Sunday 31 March 2013

MAJINA YA MALAIKA NA KAZI ZAO

Mwenyezi Mungu S.W.T. kajaalia kila kitu alichokiumba kina jina lake maalum ili iwe ni alama yake ya kutambulikana kwake. Na kama vile kila mwanaadamu analo jina lake basi ni hivyo hivyo kwa Malaika, kila Malaika ana jina lake, lafudhi ya majina yao hayafanani na lafudhi ya majina ya kibinaadamu, yaani wao hawana majina kama Athmani, au Ramadhani na Mariam kadhalika na hii inawezekana pengine ni kwa sababu wao wameumbwa si waume wala wake. Mwenyezi Mungu S.W.T. na Mtume wake S.A.W. wametufunulia ndani ya Qur-ani na Hadithi majina ya Malaika 12 pamoja na shughuli zao, kama ifuatavyo:-

1.JIBRIL.


Jibril ni mkubwa wa Malaika na ametajwa katika aya zaidi ya moja ndani ya Qur-ani. Mwenyezi Mungu S.W.T. kasema katika Suratil Baqarah aya ya 97, “


قُلْ مَنْ كَانَ عَدُوًّا لِجِبْرِيلَ فَإِنَّهُ نَزَّلَهُ عَلَى قَلْبِكَ بِإِذْنِ اللَّهِ مُصَدِّقًا لِمَا بَيْنَ يَدَيْهِ وَهُدًى وَبُشْرَى لِلْمُؤْمِنِينَ


Maana yake, “Sema: “Aliyekuwa ni adui wa Jibril, (kwa kuwa ndiye aliemletea Utume Nabii Muhammad asiwapelekee Mayahudi ni bure hana kosa Jibril); hakika yeye ameiteremsha Qur-ani moyoni mwako kwa idhini ya Mwenyezi Mungu (sio kafanya kwa kupendelea kwake); (Qur-ani) inayosadikisha yale yaliyokuwa kabla yake, na ni uwongozi na khabari njema kwa wanaoamini.”


Jibril A.S. ni Malaika mwenye nguvu sana, na Mwenyezi Mungu S.W.T. amemsifu katika Surat Najm aya ya 5 kwa nguvu zake, kasema,


"Amemfundisha (Malaika) Mwenye nguvu sana."


Na baadhi ya Wanavyuoni wamesema kwamba,

“Jibril A.S. kwa ushujaa na nguvu zake aliweza kuiinua miji ya watu wa Luut pamoja na kila kitu kilichomo ndani yake pamoja na watu wake ambao idadi yao inasemekana kuwa ni watu mia nne elfu, aliwainua mpaka mbinguni kwa kutumia bawa lake moja kati ya mabawa yake mia sita. Mbwa na majogoo walisikika sauti zao na Malaika wengine wakati wakilia; na kwa amri ya Mola wake aliiangamiza miji ile na kila kilichokuwemo humo kwa kuigeuza juu chini.”

Mwenyezi Mungu S.W.T. kasema katika Surat Huud aya ya 82, “

فَلَمَّا جَاءَ أَمْرُنَا جَعَلْنَا عَالِيَهَا سَافِلَهَا وَأَمْطَرْنَا عَلَيْهَا حِجَارَةً مِنْ سِجِّيلٍ مَنْضُودٍ

Maana yake, “Basi ilipofika amri yetu tuliigeuza nchi juu chini, na tukawateremshia mvua ya changarawe za udongo mgumu uliokamatana wa Motoni.”


Moja ya kazi ya Malaika huyu mwaminifu ni kupeleka wahyi kwa Mitume na Manabii wote waliotangulia. Na alimwijia mara nyingi zaidi Mtume wetu S.A.W. kuliko Mitume wengine wote, kwa ajili ya kumshushia wahyi au kumfundisha baadhi ya mambo kutoka kwa Mola wake kama vile kusali na kusoma Qur-ani. Jibril ameitwa kwa majina tofauti ndani ya Qur-ani. Na majina yenyewe ni haya yafuatayo:-

1.1.ROHO (RUUH).


