneza uzushi huzidi kila uzushi unapozidi kusambaa na mwenye kuanza kueneza uzushi hubeba dhambi za kila mtu anayepokea na kujifunza uzushi huo:

 عن أبي هريرة رضي الله عنه عن النبي صلى الله عليه وسلم أنه قال : ( من دعا إلى هدى كان له من الأجر من أجور من تبعه لا ينقص من أجورهم شيئاً ومن دعا إلى ضلالة كان عليه من الإثم مثل آثام من تبعه لا ينقص ذلك من آثامهم شيئاً)   رواه مسلم  

Kutoka kwa Abu Hurayrah (Radhiya Allaahu ‘anhu) kwamba Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) kasema: ((Atakayelingania kwenye uongofu atapata thawabu (ujira) wa yule atakayemfuata bila ya kupungukiwa chochote katika thawabu zao. Na atakayeelekeza katika upotofu atapata dhambi mfano wa dhambi za yule atakayefuata bila ya kupungukiwa chochote katika dhambi zao)) [Muslim]

Tumefanya utafiti mkubwa kutafuta kauli kama hizo kuhakikisha kama ipo kauli ya Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) inayotaja fadhila za siku hizo kama zilivyotajwa humu lakini hatukupata. Mojawapo ya matokeo ya utafiti ni kupata fatwa kutoka kwa Maulamaa kutoka Markaz ya Fataawa walioulizwa kuhusu ujumbe huo nao pia wamehakikisha kuwa ni uzushi usio na dalili yoyote [Markaz al-Fataawa 24 Dhul-Hijjah 1424/16-02-2004].

Tunawanasihi ndugu zetu Waislamu wasome mada muhimu katika kiungo kifuatacho ili watambue hatari ya kueneza uzushi:

 
Hatari Ya Kueneza Hadiyth Dhaifu Na Visa Vya Uongo

Vilevile mtu anatakiwa asome mada hii hapa chini yenye kuhusu uzushi wenye kufanana na huo:

 

Uzushi Unaodaiwa Kuhusu Mambo Yaliyotokea Siku Ya Ashuraa Tarehe 10

 

Jambo jingine muhimu tunalopenda kuwatanabahisha ni kuhusu jinsi hayo majina ya miezi ya Kiislam yanavyoitwa au yalivyozoeleka kuitwa kama tulivyoona kwenye huo ujumbe wa kutungwa kwa jina la mfungo mosi, mfungo pili, mfungo tatu n.k., hakika ni majina yaliyozoeleka lakini si sahihi kwani yanapoteza ufahamu wa majina sahihi na mpangilio wa hiyo miezi ya Kiislam. 

Miezi ya Kiislam hujulikana mwezi wa kwanza kama ni Muharram lakini wao huo mwezi wa kwanza umeitwa ni mfungo nne, na mwezi wa Dhul-Hijjah ambao ni mwezi wa kumi na mbili, wao wanauita mfungo tatu! Hivyo Waislam wengi hudhani kuwa huu mwezi wa 12 wa Dhul-Hijjah tulionao sasa kuwa ni mwezi wa 3 badala ya 12. Kutoka katika mpango uliowekwa na Uislam na kufuata mipango na taratibu za kimila na kitamaduni, kunasababisha mafunzo ya Dini kutofahamika kamwe, au kusahaulika kabisa. Leo hii, Waislamu wengi Waswahili hawajui miezi ya Kiislam kwa majina yake ingawa wengi wanaijua hiyo ‘mifungo’. Huo ni ukweli wenye kusikitisha. Na wengi huita kalenda na tarehe za Kiislam kuwa ni tarehe za Kiarabu badala ya Kiislam; ilihali kuna tofauti kubwa kati ya Uislamu na Uarabu. Miezi ya Kiislam ni hiyo tuliyozungumzia hapo juu na tutaweka chini kabisa mpangilio wake wa majina ya miezi yote ya mwaka mzima. Kalenda au tarehe za kiarabu ni tofauti na za Kiislam na mtu akitaka kujua atazame magazeti ya Kiarabu ataona tofauti. Hivyo, Waislam wajizoeshe kuita tarehe za Kiislam au miezi ya Kiislam na si ya Kiarabu, maana kuna Wakristo Waarabu nao hawafuati kalenda yetu ya Kiislam.

Miezi Ya Kiislam (Kila Muislam Ajitahidi Kuijua Na Kuihifadhi)

1- Muharram محرّم

2- Swafar صفر

3- Rabiy’u al-Awwal ربيع الأول

4- Rabiy’u ath-Thaaniy au Rabiy’u al-Aakhirربيع الآخر  أو ربيع الثاني

5- Jumaada al-Uwlaa جمادى الأول

6- Jumaada ath-Thaaniy au Jumaada al-Aakhir جمادى الآخر  أو جمادى الثاني

7- Rajab رجب

8- Sha’abaan شعبان

9- Ramadhaan رمضان

10- Shawwaal شوّال  

11- Dhul-Qa’adah ذوالقعدة

12- Dhul-Hijjah ذوالحجة

Inasikitisha sana kuona Muislam

 kahifadhi miezi yote ya kikafiri, lakini hawezi kutaja hata miezi sita ya Kiislam. Sana sana utakuta Muislam anajua ile miezi ya karibu na Ramadhaan kama Rajab, Sha’abaan na pia labda mwezi huu wa Dhul-Hijjah na wengine huujua Rabiy’ul al-Awwal kwa sababu ya kusherekea tu Mawlid na huenda asijue kuwa ni Rabiy’u al-Awwal, bali atakuwa anaujua kwa jina la kijamii ‘Mfungo sita’! Huu ndio msiba tulionao Waislam, inatubidi tuamke hivi sasa na tuzindukane na usingizi wa miaka na miaka. Na silaha pekee ya kuzindukana na hayo, ni ELIMU SAHIHI ya Dini.

Pia tunawaomba ndugu zetu kwamba wanapopata jambo lenye shaka kwanza wawe wanahakikisha kabla ya kutuma kwa wenzao kwani tutambue kuwa Muislamu inapomfikia kauli inayodaiwa kuwa ni ya Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) basi imeshakuwa ni waajib kwake kuhakikisha. Akipata dalili ya usahihi wake atume kwa wenziwe kama tunavyoamrishwa kufikisha kwa wengine japo Aayah moja na kuamrishana mema na kukatazana maovu. Lakini ikiwa hakupata dalili yake ni bora kuacha kutuma kuliko kuleta madhara ya uzushi na kuzidisha ufisadi katika dini na jamii kwa ujumla kwa kupoteza mafunzo sahihi na kueneza mafunzo ya uzushi.

Kidokezo Cha Kuweza Kutambua Hadiyth Zisizo Sahihi Au Ujumbe Wa Uongo:

Ndugu Muislam, ukitaka kugundua haraka ujumbe ulioupata kwenye barua pepe (e-mail) au ujumbe kwenye simu za mkono, kwanza kitakachokujulisha kuwa ujumbe huo una utata na sio sahihi, ni kuwa, mara nyingi maelezo yaliyomo ndani ya ujumbe huo zikiwemo zinazosemwa ni Hadiyth, utakuta hazitajwi zilipotolewa, kama ni Hadiyth utaona haisemwi nani kasimulia, nani kapokea, kitabu gani, hakuna hata Imaam wa Hadiyth (Muhaddith) aliyetajwa kwenye Hadiyth hiyo n.k. Hayo yote yanatosha kumtia mashaka mtu kuhusiana na alichokipokea. Hivyo, endapo utapokea ujumbe au Hadiyth ambayo imekuja tu na kudaiwa kasema Mtume, bila kutajwa zaidi ya hivyo… basi mrudishie aliyekutumia na muombe akueleze Hadiyth hiyo iko kwenye kitabu kipi, na nani kaisimulia na kama ni sahihi au dhaifu. Usiwe na pupa ya kueneza au kusambaza kwa wengine hadi kwanza upate uhakika 100%. Vilevile unaweza kutuandikia maswali@alhidaaya.comkuulizia masuala kama hayo na inshaAllaah tutakusaidia haraka katika masuala hayo.

 

Na Allaah Anajua zaidi

Monday 8 September 2014

17 Rules of Islamic Dream Interpretations


Ibn Qutaybah ad-Dinawari رحمه الله says in his book about dream interpretations, “There is nothing in which people deal with from the different sciences that is more obscure, delicate, exalted, noble, difficult and problematic than dreams because they are a type of revelation and type of Prophethood.”

Narrated Anas bin Malik رضي الله عنهAllah’s Messenger صلى الله عليه و سلمsaid, “A good dream (that comes true) of a righteous man is one of forty-six parts of prophet hood.” [Sahih al-Bukhari]

Some scholars tried to give explanation to this ratio of 1:46. We have no way to find out that if their explanation is correct or not. Prophet hood of Prophet صلى الله عليه و سلم extended from 40 to 63 years meaning for 23 years. We know from Seerah that six months before becoming a Prophet, Messenger of Allah صلى الله عليه و سلمwas seeing dreams that would come out to be true on a very frequent basis so much so that he would see a dream one night and it would come to be true the next morning. So the ratio of 6 months to 23 years is 1:46.

1) There are 3 types of dreams: Imam at-Tirmidhi رحمه الله narrates from Muhammad Ibn Sirin رحمه الله who narrates from Abu Hurairah رضي الله تعالى عنه that Prophet صلى الله عليه وسلم said, “There are three types of dreams: 1) True Dreams 2) A dream in which a person is speaking to himself (i.e. whatever you were thinking about in the day time, you see at night) 3) A dream from shaytaan in which he wants to make you sad ”

In one hadith it is mentioned that one should stand up and pray and in another the he should not mention it to anyone.

Abu Salamah رضي الله عنه once said, “Sometimes I would see a dream that would be heavier on me than carrying a mountain. But since I heard this hadith I wouldn’t care about the bad dream I would see.”

Narrated Abu Sa‘id Al-Khudri رضي الله عنه: The Prophet صلى الله عليه و سلم said, “If anyone of you sees a dream that he likes, then it is from Allah, and he should thank Allah for it and narrate it to others; but if he sees something else, i.e., a dream that he dislikes, then it is from Satan, and he should seek refuge with Allah from its evil, and he should not mention it to anybody, for it will not harm him.” [Sahih Muslim]

Q1) A question arises, is every dream that a believer sees good?

A1) Al Muhallab رحمه الله says, “Most of the dreams of the righteous people are good dreams because sometimes a righteous person could see a dream that is meaningless but that is not very frequent because shaytaan’s control on them is very weak. And the opposite is true with other people because shaytaan has a stronger grasp over them. People are of the categories:

1) The Prophets: all of their dreams are truthful and but sometimes they need interpretation. The good dream is divided into 2 categories:
a) Direct dream: something one would see in a dream and the exact scene repeats itself in day-time when you are awake and this dream does not need interpretation.
b) A dream the comes in symbols and it needs to be interpreted.

2) The righteous: most of the time their dreams are truthful (most of them need to interpreted) and sometimes their dream are direct.

3) Rest of the people: most of their dreams are not true but some of them could be true.” [Fath al-Bari bi Sharh Sahih al-Bukhari]

2) Do not mention the dream for interpretation except to a scholar or a person who would advise you sincerely.

Prophet صلى الله عليه و سلم said, “You should not mention this dream to an envious person…”

There is also evidence for this in the Qur`an: (Remember) when Yûsuf (Joseph) saidto his father: “O my father! Verily, I saw (in a dream) eleven stars and the sun and the moon, I saw them prostrating themselves to me.” He (the father) said: “O my son! Relate not your vision to your brothers, lest they arrange a plot against you. Verily! Shaitân (Satan) is to man an open enemy! {Surat al-Yusuf, ayatyn 4-5}

3) Seeing Prophet صلى الله عليه و سلم:

Narrated Anas رضي الله عنه the Prophet صلى الله عليه و سلم said, “Whoever has seen me in a dream, then no doubt, he has seen me, for Satan cannot imitate my shape. [Sahih al-Bukhari]

Q2) There is an issue here, what if a person sees Prophet صلى الله عليه و سلم and he feels that it is him but his description in the dream if different than the one we know of from ahadith. So is the person in the dream Prophet صلى الله عليه و سلم?
A2) Az-Zuhri رحمه الله says that Ibn Sirin رحمه الله said, “If you see him according to his description.” An-Nawawi رحمه الله, however, has a contrary view and he says, “As long as you felt in your dream that the person you saw was Prophet صلى الله عليه و سلم then it is him even if he comes in a different form.” Ibn Taymiyyah رضي الله عنه supports the view of Ibn Sirin رحمه الله

4) A repetition of a dream is a sign of its truth. It does not matter if the same person sees the dream more than once or more than one person.

‘AbduLlah ibn ‘Umar رضي الله عنهما reported that some people were shown the Night of Qadr as being in the last seven days (of the month of Ramadan). The Prophet صلى الله عليه و سلم said, “I see that your dreams strengthen each other that Night of Qadr is in the last seven nights of Ramadhan so whoever searches for it, would search for it in the last seven days (of Ramadan).” [Sahih al-Bukhari]

Also the dream about Adhan when 2 Sahabah ضي الله عنهما saw the same dream.

5) Q3) When is the most expected time to see a righteous dream? At night or day time? Are all the times equal (whether seen at the beginning of the night or end of the day)?

A3) Ibn Sirin رحمه الله said, “Dreams of day time are equal to the dreams of night.” [Sahih Muslim]

6) Ibn Battal رحمه الله said, “Dreams are of two types: a clear evident dream like somebody would dream about himself giving dates to someone and during the day time he would give somebody dates. This type of dream doesn’t need any interpretation. Secondly, a dream that comes in symbols and this type you would understand its meaning unless you get it interpreted by a person who has knowledge and experience dream interpretation because sometimes the symbols are very delicate and sophisticated.”

Like the dream Prophet صلى الله عليه و سلم saw in which he was drinking milk from a vessel and when some of it was remaining, he gave it ‘Umar رضي الله عنه. Prophet صلى الله عليه و سلم interpreted it as knowledge. This means that Prophet صلى الله عليه و سلم absorbed the knowledge and he mentions that the milk was so much that it started flowing beneath his nails. So he had so much knowledge in him, that it started flowing from him.

7) Dreams can be about the past or the present or the future.

8) True dreams increase towards the end of times.

Ibn Sirin رحمه الله said,” I heard Abu Hurairah saying, ‘Prophet صلى الله عليه و سلم said, “When Time approaches, the dream of the believer rarely would lie.’” [Sahih al-Bukhari]

“When Time approaches…”is explained in two different opinions:

1)Al-Khattabi رحمه الله said, “The meaning of ‘When Time approaches…” is the time of night and the time of day. When the time of night approaches the length the time of day, then the dreams of the believer will be true. These are the two times when flowers open up and when fruits are ripe. The scholars of dream interpretation actually state that these are the two time when the dreams are most likely to be true.”

2)Al-Qurtubi رحمه الله says, “What is meant by this hadith, and Allah سبحانه و تعالى knows best, is the end of times and it is talking about the group of believers that will be with ‘Isa ibn Maryam عليه سلام after he kills dajjal.”

Ibn Abi Jamrah رحمه الله says,” The reason why the believer sees true dreams at the time is because the believer will be ghareeb (stranger) as was mentioned in the hadith, ‘Islam began as something strange and it will return to the way it began being strange so give glad tidings to the strangers so give glad tidings to the strangers.’”

Ibn Hajar al-‘Asqalani رحمه الله comments on all the opinions by saying, “Whenever the times are difficult for the believer, he will see dreams that are true frequently because he needs help. When the believer is alone, when the times are difficult, when you don’t find people supporting on truth, then Allah سبحانه و تعالى will inspire you to give you glad tidings through the good dreams you would see and this is to give the believers in those difficult and testing times gives the believers strength, it gives them confidence, it gives them hope so they would see a lot of dreams that would come true.”

For example the brothers who are doing Jihad feesabiliLlah see a lot of dreams that come out to be true because they are being tested by Allah سبحانه و تعالى thus He assists them.

9) Most of the times, if the dream is a glad tiding from Allah سبحانه و تعالى it would take a long for it to occur while if it is a warning it would occur swiftly.

For example Yusuf عليه سلام’s dream took a very long time for it to happen around 40 years. Some scholars say this is because Allah سبحانه و تعالى gives the believer glad tidings early on to give him confidence and hope, to inspire him in his life. While if it is a warning, you would see it and it would occur very soon so that it would be the reason of fear in your heart.

10) Dreams are glad tidings and warnings but can not be used as a source of Shari‘ah.

Ash-Shatbi رحمه الله says regarding this, “Benefit of the dream in giving the believer a glad tiding or warning not in legislation and judgement or rulings.”

11) If one sees a dream that is very long like a movie or someone is chasing you and it never ends then most likely that dream doesn’t mean anything. True dreams are short and concise.

12) The dream of a believer pleases him but it does not make him proud or over confident.

Ibn Muflih رضي الله عنه mentions in his book Adaab ash-Shar‘iyah, “Ibrahim al-Humaydi was righteous man and Imam Ahmad bin Hanbal visited him so Ibrahim told Imam Ahmad, ‘My mother has seen a dream for you where she saw this-and-that for you,’ and then he mentioned Jannah. Imam Ahmad said, ‘My brother, Sahl ibn Salamah, people used to see dreams for him similar to what you mentioned and in the end he ended up shedding blood so the dream pleases the believer, it doesn’t make him boastful.”

13) Dream interpretation is not certain but presumptive and Allah سبحانه و تعالى says in Surah Yusuf: “And he said to the one he presumed to be saved…” {ayah # 42}

Ibn Kathir رحمه الله mentions in his An-Nihayah wal Bidayah that there was a caliph (not a good one) of Ibn ‘Abbas who saw dream that he was climbing a dream with 28 steps. So he had that dream interpreted. The one who interpreted his dream told him that the meaning of this dream is, “You will rule for 28 years.” But he died six months later. He died at the age of 28 so the steps were representing his age not the time for his rule.

There was a woman who dreamt that her daughter would break three banners (flag carried in war time). So she went to Ibn Sirin رحمه الله and he interpreted that dream saying, “If her dream is true, it means that she would marry three noble men all of them would be killed.” When her daughter grew up, she married Yazid ibn al-Muhallab who was a great leader in ‘Iraq and he was killed. Later on, she married ‘Amr ibn Yazid at-Taymi and he was killed. Her third marriage was with al-Hasan ibn ‘Uthman ibn ‘Abdur Rahman ibn ‘Awf رحمه الله, the grandson of the Sahabi ‘Abdur Rahman bin ‘Awf. She had an argument with him and she told him, “In the Name of Allah, you would be killed.” He asked her the reason and she told him about her dream. He said, “Alright, I am going to divorce you since you think I am going to be killed now!” Finally, she married al-‘Abbas ibn ‘AbdiLlah ibn Harith ibn Nawfal ibn Harith ibn ‘Abdul Muttalib and he was killed.

One man saw in a dream, during the plague, that caskets were coming out of his house and the number of them was equal to the number of his family. So, he interpreted the dream that his entire family would be killed in the plague. And the dream started to manifest itself. His family were dying one after the other and all the bodies were coming out of his house exactly how he saw in his dream until he was the last member of his family left so he was pretty sure that he would be killed by the plague because his dream was, until now, true. But a thief came into his house and was struck by the plague, he fell ill in his house, he died and he was the last body to leave the house and not the person who saw the dream.

14) It is haram and a great sin to claim that one has a seen a dream whilst he has not seen it or to lie in it.

Narrated ‘AbduLlah ibn ‘Abbas رضي الله عنه that the Prophet صلى الله عليه و سلم said, “Whoever claims to have seen a dream that he has not seen, would be told to tie between two hairs on the Day of Judgement.”

15) A dream could be seen by a person but it could be for someone else.
Al Hakim and ‘AbduLlah Ibn Mubarak narrate that someone saw a dream for Abu Jahl that he became a Muslims and pledged allegiance to Prophet صلى الله عليه و سلم. But this never happened. So this dream was for his son, ‘Ikrimah رضي الله عنه who became a Muslim and pledged allegiance to Prophet صلى الله عليه و سلم later on.

A dream was seen for Usayd bin Abil ‘Aas that he became the governor of Makkah and he never did but his son ‘Attab became the governor of Makkah.

16) Same symbol in a dream could mean different things for different people

For example: A man came to Ibn Sirin رحمه الله and told him that he had seen himself in a dream giving Adhan. Ibn Sirin رحمه الله replied, “You will make Hajj.” Another man came with the same dream and Ibn Sirin رحمه الله replied, “You are a thief!” Ibn Sirin رحمه الله was asked the reason of him giving different interpretations of the same dream to different people and he said, “Because I saw in the first man’s face righteousness and Allah سبحانه و تعالى says in the Qur`an that Ibrahim عليه سلام made adhan calling people to Hajj so I interpreted this mean that this person would make Hajj. Whilst I saw evil on the face of the other man and Allah سبحانه و تعالى says in Surah Yusuf, ‘then a crier cried: ‘O you (in) the caravan! Surely, you are thieves!’ so I interpreted it to mean that this person is a thief.’”

17) Prophet صلى الله عليه و سلم said, “A dream is hanging on the leg of a bird (and in another narration on the wing of the bird) as soon as it is interpreted, it happens as it was interpreted.” So some scholars say that if you take your dream to a scholar, it would happen as it is interpreted by him so that’s why you must take it to a person who has knowledge about dream interpretation and or a person who would give you a sincere advice and not to the person who is envious so if the dream is interpreted it would happen as he interpreted.

However,

there is a difference of opinion regarding this issue.

And Allah سبحانه و تعالى knows best.

Source: Islam best Religion website.