Naye ndiye "Roho ambae alitumwa kwa Bibi Maryam mama wa Nabii Issa A.S."

Kama alivyomuita Mwenyezi Mungu S.W.T. katika Surat Maryam aya ya 17, “

فَأَرْسَلْنَا إِلَيْهَا رُوحَنَا فَتَمَثَّلَ لَهَا بَشَرًا سَوِيًّا

Maana yake, “Tukampeleka Roho Yetu (Jibril A.S.) akajifananisha kwake (kwa sura ya) binaadamu alie kamili.”

1.2.ROHO MWAMINIFU (RUUHUL AMIIN).


Na katika Qur-ani anajulikana pia kama "Roho mwaminifu" Mwenyezi Mungu S.W.T. kasema katika Surat Ash-Shu`araa aya ya 193 na ya 194, “


نَزَلَ بِهِ الرُّوحُ الأمِينُ * عَلَى قَلْبِكَ لِتَكُونَ مِنْ الْمُنذِرِينَ

Maana yake, “Ameuteremsha haya Roho mwaminifu (Jibril). Juu ya moyo wako, ili uwe miongoni mwa Waonyaji.”

1.3.ROHO TAKATIFU (RUUHUL QUDUS).


Naye kaitwa na Mwenyezi Mungu S.W.T. kwa jina la "Roho takatifu" katika Suratil Nahal aya 102, “


قُلْ نَزَّلَهُ رُوحُ الْقُدُسِ مِنْ رَبِّكَ بِالْحَقِّ… 

Maana yake, “Sema: “Roho takatifu (yaani Jibril) ameiteremsha hii (Qur-ani) kutoka kwa Mola wako kwa haki…”

1.4.NAMUUS.


Na ameitwa "Namuus" kama alivyosema Waraqa bin Noufal kumwambia Mtume S.A.W. wakati wa mwanzo kabisa Jibril alipomteremshia wahyi Mtume S.A.W.. Kasema Noufal, “


"لقد جاءك النَّامُوسُ الَّذِي أَنْزَلَ اللَّهُ عَلَى مُوسَى".

Maana yake, “Amekuijia Namuus (yaani Jibril) ambaye alimteremsha Mwenyezi Mungu kwa (Nabii) Musa (A.S.).”


Naye ni Malaika mwenye heshima na cheo kikubwa sana mbele ya Mola wa walimwengu wote. Mwenyezi Mungu S.W.T. kamsifu kwa sifa za nguvu zake na cheo chake katika Surat Takwyr aya ya 20, “


ذِي قُوَّةٍ عِنْدَ ذِي الْعَرْشِ مَكِينٍ

Maana yake, “Mwenye nguvu, mwenye cheo cha heshima kwa Mwenyezi Mungu.”

2.MIKAIIL.


Mikaiil ni Malaika mwingine mwenye daraja ya juu mbele ya Mwenyezi Mungu S.W.T. kama alivyomtaja katika Suratil Baqarah aya ya 98, “


مَنْ كَانَ عَدُوًّا لِلَّهِ وَمَلائِكَتِهِ وَرُسُلِهِ وَجِبْرِيلَ وَمِيكَالَ فَإِنَّ اللَّهَ عَدُوٌّ لِلْكَافِرِينَ

Maana yake, “Aliyekuwa adui wa Mwenyezi Mungu na Malaika Wake na Mitume Wake na Jibril na Mikaiil (basi mtu huyo anatafuta kuangamia) kwani Mwenyezi Mungu ni adui wa makafiri.”