Friday 1 August 2014

SIKU YA IJUMA NA HUKMU ZAKE

Makala hii imetaarishwa na swahiliminbar.com

Siku ya Ijumaa, ni siku bora kabisa iliyotokewa na jua. Katika siku hii Mwenyezimngu Alimuumba Adam,na Kiyama kitasimama siku ya ijuma, na ni siku ya Idi kwa Waislamu. Kwa hivyo, yameamrishwa baadhi ya mambo katika siku, miongoni mwao: hutuba ya Ijumaa,kuoga, kujitia manukato, kwenda Ijumaa kwa kuvaa vazi zuri zaidi napambo zuri zaidi, kwenda Ijumaa mapema, kukaa karibu na imamu na kuutayarisha moyo kusikiliza mawaidha na utajo wa Mwenyezi Mungu.

Utangulizi

 Enyi watu, Mcheni Mwenyezi Mungu (Subhaanahu wa Taala). Na mjuwe ya kuwa hakika Mwenyezi Mungu (Subhaanahu wa Taala) huumba atakavyo na huchagua atakavyo. Amesema Mwenyezi Mungu (Subhaanahu wa Taala):

قال تعالى: {وَرَبُّكَ يَخْلُقُ مَا يَشَاءُ وَيَخْتَارُ مَا كَانَ لَهُمُ الْخِيَرَةُ  } [القصص: 68]

{{ Na Mola wako huumba atakavyo na huchagua atakavyo,  hawana viumbe hiari}}.. Na Mwenyezi Mungu (Subhaanahu wa Taala) ndie anaye jua hekima kwa kila kitu anacho kichagua miongoni mwa viumbe vyake.  Mwenyezi Mungu (Subhaanahu wa Taala) huchagua Mitume miongoni mwa Malaika na watu. Na Mwenyezi Mungu (Subhaanahu wa Taala) ameufadhilsha Mji wa Makka kushinda sehemu nyingine. Na akauchagua Mji wa Madina kuwa ni mji aliohamia Mtume (Swalla Llahu ‘alayhi wasallam) na Masahaba. Kisha akauchagua Baytul Maqdis akajalia ni sehemu ya Mitume wengi ambayo Mwenyezi Mungu (Subhaanahu wa Taala) ametuelezea habari zao katika Qur’an Tukufu. Na Mwenyezi Mungu (Subhaanahu wa Taala) amefadhilisha baadhi ya Miezi kuliko mingine na Usiku na Mchana. Akachagua Miezi mine Mitukufu (Dhul-qa’ada, Dhul-hijja, Muharam na Rajab). Na bora wa masiku ni siku ya Ijumaa. Kwa hivyo, mtukuzeni Allah (Subhaanahu wa Taala) na kumsifu na kumsalia Mtume Muhammad (Swalla Llahu ‘alayhi wasallam).

Hukumu ya Swala ya Ijumaa

Swala ya Ijumaa ni miongoni mwa swala muhimu za faradhi. Na sharia imetia mkazo zaidi na kusisitiza kutekelezwa swala ya ijumaa kwa jamaa. Na malipo yake ni makubwa zaidi.

Fadhila za siku ya Ijumaa:

1.      Kupata Thawabu na Malipo kwa kila hatua ya kwenda Msikitini sawa na Mtu aliyesimama kuswali na kufunga Mwaka mzima. Amesema Mtume (Swalla Llahu ‘alayhi wasallam) : [ Mwenye kuoga na kujisafisha, kisha akaenda Msikitini na mapema na akamkurubia Khatibu na akasikiliza kwa utulivu. Mwenyezi Mungu (Subhaanahu wa Taala) atamlipa kwa kila hatua malipo sawa na Mtu aliyesimama kuswali na kufunga Mwaka mzima] (Imepokewa na Ahmed).

2-     Kusamehewa Madhambi yake ya wiki mzima pamoja na siku tatu za ziada. Amesema Mtume (Swalla Llahu ‘alayhi wasallam) : [ Mwenye kutawadha vizuri, kisha akaja Msikitini na akamsikiliza Khatibu na kunyamaza. Anasemehewa Madhambi yake ya wiki mzima pamoja na siku tatu]. Imepokewa na Muslim.

3-                 Kukubaliwa dua katika siku hii tukufu. Amesema Mtume (Swalla Llahu ‘alayhi wasallam) : [Hakika katika Siku ya Ijumaa kuna wakati, haafikiwi Muislamu na wakati huo hali akiwa anamuomba Allah, ila Mwenyezi Mungi humkubalia Dua yake].

Adabu na Sunna za Siku ya Ijumaa:

-           Kuoga na kujisafisha na kupaka manukato mazuri pamoja na kuondosha harufu mbaya mwilini.. Amesema Mtume (Swalla Llahu ‘alayhi wasallam) : [Mwenye kuoga siku ya Ijumaa, kisha akaenda Msikitini na mapema. Mfano wake ni kama mtu aliyetowa sadaka ya Ngamia].

-          Kwenda Msikitini mapema na kumkurubia khatibu. Amesema Mtume (Swalla Llahu ‘alayhi wasallam) : [Nedeni mkasali sala ya Ijumaa, na mkae karibu na khatibu].

-           Kujishughulisha kwa Kumtaja Allah, kusoma Qur’an, kuomba msamaha, kuomba dua kwa wingi na kumsalia Mtume Muhammad (Swalla Llahu ‘alayhi wasallam).

-          Kumsilikiza Khatibu kwa utulivu, bila ya kujishughulisha na mambo mengine.Asema Mtume (Swalla Llahu ‘alayhi wasallam) : [Mwenye kutawadha vizuri, kisha akaja Msikitini na akamsikiliza Khatibu na kunyamaza. Anasemehewa Madhambi yake ya wiki mzima pamoja na siku tatu]. Imepokewa na Muslim.

Mambo yalio katazwa katika swala ya Ijumaa:

-          Kuja Msikitini kuchelewa na kukata safu kwa kuruka watu, kwa lengo la kutaka kukaa safu ya mbele. Siku moja Mtume (Swalla Llahu ‘alayhi wasallam) alimuona mtu akikata safu na kuruka watu; Akamuambia kaa chini kwa hakika umewaudhi watu na umefanya maasi makubwa.
-          Kuwashawishi waja wa Mwenyezi Mungu, kwa kusoma Qur’an kwa sauti kubwa, au kufanya Dhikri kwa sauti ya juu. Mtume (Swalla Llahu ‘alayhi wasallam) aliwakataza Masahaba kusoma kwa sauti ya juu, na akawambia; Asisome mmoja wenu Qura’n kwa sauti ya juu kuliko mwingine.
-          Kuzungumza wakati wa Khatibu anatoa khutbah ya Ijumaa.  Amesema Mtume (Swalla Llahu ‘alayhi wasallam) : [Ukimuambia mwenzako nyamaza na Khatibu akiwa anazungumza, kwa hakika umeharibu swala ya Ijumaa].

Khatari ya kuacha kuswali swala ya Ijumaa

Mtume Muhammad amesisitiza na kutilia mkazo juu la suala la kutekeleza swala ya Ijumaa. Na akawatahadharisha Waislamu wanaoacha kutekeleza swala hii. Adhabu kubwa watakayo pata watu hao hapa duniani ni nyoyo zao kuwa ngumu na kupigwa muhuri wa kughafilika. Amesema Mtume (Swalla Llahu ‘alayhi wasallam):  [ Hawataendelea watu kuacha  swala ya Ijumaa, mpaka Mwenyezi Mungu apige muhuri nyoyo zao, kisha watakuwa niwenye kuishi katika mughafala].

 Ndugu Waislamu, tujihadhari sana na kuacha swala ya Ijumaa, kwasababu adhabu yake ni nzito sana. Moyo ukiwa mgumu, basi mwanadamu anakuwa sawa na myama, hajali lolote wala chochote. Utamuona hamuogopi Mwenyezi Mungu, kwa kufanya maasi usiku na mchana.

 Tunamuomba Allah (Subhaanahu wa Taala) athibitishe nyoyo zetu juu ya twaa yake, na atulinde na machafu yote.

KHUTBA YA PILI

Ndugu Waislamu, katika  Mafundisho ya Mtume Muhammad (Swalla Llahu ‘alayhi wasallam) ni kuitukuza siku hii ya Ijumaa, kwani hii ni siku tukufu ilio chaguliwa na Mwenyezi Mungu (Subhaanahu wa Taala) na kupatiwa Umma huu wa mwisho.

Mtume Muhammad (Swalla Llahu ‘alayhi wasallam) alikhusisha baadhi ya vitendo katika siku ya Ijumaa:
-          Kusoma Surat Sijdah na Surat Insaan katika swala ya Al-Fajiri. Imepokewa na Abu Hureirah – Radhi za Allah ziwe juu yake- { Alikuwa Mtume akisoma katika swala ya Al-Fajri siku ya Ijumaa (Surat Sijdah) katika rakaa ya kwanza. Na katika rakaa ya pili (Surat Insaan) } Muslim.
-          Kusoma Surat Al-Kahfi. Amesema Mtume (Swalla Llahu ‘alayhi wasallam): {Mwenye kusoma  Surat Al-Kahfi  siku ya Ijumaa, Mwenyezi Mungu anampa mwangaza baina ya Ijumaa mpaka Ijumaa nyingine}. Al-Bayhaqi na Haakim.

-          Kuzidisha kwa wingi kumsalia Mtume Muhammad (Swalla Llahu ‘alayhi wasallam). Amesema Ibnu-Qayyim: “Mtume wa  Mwenyezi Mungu ni Bwana wa viumbe vyote, na siku ya Ijumaa ni bwana wa siku zote. Kumswalia Mtume siku hii ina malipo mengi kushinda siku nyingine”.
-          Kuzidisha kumuomba Allah (Subhaanahu wa Taala) katika siku hii. Kwasababu kuna wakati wa kukubaliwa dua ya Muislamu. Amesema Mtume (Swalla Llahu ‘alayhi wasallam) : [Hakika katika Siku ya Ijumaa kuna wakati, haafikiwi Muislamu na wakati huo hali akiwa anamuomba Allah, ila Mwenyezi Mungu humkubalia Dua yake].

Mwisho

Ndugu katika Imani, kama tulivyo sikia umuhimu wa siku ya Ijumaa, na namna sheria ilivyo tilia mkazo siku hii. Na vilivile malipo na thawaabu nyingi kwa Yule atakae tekeleza ibada kwa masharti yake na nguzo zake. Ni jukumu letu kufanya bidii kwa kufanya ibada mbali mabali kama alivyo tufundisha Mtume (Swalla Llahu ‘alayhi wasallam), ili tuweze kupata malipo na thawabu nyingi kutoka kwa Allah (Subhaanahu wa Taala).  Enyi Waislamu, Tushindaneni kufuata Sunna na Mafundisho ya Mtume (Swalla Llahu ‘alayhi wasallam) katika siku hii kuu.

Mwenyezi Mungu atujaalie miongoni mwa waja wake wema na atupe uwezo wa kufuata Sunna za Mtume (Swalla Llahu ‘alayhi wasallam). Tunamuomba Allah atukubalie  ibada zetu na atupe mwisho mwema tukiondoka duniani.

Monday 21 July 2014

Dua za Mtume Muhammad s.a.w


Du’aa katika Sunnah ziko nyingi sana. Aghlabu ya du’aa za Mtume (صلى الله عليه وسلم) zilikuwa za mukhtasari wa maneno kwa maana kauli zake fupi lakini zenye maana tele na hikma kama alivyosema mwenyewe katika usimulizi ufuatao:

عَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ (رضي الله عنه) أَنَّ رَسُولَ اللَّهِ (صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ) قَالَ: "فُضِّلْتُ عَلَى الأَنْبِيَاءِ بِسِتٍّ: أُعْطِيتُ جَوَامِعَ الْكَلِمِ, وَنُصِرْتُ بِالرُّعْبِ, وَأُحِلَّتْ لِيَ الْغَنَائِمُ, وَجُعِلَتْ لِيَ الأَرْضُ طَهُورًا وَمَسْجِدًا, وَأُرْسِلْتُ إِلَى الْخَلْقِ كَافَّةً, وَخُتِمَ بِيَ النَّبِيُّونَ

Imepokewa kutoka kwa Abu Huraryah (رضي الله عنه) kwamba Mtume (صلى الله عليه وسلم) amesema: ((Nimefadhilishwa juu ya Manabii kwa mambo sita; nimepewa ‘Jawaami’al-Kalimi’[1] na nimenusuriwa kwa [kutiwa] hofu [katika nyoyo za maadui] na nimehalalishiwa ghanima[2] na nimefanyiwa ardhi kuwa kitoharishi na masjid [mahali pa kuswali], na nimetumwa kwa viumbe wote, na Manabii wamekhitimishwa kwangu))[3]

Tunazigawanya Du’aa hizo katika maudhui mbali mbali na kutokana na hali zinazomkabili Muislamu:

-Du’aa Alizokuwa Akiomba Sana Mtume (صلى الله عليه وسلم )

Kuomba kheri za dunia na Akhera

رَبَّنَا آتِنَا فِي الدُّنْيَا حَسَنَةً وَفِي الأَخِرَةِ حَسَنَةً وَقِنَا عَذَابَ النَّارِ

Rabbaana aatinaa fid-dduniya hasanatan wafil Aakhirati hasanatan wa qinaa adhaaban-naari[4]

Mola wetu, tupe katika dunia mema na katika Akhera mema na Tukinge adhabu ya Moto[5]

Kuthibitika Katika Dini Na Utiifu

‏ يَا مُقَلِّبَ الْقُلُوبِ ثَبِّتْ قَلْبِي عَلَى دِينِك

Yaa muqallibal quluwbi, thabbit qalbiy ‘alaa Diynika

Ee Mwenye kupindua nyoyo, Thibitisha moyo wangu katika Dini Yako[6]

اللَّهُمَّ مُصَرِّفَ الْقُلُوبِ صَرِّفْ قُلُوبَنَا عَلَى طَاعَتِكَ

Allaahumma Muswarrifal quluwbi, swarrif quluwbanaa ‘alaa twaa’atika

Ee Allaah, Mwenye kugeuza nyoyo, zigeuzi nyoyo zetu katika utii Wako[7]

-Du’aa Za Maombi Ya Ujumla

‏ اللَّهُمَّ إِني أسْأَلُكَ مِنْ الْخَيْرِ كُلِّهِ عَاجِلِهِ وَآجِلِهِ مَا عَلِمْتُ مِنْهُ وَمَا لَمْ أعْلَمْ، وَأعُوذُ بِكَ مِنَ الشَّرِّ كُلِّهِ عَاجِلِهِ وَآجِلِهِ مَا عَلِمْتُ مِنْهُ وَمَا لَمْ ‏‏ أعْلَمْ، اللَّهُمَّ إِنِّي أسْأَلُكَ مِنْ خَيْرِ مَا سَألَكَ عَبْدُكَ وَنَبِيُّكَ، وَأعُوذُ بِكَ مِنْ شَرِّ مَا استعَاذَ بِكَ مَنْهُ عَبْدُكَ وَنَبِيُّكَ، اللَّهُمَّ إنِّي أسْأَلُكَ الْجَنَّةَ وَمَا قَرَّبَ إلَيْهَا مِنْ قَوْلٍ أوْ عَمَلٍ وَأعُوذُ بِكَ مِنْ النَّارِ وَمَا قَرَّبَ إِلَيْهَا مِنْ قَوْلٍ أوْ عَمَلٍ، وَأسْأَلُكَ أنْ تَجْعَلَ كُلَّ قَضَاءٍ قَضَيْتَهُ لِي خَيْرًا

Allaahumma inniy as-aluka minal-khayri kullihi ‘aajilihi wa aajilihi, maa ‘alimtu minhu wamaa lam a’lam. Wa a’uwdhu Bika minash-sharri kullihi ‘aajilihi wa aajilihi maa ‘alimtu minhu wamaa lam a’lam. Allaahumma inniy as-aluka min khayri maa saalaka ‘Abduka wa Nabiyyuka, wa a’uwdhu Bika min sharri masta’aadha Bika minhu ‘Abduka wa Nabiyyuka. Allaahumma inniy as-alukal-Jannata wamaa qarraba ilayhaa min qawlin aw ‘amal, wa a’uwdhu Bika minan-nnaari wamaa qarraba ilayhaa min qawlin aw ‘amal, wa as-aluka antaj-’ala kulla qadhwaai qadhwaytahu liy khayraa

Ee Allaah, hakika mimi nakuomba kheri zote zilizokaribu na mbali nizijuazo na nisizozijua. Najikinga Kwako shari zote za karibu na za mbali nizijuazo na nisizozijua. Ee Allaah, hakika nakuomba kheri alizokuomba mja Wako na Nabii Wako, na najikinga Kwako shari alizojikinga nazo mja Wako na Nabii wako. Ee Allaah, hakiki mimi nakuomba Pepo na yanayokaribisha kwayo katika kauli au amali, na najikinga Kwako Moto na yanayokaribisha kwayo katika kauli au amali, na nakuomba Ujaalie kila majaaliwa yangu [uliyonikidhia] yawe kheri[8]

‏ اللَّهُمَّ إِنِّي أسْألُكَ الْهُدَى وَالتُّقَى وَالْعَفَافَ وَالْغِنَى

Allaahumma inniy as-alukal-hudaa wat -ttuqaa wal ‘afaafa wal ghinaa

Ee Allaah hakika mimi nakuomba uongofu na ucha-Mungu na kujichunga[9] na kutosheka[10]

Kuomba Hidaaya:

اللَّهُمَّ اهْدِنِي وَسَدِّدْنِي, اللَّهُمَّ إِنِّي أَسْأَلُكَ الْهُدَى وَالسَّدَادَ

Allaahumma-hdiniy wasaddid-niy, Allaahumma inniy as-alukal-hudaa was-ssadaad

Ee Allaah, niongoe na nionyoshe sawasawa. Ee Allaah hakika mimi nakuomba hidaaya na unyofu[11]

Kuomba hesabu ya sahali Aakhirah Na Kuwa pamoja na Mtume (صلى الله عليه وسلم ) Peponi.

اللَّهُمَّ حَاسِبْنِي حِسَابًا يَسِيرًا

Allaahumma haasibniy hisaaban -yasiyraa

Ee Allaah nihesabie hisabu iliyo sahali[12]

اللَّهُمَّ إِنِّي أَسْأَلُكَ إِيمَانًا لاَ يَرْتَدُّ, وَنَعِيمًا لاَ يَنْفَدُ, وَمُرَافَقَةَ النَّبِيِّ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ فِي أَعْلَى غُرَفِ الْجَنَّةِ جَنَّاتِ الْخُلْدِ

Allaahumma inniy as-aluka iymaanan laa yartaddu, wa na’iyman laa yanfaddu, wa muraafqatan-Nabiyyi Swalla-Allaahu ‘alayhi wa sallam fiy a’-laa ghurafil-Jannah, Jannaatil-khuldi

Ee Allaah, hakika nakuomba imani isiyoritadi [isiyobadilika], na neema zisizoisha na kuambatana na Nabii Swalla-Allaahu ‘alayhi wa sallam katika vyumba vya ghorofa za juu kabisa Peponi, Pepo za kudumu milele[13]

-Kuomba Wingi Wa Iymaan, Taqwa Na Hifadhi

اللَّهُمَّ أَعِنِّي عَلَى ذِكْرِكَ وَشُكْرِكَ وَحُسْنِ عِبَادَتِكَ

Allaahumma a’inniy ‘alaa dhikrika, wa shukrika wa husni ‘ibaadatika

Ee Allaah nisaidie juu ya utajo Wako [kukudhukuru], na kukushukuru na uzuri wa ‘ibaadah Zako[14]

‏‏اللَّهُمَّ اقْسِمْ لَنَا مِنْ خَشْيَتِكَ مَا يَحُولُ بَيْنَنَا وَبَيْنَ مَعَاصِيكَ، وَمِنْ طَاعَتِكَ مَا ‏ ‏تُبَلِّغُنَا ‏بِهِ جَنَّتَكَ، وَمِنْ الْيَقِينِ مَا تُهَوِّنُ بِهِ عَلَيْنَا مُصِيبَاتِ الدُّنْيَا، وَمَتِّعْنَا بِأسْمَاعِنَا وَأبْصَارِنَا وَقُوَّتِنَا مَا أحْيَيْتَنَا, وَاجْعَلْهُ ‏الْوَارِثَ مِنَّا، وَاجْعَلْ ثَأرَنَا عَلَى مَنْ ظَلَمَنَا وَانْصُرْنَا عَلَى مَنْ عَادَانَا، ولا تَجْعَلْ مُصِيبَتَنَا فِي دِينِنَا، وَلا تَجْعَلْ الدُّنْيَا أكْبَرَ هَمِّنَا وَلا مَبْلَغَ عِلْمِنَا، وَلا تُسَلِّطْ عَلَيْنَا مَنْ لا يَرْحَمُنَا

Allaahumma-qsim-lanaa min khash-yatika maa yahuwlu baynanaa wa bayna ma’swiyk, wamin twaa’atika maa tuballighunaa bihi Jannatak, wa minal-yaqiyni maa tuhawwinu bihi ‘alaynaa muswiybaatid-duniya, wa matti’-naa biasmaa’inaa wa abswaarinaa wa quwwaatinaa maa ahyaytanaa waj-’alhul-waaritha minnaa waj-’al thaaranaa ‘alaa man dhwalamanaa wanswurnaa ‘alaa man ‘aadaana, walaa taj-’al muswiybatanaa fiy diyninaa, walaa taj-’alidduniya akbara hamminaa walaa mablagha ‘ilminaa, walaa tusallitw ‘alaynaa man-llaa yarhamunaa

Ee Allaah tugawanyie sisi hofu Yako itakayotenganisha baina yetu na baina maasi Yako, na utiifu utakaotufikisha katika Pepo Yako, na yaqini itakayotusahilishia misiba ya dunia, na tustareheshe kwa masikio yetu, na macho yetu, na nguvu zetu madamu Utatuweka hai, na yajaalie yawe ni urithi wetu na Jaalia iwe lipizo kwa anayetudhulumu, na tunusuru dhidi ya anayetufanyia uadui, na wala Usitufanyie msiba wetu ni Dini yetu, wala Usifanye dunia kuwa ndio hima yetu kubwa kabisa, na wala upeo wa elimu yetu, wala Usitusaliti kwa asiyetuhurumia[15]

Saturday 19 July 2014

HALI ZA WEMA WALIOPITA NDANI YA RAMADHAN

Makala imeandaliwa na Raudhwah Islamic Group

Kila sifa njema zinamstahikia Allah Mola wa viumbe vyote. Sala na salamu zimuendee Mtume wetu Muhammad (swalla Allahu alaihi wa sallam) na ahli zake na maswahaba wake.