Naye amewakilishwa kwa ajili ya mvua na mimea kwa amri ya Mola wake. Mwenyezi Mungu S.W.T. kasema katika Suratil A`araaf aya ya 57, “

وَهُوَ الَّذِي يُرْسِلُ الرِّيَاحَ بُشْرًا بَيْنَ يَدَيْ رَحْمَتِهِ حَتَّى إِذَا أَقَلَّتْ سَحَابًا ثِقَالا سُقْنَاهُ لِبَلَدٍ مَيِّتٍ فَأَنزَلْنَا بِهِ الْمَاءَ فَأَخْرَجْنَا بِهِ مِنْ كُلِّ الثَّمَرَاتِ كَذَلِكَ نُخْرِجُ الْمَوْتَى لَعَلَّكُمْ تَذَكَّرُونَ


Maana yake, “Na Yeye Ndiye anayepeleka pepo (za kuvuma) kuwa ni bishara (khabari njema) kabla ya kufika Rehema Yake (mvua). Hata hizo pepo zinapobeba mawingu mazito tunayachunga mpaka kwenye nchi iliyo kufa. Kisha tunateremsha kwayo maji, ndio kama hivyo tukatolesha kila aina ya matunda. Basi hali kadhalika tunavyo wafufua wafu, ili mpate kukumbuka.

3.ISRAFIIL.


Israfiil ni jina la Malaika ambaye atakayepuliza baragumu siku ya Kiyama. Naye ni mmoja wa Malaika ambaye aliyekuwa akitajwa sana na Mtume wetu S.A.W. katika dua yake kila anapoamka usiku kuabudu. Alikuwa Mtume S.A.W. anamtaja yeye pamoja na Jibril na Mikaiil, kasema katika Hadithi iliyopokelewa na Aisha R.A.A.H. na iliyotolewa na Abu Daud, “

"اللَّهُمَّ رَبَّ جِبْرِيلَ وَمِيكَائِيلَ وَإِسْرَافِيلَ أَنْتَ تَحْكُمُ بَيْنَ عِبَادِكَ فِيمَا كَانُوا فِيهِ يَخْتَلِفُونَ ، اهْدِنِي لِمَا اخْتُلِفَ فِيهِ مِنَ الْحَقِّ بِإِذْنِكَ إِنَّكَ تَهْدِي مَنْ تَشَاءُ إِلَى صِرَاطٍ مُسْتَقِيمٍ".

Maana yake, “Ewe Mwenyezi Mungu! Mola wa Jibril na Mikaiil na Israfiil Wewe Ndiye unayehukumu baina ya waja Wako katika yale waliokuwa wakikhitilafiana, niongoze kwendea haki katika yale waliokhitilafiana kwa idhini Yako, unamuongoza umtakae kwendea njia iliyonyooka.”

4.MAALIK.


Maalik ni jina la Malaika mkubwa wa Malaika walio walinzi wa Motoni. Mwenyezi Mungu S.W.T. kasema katika Surat Zzukhruf aya ya 77, “

وَنَادَوْا يَا مَالِكُ لِيَقْضِ عَلَيْنَا رَبُّكَ قَالَ إِنَّكُمْ مَاكِثُونَ

Maana yake, “Nao watapiga kelele (kumwambia yule Malaika anayewaadhibu waseme) “Ee Maalik! Naatufishe Mola wako!” (Maalik) aseme “Bila shaka mtakaa humu humu (Motoni).”

5.RIDHWAAN.


Ridhwaan ni jina la Malaika ambae kazi yake ni mlinzi wa Peponi. Mwanachuoni Ibn Kathiir kasema, “

"وخازن الجنة ملك يقال له رضوان ، جاء مصرحا به في بعض الأحاديث".

Maana yake, “Na mlinzi wa Peponi ni Malaika anaeitwa Ridhwaan, ameitwa (kwa jina) Musarrihan katika baadhi ya Hadithi.”

6.MUNKAR NA NAKIIR.