Kutoka kwa Abi Hurayra (radhiya Allahu anhu), Amesema Mtume (swalla Allahu alayhi wasallam) ““Yoyote atakaefunga Ramadhan, kwa imani na kwa kutarajia malipo atasamehewa dhambi zake zilotangulia”. Bukhari na Muslim.

Katika makala hii leo tutaelezea vipi Mtume (swalla Allahu alayhi wasalla), maswahaba,matabiina na wema wengine waliopita walivyokuwa wakiuthamini mwezi wa Ramadhan. Na vipi walikuwa wakijitahidi katika kufanya ibada ndani ya Ramadhan ili waweze kufikia malengo ya Ramadhan pamoja na kupata ujira mkubwa kutoka kwa Allah (subhanahu wataala) ikiwemo kusamehewa dhambi zao zilizopita.

Wengi wetu tunafunga ila bidii inayotakiwa ambayo tuifanye ndani ya Ramadhan hatuioneshi au haitoshelezi na ndio maana kila mwaka tunafunga na hatuoni matunda ya funga zetu wala hatuoni raha ya mwezi mtukufu wa Ramadhan.

Mtume (swalla Allahu alayhi wasallam) alikuwa ni mwenye kuupokea mwezi mtukufu wa Ramadhan kwa kufunga sana ndani ya mwezi wa Shaaban. Pia unapoingia mwezi wa Ramadhan alikuwa ni mwingi wa kufanya ibada na zaidi huzidisha pale linapoingia kumi la mwisho pia hukaa iitikafu. Amesema Bibi Aisha (radhiya Allahu anha) "Zilipokuwa zikiingia siku kumi za mwisho (za Ramadhan), Mtume (swalla Allahu alayhi wasallam) alikuwa akiuhuisha usiku kwa kufanya ibada, akiamsha familia yake usiku, na akikaza Izaar yake (shuka inayovaliwa kiunoni makusudio hapa ni kuwa alikuwa akijibidiisha sana). Bukhari na Muslim.
Pia  imepokewa kutoka kwa Aisha (Radhiya Allaahu anhaa) kwamba: Mtume (swalla Allaahu alayhi wa sallam) alikuwa akifanya Itikaaf kila Ramadhaan siku kumi, ulipofika mwaka wake wa kuaga dunia alifanya Itikaaf siku ishirini" Bukhari

Pia  alikuwa Mtume (swalla Allahu alayhi wasallam) akisoma Quraan pamoja na kuja kusomeshwa Quraan na mwalim wake Sayydina Jibri. “Mtume (Swalla Allaahu alayhi waaalihi wasallam) alikuwa ni mbora (mwenye matendo mema) kwa watu, na alikuwa mbora zaidi katika Ramadhan kwa sababu Jibril alikuwa akimjia kila usiku wa Ramadhaan akimfundisha Qur-aan” Al-Bukhaari

Huyu ndie aliekuwa kipenzi cha Allah (subhanahu watala) akifanya matendo kama hao. Kipenzi ambae ameshasamehewa dhambi zake zilizopita na zijazo. Je vipi mimi na wewe?

Vipi yalikuwa mapokezi ya wema waliopita kwa ajili ya Ramadhan? Wema waliopita walikuwa wakiupokea mwezi wa Ramadhan kwa furaha pamoja na maandalizi mazuri na makubwa ya kuupokea mwezi mtukufu wa Ramadhan.  Anasema Muala Ibn Fadhwal “ Walikuwa watu wema miezi sita wakimuomba Allah (subhanahu wataala)  awafikishe Ramadhan ”

Wema waliopita walizifahamu hadithi hizi na ndio maana nao walijibidiisha katika kufanya mazuri ndani ya Ramadhan. Dua zao njema walizielekeza kwa Allah (subhanahu wataala) awafikishe mwezi wa Ramadhan wakiwa ni wazima ili waweze kufunga na kutekeleza ibada mbali mbali ndani ya Ramadhan. Pia walikuwa wakimuomba Allah (subhanahu wataala) daima wawe katika uongofu ili isije ikaingia Ramadhan na wao hawako katika utiifu wa Allah (subhanahu wataala). Pia wakimuomba Allah (subhanahu wataala) awatakabalie saumu zao watakazokuja kuzifunga.

Ukiangalia ni namna gani ambavyo walikuwa wakiuthamini mwezi huo. Mtu huanza kuupokea kwa dua za kumuomba Allah awafikishe miezi sita kabla ya kuingia Ramadhan na miezi iliyobaki hujibidiisha na kufanya Ibada. Sisi umma wa sasa tunasubiri karibu Ramadhan kufika ndio tunaanza kujiandaa nao tena kwa kuwaza vyakula tena kufanya israfu na sio vipi mtu atajipanga kwa ajili ya Ibada.

Wema waliopita waliitumia Ramadhan kwa kufanya matendo mema. Matendo yale yale ambayo alikuwa akiyafanya Mtume (swalla Allahu alayhi wasallam) kwani walifahamu kuwa kigezo chao ni Mtume Muhammad (swalla Allahu alayhi wasallam) na wakajibidiisha katika kumfuata.

Sasa tuangalie mifano hai vipi waliingia kwenye milango ya Kheri ya ndani ya Ramadhan :

Kusoma Quraan

Mwezi wa Ramadhan ni mwezi wa Quraan na ndio mwezi ambao imeteremshwa Quraan. Mtume(swalla Allahu alayhi wasallam) alikuwa mwingi wa kusoma Quraan ndani ya Ramadhan na  wema waliopita walitumia Ramadhan kwa kusoma Quraan.

Sayyidina Othmaan Ibn Affan alikuwa akimaliza msahafu kila sik umara moja.
Az zuhr mmoja ya wema waliopita wakati ilipokuwa ikiingia Ramadhan alikuwa akiacha kusoma hadithi na elimu nyengine alikuwa akiutumia muda wake wote kuisoma Quraan.

Qatadah alikuwa akimaliza kusoma Quraan kikawaida kila siku 7 mara moja lakini ndani ya Ramadhan kila baada ya siku 3 mara moja.

Kusali sala za Usiku

Kama tulivyoona kuwa Mtume (swalla Allahu alayhi wasallam) alikuwa ni mwenye kusali usiku na alikuwa akiwaamsha watu wake katika kumi la mwisho. Ummul Muuminina Aisha (Radhiya Allaahu anhaa):“Msiwache kuswali usiku (Qiyaamul Layl), kwani hakika Mjumbe wa Allah (Swalla Allaahu alayhi waaalihi wasallam) alikuwa hawachi kuswali usiku, na alikuwa Mjumbe wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) kama anaumwa au anaona uvivu huswali kwa kukaa.” Imepokelewa na Ahmad.

Hivyo hivyo na watu wema nao walimfuata Mtume (swalla Allahu alayhi wasallam). Amepokea Zayd bin Aslam kutoka kwa baba yake kuwa:“Alikuwa Umar bin Al-Khattwaab (Radhiya Allaahu anhu) akiswali usiku  Anavyomjaaliya Allah, hadi inapokuwa Aakhirul Layl -mwisho wa usiku– huwaamsha ahli zake kwa Swalah; huwaambia: Swalah Swalah, kisha husoma Aayah hii: “Na waamrishe watu wako Swalah, na ufanye subira kwa hayo. Sisi hatukuombi wewe riziki, bali Sisi ndio tunakuruzuku. Na mwisho mwema ni kwa mcha Mungu” (Twaahaa: 132). Imepokelewa na Maalik, katika Al-Muwattwa

Na katika Hadiyth ya nyengine ya Abdullaah bin Abi Bakr (Radhiya Allaahu anhu) amesema: Nimemsikia baba yangu Abu Bakr (Radhiya Allaahu anhu)- akisema:” Tulikuwa tukimaliza -Qiyaam- katika Ramadhaan basi tunawaharakisha wasaidizi kwa chakula kuchelea Alfajiri (isitukute)” Imepokelewa na Maalik katika Al-Muwattwa.

Kutoa Sadaka na Kumfturisha aliyefunga

Siku moja Mjumbe wa Allaah (Swalla Allaahu alayhi wa aalihi wasallam) aliulizwa Swawm ipi bora baada ya Ramadhaan? Akajibu: “Shaban… pakaulizwa Sadaka ipi bora? Akajibu: “Sadaka katika Ramadhaan” .Imepokelewa na At-Tirmidhiy.

Amesema Mjumbe wa Allaah (Swalla Allaahu alayhi wa aalihi wa sallam): “Atakayemfuturisha aliyefunga, atapata ujira kama ujira wake -aliyefunga- bila ya kupungua chochote katika ujira wa yule aliyefunga.” Imepokelewa na Ahmad

Masahaba na wema waliopita walijitahidi sana katika kutoa sadaka pamoja na kuftarisha wenziwao kwa kujua fadhila na utukufu wa jambo hili.

Imepokewa Abu As-Siwar Al adwi amesema “ Kundi la wanaume katika kabila la la Bani Adi walikuwa wakisali msikitini. Na hakukuwa na hata mmoja aliyekuwa akifungua peke yake. Akimuona mtu wa kula pamoja nae alikuwa anakula pamoja nae na ikiwa atakosa basi anakwenda na chakula chake msikitini ili ale chakula chake pamoja na wenzake.

Huu ni kwa uchache vipi watu wema walikuwa wakijibidiisha katika kupata matunda ya mwezi wa Ramadhan.

Nasaha kwako ewe msomaji jitahidi kuiga mifano hii ya watu wema ili nawe uwe ni mwenye kupata matunda ya mwezi wa Ramadhan kwa uwezo wake Allah (subhanahu wataala).

TAQWA NA VIPI TUTAIPATA TAQWA NDANI YA RAMADHANI

Makala Imeandaliwa na Raudhwah Islamic Group

Allah (subhanahu wataala) ametufaradhishia juu yetu kufunga. Na pale alipotufaradhishia akatuambia kuwa lengo kuu la kutufaradhishia funga ni kupata uchamungu(Taqwa). Pale aliposema “Enyi mlio amini! Mmeandikiwa Saumu, kama waliyo andikiwa walio kuwa kabla yenu ili mpate kuchamngu.”(2:183). Suali linaweza kuja nini maana ya uchamungu. Na vipi mtu anaweza kuupata uchamungu ndani ya Ramadhan? Kwa uwezo wa Allah kwa uchache majibu ya masuala hayo yatapatikana ndani ya makala hii.

TAQWA

Taqwa ni vazi ambalo anatakiwa avae kila muislamu. Vazi ambalo limekusanya yale yote aliyoamrisha Allah (subhanahu wataala) ambayo yanatakiwa yatekelezwe na yale yote yaliyoharamishwa ambayo yanatakiwa kuachwa. Msingi mkuu wa taqwa ni kufuata Quraan na Sunna za Mtume (swalla Allahu alayhi wasallam). Na vazi hili la uchamungu ndio vazi bora kuliko vazi jengine lolote. Anasema Allah (subhanahu wataala) “Enyi wanaadamu! Tumekuteremshieni nguo za kuficha tupu zenu, na nguo za pambo. Na nguo za uchamungu ndio bora…”(7:26).

Taqwa ni amri kutoka kwa Allah. Allah ametuamrisha tumche yeye pekee hapa ulimwenguni. Na akatuambia tuchukue zawadi ya uchamungu kwani ndio zawadi iliyokuwa bora kabisa na ndio itakayomfaa mwanadamu siku ya kukutana na mola wake. Anasema Allah (subhanahu wataala) “Na jitengezeeni zawadi. Na hakika bora ya zawadi ni uchamngu. Na nicheni Mimi, enyi wenye akili! (2:197).

Pia Mtume (swalla Allahu alayhi wasallam) amelisisitiza hilo kwa kututaka tuwe wenye kumcha Allah (subhanahu watala)popote tulipo iwe peke yake mtu au mbele za watu. Kutoka kwa Abu Dharr Jundub Ibn Junaada na Abu Abdur Rahmaan Muadh Ibn Jabal (radhi za Allah ziwe juu yao) kutoka kwa   Mtume (swalla Allahu alayhi wasallam) amesema: "Mche Allah popote pale ulipo, na fuatisha kitendo kibaya kwa kitendo kizuri kitafuta kitendo kibaya, na kaa na watu kwa uzuri"  At-Tirmidhiy.

Sayyidina Ali Ibn Abi Taalib (radhiya Allahu anhu) aliulizwa nini maana ya uchamungu? Akajibu “ Kumuogopa Allah, Kufanyia kazi yaliyoteremshwa (Quraan na Sunna), na kuridhia kwa kidogo (alichoruzukiwa mtu na Allah), na kujiandaa na siku ya kuondoka(kifo).

Pia Sayyidina Umar Ibn Khattwaab (radhiya Allahu anhu) aliulizwa kuhusu uchamungu. Akamuuliza yule muulizaji nini utafanya ikiwa unatembea katika njia yenye miba? Yule mtu akajibu nitatembea kwa tahadhari ili isinichome miba. Sayyidina Umar akamwambia basi huo ndio uchamungu wakati unapoishi katika ulimwengu huu. Kwa maana yale yote ya haramu mtu anatakiwa achukue tahadhari nayo ili yasije kumuingiza katika moto. Na yale ya halali ndio sehemu ya mtu kuweka mguu wake.

Kwa ujumla kabisa Taqwa ni mtu kumuogopa Allah (subhanahu wataala) na kufanya yale yote aliyoamrishwa na kuwa mbali  na yale aliyokatazwa na Allah (subhanahu wataala).

NI YAPI MALIPO YA MWENYE KUMCHA ALLAH (SUBHANAHU WATAALA)

1- Kupata wepesi wa mambo yake kutoka kwa Allah (subhanahu wataal). Anasema Allah (subhanahu wataala)“Na anaye mcha Mwenyezi Mungu, Mwenyezi Mungu humfanyia mambo yake kuwa mepesi.” (65:4).
2- Kusamehewa dhambi zake na Allah (subhanahu wataala). Anasema Allah (subhanahu wataala) “Na anaye mcha Mwenyezi Mungu atamfutia maovu yake, na atampa ujira mkubwa.”(65:5).
3- Kupata njia ya kutokea katika mambo yake na kuruzukiwa bila ya kutarajiwa. Anasema Allah (subhanahu wataala) katika Suratu Twalaaq “na anaye mcha Mwenyezi Mungu humtengezea njia ya kutokea.(2) Na humruzuku kwa jiha asiyo tazamia…(3).
4- Kupata pepo ya Allah subhanahu wataala. Tujue kuwa ndani ya pepo ya Allah hatoingia ila yule ambae ni mchamungu. Anasema Allah (subhanahu wataala) :
“Na yakimbilieni maghfira ya Mola wenu Mlezi, na Pepo ambayo upana wake ni mbingu na ardhi, iliyo wekwa tayari kwa wachamngu,”(3:133).

“Hiyo ndiyo Pepo tutayo warithisha katika waja wetu walio kuwa wachamngu.”(19:63).

Na kwa upande wa hadithi kutoka kwa Abu Hurayrah (Radhiya Allaahu anhu) Amesema: Na aliulizwa Mtume (swalla Allahu ayahi wasallam ni kitu gani kitakachowaingiza watu kwa wingi peponi? Akasema: "Kumcha Mwenyeezi Mungu na tabia njema" Na akaulizwa tena ni kitu gani kitakachowaingiza watu wengi kwa wingi motoni? Akasema "kinywa (mdomo) na utupu." Imepokelewa na At-Tirmidhiy.

VIPI TUTAIPATA TAQWA NDANI YA RAMADHANI

Muislamu anaweza kuupata uchamungu kutoka kwenye Ramadhan kwanza kwa kufunga saumu yake kwa imani na kutarajai malipo kutoka kwa Allah. Unapofunga kwa imani unaamini kuwa hiyo ni amri ya Allah ambayo inatakiwa kutekelezwa kwa vile ambavyo Allah (subhanahu wataala) ameamrisha itekelezwe.

Mwenye kufunga kwa imani daima atakuwa ni mwenye kukaa mbali na kufanya na maasi. Pia kwa kutaraji malipo. Mwanadamu akiahidiwa pesa nzuri au mshahara mzuri kutokana na kazi yake atakayoifanya basi bila ya shaka atakuwa na jitihada kufanya kazi ile kwa uzuri wa hali ya juu kabisa. Je vipi ikiwa malipo yenyewe yanatoka kwa Allah? Bila ya shaka utakuwa ni mwenye jitihada za hali ya juu kabisa kwa sababu unajua unaemfanyia jambo hilo yeye hafaidiki na kitu ila wewe ndio unafaidika na pia wewe ndio unafaidika na malipo anakupa yeye. Tuangalieni uzito wa jambo hili.

Pili kuwa na Ikhlaas katika ibada zetu zote. Ikhlaas ni kufanya jambo kwa ajili ya Allah (subhanahu wataala) pekee. Na lazima mtu awe mbali kabisa na ajiepushe na masuala ya kujionesha. Sio mtu afunge ili watu wamuone. Au afanye jambo lolote la kheri kwa sababu tu watu wapate kumuona au kumsifia. Hayo ni makosa na muislamu hatakiwi kufanya hayo.

Tatu kujibidiisha katika kuswali sala za faradhi kwa uzuri na kwa khushui. Na pia kusali sala za Sunna. Mwenye kusali sala kwa khushui na kwa ajili ya Allah (subhanahu wataala) basi kwa hakika atakuwa mbali na maasi na ndipo atakapoweza kuupata uchamungu. Allah (subhanahu wataala) anasema “Hakika Sala inazuilia mambo machafu na maovu.”(29:45).

Kujibidiisha kufanya ya kheri ikiwemo kusoma quraan kutoa sadaka,kufanya umra na mengineyo.

Muislamu ajitahidi kufanya mambo kama haya ya kheri. Na mwisho abakie kumuomba Allah (subhanahu wataala) amjaalie awe miongoni mwa wacha mungu. Kwani bila ya tawfiq ya Allah hatuwezi kufika katika darja kama hizo.

Pia muislamu anatakiwa awe mbali kabisa na kujitukuza na kujiona kuwa yeye ni mchamungu kwa sababu tu anajitahidi kufanya ibada na anakuwa mbali na mambo ya haramu. Hakuna anaeweza kujijua kuwa yeye ni mchamungu isipokuwa Allah (subhanahu wataala) ndie anaetujua sisi. Anasema Allah (subhanahu wataala) “Basi msijisifu usafi. Yeye anamjua sana mwenye kujikinga na maovu “(53:32). Tuwe na tahadhari nalo sana. Muhimu ni kuwa na bidii na mwisho ni kumuomba dua Allah atuwafikishe katika hayo.

Allah atujaalie tuwe miongoni mwa wachamungu. Aaamin.

ISTIGHFAAR

Makala Imeandaliwa na Raudhwah Islamic Group


Kila sifa njema zinamstahikia Allah (subhanahu wa ta‘ala) Muumba wa kila kilichomo katika ulimwengu huu. Swala na salamu zimuendee Mtume wetu Muhammad (swalla Allahu alaihi wa sallam).

Nini maana ya Istighfaar.?

Sayyidina Ally (radhi za Allah ziwe juu yake) alimsikia mtu mmoja akisema: Astaghfirullah. Akamuuliza unajua maana ya Istighfaar? Naye akamuuliza nini maana yake ewe Amirul muuminiin? Akajibu Sayyidina Ally: “Istighfaar ni daraja la juu la uchamungu (ililyiin) nalo ni jina lenye maana ya vitu sita: Kwanza kujuta kwa yale makosa uliyoyafanya, Kuazimia kutorejea makosa uliyoyafanya, Kuwapa watu haki zao mpaka ukutane na Allah bila ya kubaki na deni hata moja, Kutekeleza fardhi zote kwa ukamilfu, usile haramu,Uonje  na utamu wa kutenda  mema kama ulivyoonja utamu wa maasi, ukishakuyatekeleza hayo ndipo useme: ASTAGHFIRULLAH hali ya kuwa unajua maana yake”.

Sayyidina Ally (radhi za Allah ziwe juu yake) ameelezea kwa undani ni nini maana ya mtu kusema Astaghfirullah. Wengi wetu tumekuwa tukitamka tu katika midomo yetu bila ya kujua maana yake.
Ni wajibu wetu waislamu kudumu na kufanya istighfaar daima na iwe kila siku. Kwani Mtume (swalla Allahu alayhi wasallam) ambae alisamehewa na Allah (subhanahu wataala) madhambi yake yaliyopita na yatakayokuja ila bado alikuwa akileta istighfaar kila siku. Je vipi sisi ambao daima ni wenye kumuasi Allah (subhanu wataala) usiku na mchana?  Imetoka kwa Abu Hurayrah (radhi za Allah ziwe juu yake) alimsikia Mtume (swalla Allahu alayhi wasallam) akisema: "Wallaahi mimi naomba maghfirah kwa Allaah na kutubu Kwake zaidi ya mara sabiini kwa siku" Bukhaariy

Sisi tunamuasi Allah (subhanahu wataala) na tunajisahau kuwa tutaondoka hapa duniani na ndio maana hatuandai mazingira ya kukutana na mola wetu. Daima tuwe ni wenye kudumu na istighfaar. Na iwe ni istighfaar kutoka ndani ya nyoyo zetu itakayothibitishwa na vitendo vyetu vyema. Istighfaar ndio jahazi la kumuokoa muumini katika dunia hii kutokana na maasi anayomuasi Allah (subhanahu wataala) asubuhi na usiku. Na ndio maana Mtume wetu (swalla Allahu alayhi wasallam) ambae ndio kigezo chetu akawa ni mwenye kudumu na istighfaar.