Munkar na Nakiir ni Malaika wawili ambao amewataja Mtume S.A.W. katika Hadithi sahihi kuwa ni Malaika waliowakilishwa kuuliza watu maswali kaburini. Nao wana umbo la kutisha na sauti kali sana. Mwenyezi Mungu S.W.T. atuepushe na adhabu ya kaburi. Kila mmoja wetu baada ya kufa kwake anapozikwa kaburini mwake humwijia Malaika hawa wawili na kumuuliza maswali kama vile. "Nani Mungu wako? Nani Mtume wako? Na nini dini yako?" Ikiwa mtu huyo hapa duniani alikuwa mtiifu kwa Mwenyezi Mungu S.W.T. na Mtume Wake S.A.W. ataweza kujibu maswali hayo kwa urahisi lakini ikiwa ni kinyume ya hivyo maswali hayo yatakuwa magumu kwake, hivyo inatupasa tujitayarishe kwa maswali hayo ya kaburini. Na urahisi wa kujibu kwake inategemea na jinsi mtu alivyoishi katika maisha yake hapa duniani. Yaani mtu mwema au muovu?

7.HARUUT NA MARUUT.


Nayo haya ni majina ya Malaika wawili aliowatuma Mwenyezi Mungu S.W.T. kwa watu wa Baabil (Babylon hivi sasa ni nchi ya Iraq) ili wawafanyie mtihani wa kuwafundisha uchawi. Na walikuwa hawamfundishi mtu yeyote yule ila baada ya kumuonya kwao kwamba ukitaka tukufunze basi utakufuru. Mwenyezi Mungu S.W.T. kasema katika Suratil Baqarah aya ya 102, “


وَمَا كَفَرَ سُلَيْمَانُ وَلَكِنَّ الشَّيَاطِينَ كَفَرُوا يُعَلِّمُونَ النَّاسَ السِّحْرَ وَمَا أُنزِلَ عَلَى الْمَلَكَيْنِ بِبَابِلَ هَارُوتَ وَمَارُوتَ وَمَا يُعَلِّمَانِ مِنْ أَحَدٍ حَتَّى يَقُولا إِنَّمَا نَحْنُ فِتْنَةٌ فَلا تَكْفُرْ… 


Maana yake, “Na (Nabii) Suleiman hakukufuru, bali Mashetani ndio waliokufuru, wakiwafundisha watu uchawi (waliokuwa wakiujua wenyewe tangu zamani) na (uchawi) ulioteremshwa kwa Malaika wawili, Haruut na Maruut, katika mji wa Baabil. Na wala (Malaika hao) hawakumfundisha mtu yeyote mpaka wamwambie: “Hakika sisi ni mtihani, basi usikufuru…”

8.IZRAIL.


Na hili ndilo jina alilopewa Malaika wa mauti, jina hili halikutajwa ndani ya Qur-ani wala halikutajwa katika Hadithi sahihi, lakini hii ni kauli ya Wanavyuoni kwa jina hili.

9.RAQIIB NA ATIID.


Hayo ni majina ya Malaika wawili, ambao wamewakilishwa na Mwenyezi Mungu S.W.T. kwa ajili ya kuandika kauli na vitendo vya watu. Na maana ya majina haya Raqiib na Atiid ni kuwa wamehudhuria, mashahidi kwa vile daima hawaachani wako pamoja na watu ila kwa baadhi ya mambo fulani, kama vile mtu akiwa na janaba au akiwa uchi au akiingia msalani (chooni). Mwenyezi Mungu S.W.T. kasema katika Suratil Qaaf aya ya 17 na ya 18, “


إِذْ يَتَلَقَّى الْمُتَلَقِّيَانِ عَنْ الْيَمِينِ وَعَنْ الشِّمَالِ قَعِيدٌ * مَا يَلْفِظُ مِنْ قَوْلٍ إِلا لَدَيْهِ رَقِيبٌ عَتِيدٌ

Maana yake, “Wanapopokea wapokeaji wawili, anaekaa kuliani na (anaekaa) kushotoni, (Malaika). Hatoi kauli yoyote isipokuwa karibu nae yuko mngojeaji (mwangalizi) tayari (kuandika).”

Thursday 14 March 2013

Sayyid Al-Istighfaar (Bwana Wa Al-Istighfaar )

Mwenyezi Mungu Anasema:

{{Na ambao pindi wafanyapo uchafu au wakajidhulumu nafsi zao humkumbuka Mwenyezi Mungu na wakamwomba msamaha kwa dhambi zao - na nani anaye futa dhambi isipo kuwa Mwenyezi Mungu? - na wala hawaendelei na waliyo yafanya na hali wanajua.}} [Al-‘Imraan: 135]

Imesimuliwa kuwa Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesema:

((Mwenyezi Mungu huifurahia toba ya mja wake kuliko mmoja wenu anapokuwa juu ya mnyama wake jangwani akamuangusha na kumkimbia.)) [Imepokewa na Al-Bukhaariy]

Na katika riwaya ya Muslim na wengine:

((Mwenyezi Mungu huifurahia toba ya mja wake kuliko mmoja wenu anapokuwa juu ya mnyama wake jangwani akamuangusha na kumkimbia. Mnyama huyo akiwa amebeba chakula chake na maji yake, kisha mtu huyo akakata tamaa, akauendea mti na kuegemea chini ya kivuli chake akiwa keshakata tamaa ya kumuona mnyama wake tena. Na anapokuwa katika hali hiyo, ghafla anamuona mnyama wake mbele yake. Akazishika hatamu zake, kisha akasema kwa furaha: "Mola wangu Wewe ni mja wangu na mimi ni mola wako". Alikosea kwa wingi wa furaha.))

Na maana ya Mwenyezi Mungu kuifurahia toba hiyo ni kuwa anaridhika na nia ya mja wake huyo juu ya kuwa alikosea kutamka.

Miongoni mwa du’aa za kuomba maghfira, ni hii du’aa inayoitwa 'Sayyidul-Istighfaar' (Du’aa bora ya kuomba maghfira kupita zote) aliyotuusia Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam). Du’aa ambayo ndani yake imekusanya maana zote za tawbah na kukiri, na kwamba hapana mwenye kusamehe makosa isipokuwa Mwenyezi Mungu (Subhaanahu wa Ta’ala).

Imeposimuliwa kutoka kwa Shaddaad bin ‘Aws (Radhiya Allaahu ‘Anhu) kuwa Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: ((Bwana wa kuomba maghfira ni kusema:
اللَّهُمَّ أَنْتَ رَبِّي لا إِلَهَ إلا أَنْتَ خَلَقْتَنِي وَأَنَا عَبْدُكَ وَأَنَا عَلَى عَهْدِكَ وَوَعْدِكَ مَا اسْتَطَعْتُ أَعُوذُ بِكَ مِنْ شَرِّ مَا صَنَعْتُ أَبُوءُ لَكَ بِنِعْمَتِكَ عَلَيَّ وَأَبُوءُ لَكَ بِذَنْبِي فَاغْفِرْ لِي فَإِنَّهُ لا يَغْفِرُ الذُّنُوبَ إِلا أَنْتَ.
Allaahumma anta Rabbiy laa ilaaha illa Anta. Khalaqtaniy wa ana ‘abduka. Wa ana ‘alaa ‘ahadika wa wa’adika ma statwa’atu. A’udhu bika min sharri ma swana’atu. Abu-u laka bini’imatika ‘alayya wa abu-u laka bidhanbiy, faghfirliy, fainnahu laa yaghfiru dhunuuba illaa anta.

Akasema: Atakayesema hayo wakati wa mchana akiwa na yakini juu yake akafa siku hiyo kabla ya usiku kuingia, huyo ni katika watu wa Peponi. Na atakayesema hayo wakati wa usiku akiwa na yakini juu yake akafa kabla ya asubuhi kuingia, huyo ni katika watu wa Peponi.)) [Imepokewa na Al-Bukhaariy, At-Tirmidhiy, An-Nasaaiy na wengine]