Anasema Sufyan “ Ajabu kwa mwenye kuzama na pamoja yake jahazi la kumuokoa.” Wakauliza walio pamoja nae “Na ni lipi hilo jahazi la uokovu? Akajibu ISTIGHFAAR”

MANENO YA KUMPA FARAJA MWENYE KUASI

Anasema Allah (subhanahu wataala) “ Sijapata kumghadhabia mtu kama ninavyomghadhabia mtu ambae anaona dhambi yake ni kubwa kuliko msamaha wa Allah”

Maneno haya yanatupa picha halisi kuwa Allah (subhanahu wataala) anataka aombwe msamaha na wala mtu asione kafanya kubwa ambalo hawezi kusamehewa na Allah. Juu ya lolote ambalo mtu amelifanya basi alete istighfaar kwa Allah (subhanahu wataala) nae atamsamehe kwani hakika ya Allah ni mwingi wa kusamehe. "Na hakika Mimi ni Mwingi wa Kusamehe kwa anayetubia, na akaamini, na akatenda mema, tena akaongoka" (Twaaha:82)

Imetoka kwa Anas (Radhiya Allahu anhu) ambaye amesema: Nimemsikia Mtume (Swalla Allahu alayhi waaalihi wasallam) akisema: "Amesema Allahِ: Ewe Mwanadam! Hakika ukiniomba na ukanitaraji (kwa malipo) Nitakusamehe yale yote uliyonayo na wala Sijali, Ewe Mwanadam! Lau zingefikia dhambi zako ukubwa wa mbingu, kisha ukaniomba msamaha, Ningekughufuria bila ya kujali (kiasi cha madhambi uliyoyafanya). Ewe Mwanadam, Hakika ungenijia na madhambi yakaribiayo ukubwa wa ardhi, kisha ukakutana nami na hali hukunishirikisha chochote, basi Nami Nitakujia na msamaha unaolingana nao"Imepokelewa na At-Tirmidh

Hivyo ndugu zangu wakiislamu daima tuwe ni wenye kuomba msamaha kikweli kwa Allah (subhanahu wataala) ili turudi kwa Allah akiwa yupo radhi na sisi na tusiwe wenye kukata tamaa na rehma za Allah (subhanahu wataala).

BAADHI YA ISTIGHFAAR MUHIMU
Bwana wa Istighfaar
Imetoka kwa Shaddaad Bin Aws (radhi za Allah ziwe juu yake) kwamba Mtume (swalla Allahu alayhi wasallam) kasema: Bwana wa Istighfaar  ni kusema: "Allaahumma Anta Rabbiy laa ilaaha illa Anta, Khalaqtaniy wa-ana ‘Abduka, wa-ana ‘alaa ‘Ahdika wa-Wa’dika mas-tatwa’tu. A’uudhu Bika min sharri maa swana’tu, abuu Laka Bini’matika ‘alayya wa abuu bidhambi, Faghfir-liy fainnahu laa yaghfirudh-dhunuuba illa Anta" 
Maana yake ni :
"Ee Allaah,  Wewe ni Mola wangu, hapana mola apasae kuabudiwa kwa haki ila Wewe, Umeniumba mimi na mimi ni mja Wako, nami niko juu ya  ahadi Yako, na agano lako, kiasi cha uwezo wangu, najilinda Kwako kutokana  na shari ya nilichokifanya, nakiri  Kwako kwa kunineemesha, na nakiri kwa madhambi yangu, basi nakuomba unisamehe kwani hasamehi madhambi ila Wewe"Bukhaariy.

Mtume (swalla Allahu alayhi wasallam) amesema " Yeyote atakaesema "ASTAGHFRIULLAHA LLADHY LAA ILAHA ILLA HUWAL HAYYUL QAYYUM WA-ATUBU ILAYHI"
“Namuomba msamaha Allah ambaye hapana mola apasae kuabudiwa kwa haki ila yeye, aliye hai aliyesimama kwa dhati yake, na ninatubia kwake”………Allah atamsamehe hata kama ana makosa ya kukimbia vitani’

DUA YA NABII YUNUS
Dua ya Nabii Yuunus (alayhis-salaam) alipokuwa tumboni mwa  samaki alisema maneno yafuatayo "Laa ilaaha illa Anta Subhaanaka inniy kuntu minadh-dhwaalimiyn"
“Hapana mungu isipo kuwa Wewe Subhaanaka Uliyetakasika. Hakika mimi nilikuwa miongoni mwa wenye kudhulumu"  (Suratul Anbiyaa: 87).

NI ZIPI FAIDA ZA ISTIGHFAAR?

Kutoka kwa Abdillah bin Abbas radhi za Allah ziwe juu yao amesema, amesema Mtume (swallalahu alayhi wasallam): “ Mwenye kuleta Istighfaar/akaomba msamaha, Allah humjaalia mtu huyo katika kila zito na tatizo apate ufunguzi, na kila tatizo atapata faraja, na atamruzuku bila ya yeye kutegemea.”
Hadithi hii inatuonesha kwa namna gani mtu anapoleta istighfaar na kuomba msamaha Allah humpa kheri tofauti tofauti.

Faida nyengine ya istighfaar tutaipata kutoka ndani ya Quraan kupitia kisa cha Hassan Al Basri.
Mtu wa kwanza alimuendea Hassan Al Basri akamuambia kuwa nina tatizo la mtoto Hassan Al basri akamjibu lete istighfaar.Mtu wa pili akamuendea Hassan Al Basri  akamwambia nina ugumu wa maisha na hali yangu ni maskini.Nini nifanye nipate wepesi? Akamwambia lete istighfaar.Mtu wa tatu akamuendea Hassan Al Basri akamwambia mazao yangu yanakauka na mvua hakuna.Nini nifanye?akamwambia lete istighfaar.Watu waliokuwa wakisikia yale majibu wakamwambia vipi leo mbona kila anaekuja na jambo lake unamwambia lete istighfaar.au hujui nini wafanye? Hassan Al Basri akawajibu hivi mumesahau katika Suratu Nuuh aya 9-12 ya ALLAH aliwaambia waja wake walete istighfaar ili wapate watoto,wapate mali na wapate mvua kwa ajili ya mazao yao.” Nikasema: Ombeni msamaha kwa Mola wenu Mlezi; hakika Yeye ni Mwingi wa kusamehe(10) Atakuleteeni mvua inyeshe mfululizo.(11) Na atakupeni mali na wana, na atakupeni mabustani na atakufanyieni mito.(12).

Hii yote inaonyesha jinsi gani madhambi ndio yanayoleta balaa na mitihani duniani, kama ni bakora na adhabu kwa watu kama Allah alivoeleza kisa cha watu wa bustani na visa vya kaumu zilizopita, baada ya kukufuru na kutenda dhambi Allah aliwapa njaa na kiu pamoja ukame. Ila njia pekee ni kurudi kwa Allah (subhanahu wataala) na kuleta istighfaar.

Usiende kwa mganga kumshirikisha Allah ewe mwanadamu una matatizo, mambo yako hayakai vizuri basi kimbilia kuleta istighfaar ya kweli kutoka ndani ya moyo basi Allah (subhanahu wataala) atakusamehe dhambi zako na atakuneemesha neema mbali mbali kama alivyosema katika Quraan.

Hizi fadhila na faida kubwa katika istighfaar pale mja anapoomba msamaha kwa mola wake subhaanahuu wataala. Je ni wangapi ambao huleta istighfaar na wakapata kheri na neema hizi alizoahidi Allah (subhaanahuu wataala). Daima tudumu na kuleta ISTIGHFAAR.

Allah ni mjuzi zaidi.

VIPI UTAIPA NGUVU IMANI YAKO

Makala imeandaliwa na Raudhwah Islamic Group

Kila sifa njema zinamstahikia Allah Mola wa viumbe vyote. Sala na salamu zimuendee Mtume wetu Muhammad (swalla Allahu alaihi wa sallam) na ahli zake na maswahaba wake.

Imani ya mja huwa inapanda na kushuka. Na hii ni miongoni mwa tabia za muislamu. Kuna wakati muislamu imani yake humjaa na huwa anajitahidi katika Ibada. Sala tano hazimpiti tena kwa jamaa. Funga za sunna huwa ndio vazi lake. Adhkaar na sala za usiku ndio mapambo yake. Lakini baada ya muda haya mambo yote huwa hayafanyi tena. Na huanza uvivu wa kutekeleza mambo hayo.

Wengine wao huwa na imani kubwa sana na hamu ya kutenda matendo mema na nia hasa pale wanapokumbushwa. Ila baada ya muda hamu ile ya kufanya ibada inapotea. Lakini hawa wote tujiulize ni kipi kinachowafanya wawe hivyo? Tatizo lao ni udhaifu wa imani au kushuka kwa imani. Imani inapokuwa juu basi ndipo kheri zote huzikimbilia au ndipo hamu ya kufanya ibada humjaa mtu. Lakini imani inaposhuka basi huyu mtu huwa hana tena hamu ya mambo hayo na huwa na uvivu. Sasa nini afanye ili aipe nguvu imani yake? Leo katika makala hii tutajaribu kuelezea baadhi ya njia ambazo muislamu anaweza kuzifanya ili aweze kuipa nguvu imani yake. Njia zenyewe ni kama zifuatazo :

1-Kusoma Quraan kwa mazingatio
Endapo muislamu anapohisi imani yake imeshuka au inatetereka basi akimbilie kusoma sana Quraan. Ila aisome Quraan kwa mazingatio kwa kujua ni kipi ambacho Allah (subhanahu wataala) anakielezea ndani ya Quraan. Na ikiwa mtu hajui tafsiri ya Quraan basi asome kwa kutumia msahafu wa tafsiri.

Hakuna yeyote ambae amesoma Quraan kwa mazingatio isipokuwa umelainika moyo wake. Na hapo ndipo sifa ya muum,ni inapopatika. Na endapo ukaona kuwa unasoma Quraan na moyo wako hauathiriki na chochote basi jua wewe ni  maiti inayotembea duniani. Allah (subhanahu wataala) anasema “Hakika Waumini ni wale ambao anapo tajwa Mwenyezi Mungu nyoyo zao hujaa khofu, na wanapo somewa Aya zake huwazidisha Imani, na wakamtegemea Mola wao Mlezi.” (8:2). Aya hii inaonesha wazi kuwa yeyote yule anaesoma Quraan kwa ufahamu na mazingatio basi kwa hakika imani yake itapanda.

Pia Allah (subhanahu wataala) anasema ndani ya Suratu Muhammad aya ya 24 “Je! Hawaizingatii hii Qur'ani? Au kwenye nyoyo (zao) zipo kufuli?” Je sisi waumini hatuna mazingatio na aya za Allah? Au nyoyo zetu zimefungwa? Ndipo Allah akauliza au zina kufuli? Kwa maana zimefungika hakuna ndani yake kinachoingia. Tujitahidini tulainishe nyoyo zetu ili Quraan iwe ni ukumbusho kwetu.

Vipi watu wema walikuwa wakiathirika kwa kusoma Quraan kwa mazingatio ? Tuangalie mifano ifuatayo halafu tujiulize na sisi nafsi zetu zipo sehemu gani?

Siku moja Sayyidina Omar (radhiya Allahu anhu) alikuwa akiisoma aya katika aya za Quraan. Alipozisoma akaanza kulia na kulia. Mpaka akawa anashindwa kutoka nje ya nyumba yake kwa sababu ya kilio alichokuwa nacho. Je alilia tu bure bure? Hapana alilia kwa sababu aliyafahamu maneno ya Allah kwa upeo wa juu na akawa anajiuliza vipi yeye hali yake itakuwa. Aya yenyewe aliyoisoma ni  “Hakika adhabu ya Mola wako Mlezi hapana shaka itatokea.(7) Hapana wa kuizuia.(8). Machozi yake yalishindwa kujizuia akikaa akijiuliza vipi adhabu za Allah (subhanahu wataala) zitakuwa. Vipi mimi na wewe tunapozisoma aya kama hizi? Je nyoyo zetu hazipaswi kunyenyekea na kuwa na mazingatio?

Tumuangalie nae Omar Ibn Abdul Aziz. Siku moja Omar Ibn Abdul Aziz alisikilikana analia kwa sauti na kushindwa kujizuia.Jirani yake akaenda kumuuliza “Je ni kipi kimekusibu hadi unalia?”Omar Ibn Abdul Aziz akamwambia ”Hakuna kinachoniliza isipokuwa aya hii ndani ya Quraan,Allah(subhanahu wataala)anasema “…Na uhadharishe na Siku ya Mkutano, haina shaka hiyo. Kundi moja litakuwa Peponi, na kundi jengine Motoni”(42:7).Najiuliza ndani ya nafsi yangu je nitakuwa katika kundi lipi kati ya haya mawili?.

Hebu tuangalie vipi wenzetu wamekuwa wakiathirika na kusoma Quraan. Vipi mimi na wewe? Je hatuzipiti aya hizi? Je tunaisoma Quraan kwa mazingatio? Hawa ni wachache tu ambao wanaathirika kwa kusoma Quraan. Mifano ipo mingi ndugu zangu wakiislamu. Tujitahidini sana kuisoma Quraan kwa mazingatio ili tuweze kuzikuza imani zetu.

2- KUKITHIRISHA KUKUMBUKA MAUTI

Mauti ni safari ya lazima kwa kila mwanadamu. Nayo ni safari ya kutoka katika dunia katika maisha ya mpito na kuelekea katika maisha ya akhera. Mwanadamu yanapomkuta mauti basi muda wa mtihani wake ndio unakuwa umekwisha na kinachobaki ni kwenda kukutana na hesabu. Je ulishwahi kujiuliza ni vipi roho yako itatolewa? Itatolewa kwa ajili ya kwenda jannah au itatolewa kwa ajili ya kwenda motoni? Je ulishawahi kujiuliza vipi itakuwa hali yake pale utakapokuwa umebebwa kwenye jeneza? Je ulishawahi kukaa na kujiuliza vipi utaikuta hesabu yako? Je umeshawahi kujiuliza nini utamjibu Allah pale utakaposimamishwa mbele yake? Mauti ni mazingatio tosha kwa muislamu na kumkumbusha ili aweze kukaa katika njia ya Allah (subhanahu wataala).

Mtihani mkubwa zaidi ni watu kuyachukia mauti. Na wapokuwa wakikumbushwa kuhusu mauti huwa wanachukia na kuona Sheikh hakuwa na mawaidha ila ya kuwatisha. Kumbe wanasahau kukumbushwa mauti ni kumfanya mtu aizidishe imani yake na kujiandaa na siku ya kutoka roho. 

Mtume (swalla Allahu alayhi wasallam) anasema katika hadithi “ Kithirisheni katika kukumbuka chenye kukata ladha “ Mtume (swalla Allahu alayhi wasallam) ameyaita mauti kama ni kikata ladha. Ndiyo mauti ni yenye kukata ladha ya starehe za uongo za dunia. Mwnadamu anapokumbuka mauti basi awe anajiuliza masuala ya msingi ambayo atakutana nayo. Na endapo muislamu ataona kuwa hata akikukumbuka mauti moyo wake hauthiriki basi pi ana yeye ataingia katika kundi la wale maiti wanaotembea katika dunia hii.
Anasema Allah (subhanahu wataala) ““Kila nafsi itaonja mauti. Na bila shaka mtapewa ujira wenu kamili Siku ya Qiyaama.”(3:185).

Tujiandaeni mauti na tujitahidini katika kukithirisha kukumbuka mauti kila wakati hili litamsaidia muumini na kumuasi Allah (subhanahu wataala).

3-KUTEMBELEA MAKABURI

Makaburi nayo yana siri nzito ndani yake. Tayari tumeshamuhifadhi ndugu yetu katika kuelekea katika maisha yake ya milele. Nini kinachojiri ndani ya mauti. Mwanadamu atakapokaa na kuliwaza kaburi, giza lake na juu yake kufukiwa na michanga. Vipi atakaa ndani ya shimo hilo?  Je ulishawahi kujiuliza vipi itakuwa usiku wa kwanza ndani ya kaburi lako?Je wakati watu watakapokuwa washamzika ataweza kujibu maswali ya Munkar na Nakir? Je kaburi lake litakuwa ni bustani katika bustani ya peponi au mashimo katika mashimo ya motoni?

Mtume (swalla Allahu alayhi wasallam) ametuusia kutembelea makaburi pale aliposema “Mtume (Swalla Allaahu alayhi wa aalihi wasallam) amesema, “Nilikuwa nimewakataza kwanza kuzuru makaburi lakini kuanzia sasa yatembeleeni.” (Muslim) katika riwaya nyingine , “Kwani huko kuzuru makaburu hukukumbusheni na akhera.” (Ahmad) .Kutembelea huku sio ule wakati wa kwenda kuzika. Mtu awe anapanga siku maalum kwenda kuyatembelea makaburi kwa lengo iwe ni mazingatio kwake yeye. Kwa lengo na yeye ajiulize vipi itakuwa hali yake pale atakapowekwa ndani ya kaburi.

Sayyidina Othman Ibn Affan (radhiya Allahu anhu) alikuwa akitajiwa kuhusu moto na adhabu za Allah analia. Lakini anapotembelea makaburi huwa analia zaidi mpaka ndevu zake zikarowa machozi. Maswahaba wakamuuliza ni kipi kinachomfanya hivyo ? Sayyidina Othman akajibu kaburi ndio nyumba ya kwanza ya maisha ya akhera. Ikitengenea hali ndani ya kaburi ndio yametengenea mengine na hali ikiwa mbaya basi ndio mwanadamu amekhasirika. Sasa najiuliza vipi kaburi langu litakuwa?

Mmoja ya watu wema alikuwa akiingia sehemu ya makaburi basi huuziba uso wake kwa kilemba chake. Kwa nini huuzibaa? Ili asionekane akilia kwani alikuwa anashindwa kujizuia asilie akikaa akiliwaza kaburi lake. Litakuwa na hali gani.

Hawa ndio ambao wakikumbuka vitu kama hivi huvikumbuka kwa mazingatio makubwa ndani yake. Je vipi mimi na wewe? Sio wale ambao tunaenda kwenye makaburi na simu zetu za kuchat mkononi? Sio sisi tunaenda kwenye makaburi na mazungumzo ya kusema watu yapo kwenye midomo yetu?
Tembelea makaburi ili uizidshe imani na uwe ni mwenye kujiandaa daima na kukaa katika kaburi lako.

4- KUKAA NA MARAFIKI WEMA NA KUSHIRIKI VIKAO VYA KHERI

Rafiki huchangia kwa kiwango kikubwa maisha ya binaadamu. Na hili linathibitishwa na Mtume Muhammad(swalla Allahu alayhi wasallam) kwa kauli yake pale aliposema “ Mtu hufuata mwenendo wa rafiki yake,basi aangalie mmoja wenu ni nani anaemfanya kuwa ni rafiki” Attirmidhy.

Jitahidi sana na kuwaepuka marafiki waovu kwani hawawezi kukusaidia katika kuikuza imani yako. Kaa na rafiki mwema rafiki ambae daima atakuwa ni mwenye kukuhimiza katika kufanya yalo mema na yaliyo mazuri. Tumeona mifano ya wengi ambao wamepotoka kwa sababu tu ya marafiki.

Na Allah (subhanahu wataala) anatuambia ndani ya Quraan “Wala usimt'ii tuliye mghafilisha moyo wake asitukumbuke, na akafuata matamanio yake yakawa yamepita mpaka.”(18:28). Aya hii ni ukumbusho kwa muumini awe mbali na wale ambao hawako katika kumtii Allah (subhanahu wataala) nao hufuata matamanio ya nafsi zao.

Mtume (swalla Allahu alayhi wasallam) anasema "Mfano wa rafiki mwema na rafiki mbaya ni kama ule wa muuzaji wa misk na mhunzi. Basi kwa muuzaji wa misk, imma atakunusisha, au utanunua kwake ama angalau utafurahia harufu nzuri kwake. Na kwa yule mhunzi, imma atakuchomea nguo au utapata harufu mbaya kutoka kwake.” [Al-Bukhaariy na Muslim].

Katika tafsiri ya Hadiyth hii, Imam An-Nawawiy alisema: Mtume ((Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam)) alilinganisha rafiki mzuri na muuzaji misk kwasababu, kwa rafiki mzuri mwenye tabia ya upole, na elimu, utapata faida kwake. Na Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) alitukataza kukaa na wale wenye kufanya maovu.

Hivyo ndugu yangu muislamu tafuta rafiki mwema ambae daima mazungumzo yenu yatakuwa ni ya kheri na ni yenye kuhimizana kufanya mema na kukumbushana pale mtu anapokosea.

Pia kushiriki katika vikao vya kheri katika misikiti,kwenda katika mihadhara kwani katika vikao hivyo hukumbushwa yaliyo mema na kukatazwa yaliyo mabaya ambayo mtu yatamfaa katika maisha yake ya dunia na kesho akhera. Na tusichoke kuhudhuria kwa wingi na kwa wakati mwingi kama vile tunavyotumia wakati mwingi katika kuangalia michezo,mipira au kupoteza wakati kwa kuchat na ndani ya facebook.
Mwisho kabisa ndugu yangu wa kiislamu nakuusia mambo mawili. Jambo la kwanza kithirisha sana katika kumuomba dua Allah (subhanahu wataala) katika kuifanya imani yako isiwe yenye kutetereka na aijaalie imani yako iwe ni yenye kuzidi pale unapokutana na misukosuko. Pia kuwa ni mwenye kuihesabu nafsi yako daima kabla ya kulala hii itasaidia katika kukuzindua ni kwa kiasi gani uko mbali na Allah. Na hesabu hiyo uwe unaifanya ni sababu ya wewe kujiepusha na maasi yale ambayo umeyatenda.

Namuomba Allah atujaalie imani zetu ziwe thabiti na aturidhie pale tutapoondoka hapa duniani. Aaamin.