Maana Yake

Ee Allaah. Wewe ni Mola wangu hapana anayestahiki kuabudiwa isipokuwa Wewe
اللَّهُمَّ أَنْتَ رَبِّي لا إِلَهَ إلا أَنْتَ
Umeniumba na mimi ni mja Wako
خَلَقْتَنِي وَأَنَا عَبْدُكَ
Na mimi nimo katika kutekeleza maamrisho Yako na waadi Wako niwezavyo
وَأَنَا عَلَى عَهْدِكَ وَوَعْدِكَ مَا اسْتَطَعْتُ
Ninajikinga Kwako na kila shari niliyoitenda
أَعُوذُ بِكَ مِنْ شَرِّ مَا صَنَعْتُ
Ninakiri Kwako kwa neema Zako juu yangu
أَبُوءُ لَكَ بِنِعْمَتِكَ عَلَيَّ
Na ninakiri Kwako juu ya dhambi zangu
وَأَبُوءُ لَكَ بِذَنْبِي
Kwa hivyo unisamehe kwa sababu hapana mwenye kusamehe madhambi isipokuwa Wewe
فَاغْفِرْ لِي فَإِنَّهُ لا يَغْفِرُ الذُّنُوبَ إِلا أَنْتَ.



Wednesday 13 March 2013

Firauni (Pharaoh)





Tukawavusha bahari Wana wa Israili, na Firauni na askari wake wakawafuatia kwa dhulma na uadui. Hata Firauni alipo kuwa anataka kuzama akasema: Naamini kuwa hapana mungu ila yule waliye muamini Wana wa Israili, na mimi ni miongoni mwa walio nyenyekea!

(Quran 10:90)





Ala! Sasa? Na hali uliasi kabla yake na ukawa miongoni mwa mafisadi!

(Quran 10:91)





Leo, basi, tutakuokoa kwa mwili wako, ili uwe Ishara kwa ajili ya walio nyuma yako. Na hakika watu wengi wameghafilika na Ishara zetu.

(Quran 10:92)







Today, we will preserve your body, to set you up as a lesson for future generations

Pharaoh’s body was found in the Red Sea, this proves that the story of Moses (peace be upon him) splitting the sea with the help of Allah Almighty really happened. Pharaoh’s body is 3500 years old, it’s amazing that it was preserved very well in the sea. Even some of the mummies are not preserved this well. Also fish in the sea could have easily eaten the flesh, but they didn’t. Why is that? The answer is in the following verse of the Quran where God says:

Allah says in the HOLLY Qur'an :

We delivered the Children of Israel across the sea. Pharaoh and his troops pursued them, aggressively and sinfully. When drowning became a reality for him, he said, "I believe that there is no god except the One in whom the Children of Israel have believed; I am a submitter.Too late! For you have rebelled already, and chose to be a transgressor. Today, we will preserve your body, to set you up as a lesson for future generations. Unfortunately, many people are totally oblivious to Our signs.
Quran (10:90-92)








Pharaoh’s body. Even the internal organs are intact

Tuesday 12 March 2013

Duaa Kutoka Quran Na Maana Yake

 

 رَبِّ اجْعَلْ هَـَذَا بَلَدًا آمِنًا وَارْزُق ْأَهْلَهُ مِنَ الثَّمَرَاتِ مَنْ آمَنَ مِنْهُم بِاللّهِ وَالْيَوْمِ الآخِرِ     (البقرة:126)

Ee Mola wangu Mlezi! Ufanye huu uwe mji wa amani, na uwaruzuku watu wake matunda, wale wanao muamini Mwenyezi Mungu na Siku ya Mwisho (Al-Baqara 126)

رَبَّنَا تَقَبَّلْ مِنَّا إِنَّكَ أَنتَ السَّمِيعُ الْعَلِيمُ      
  رَبَّنَا وَاجْعَلْنَا مُسْلِمَيْنِ لَكَ وَمِن ذُرِّيَّتِنَا أُمَّةً مُّسْلِمَةً لَّكَ وَأَرِنَا مَنَاسِكَنَا وَتُبْ عَلَيْنَآ إِنَّكَ أَنتَ التَّوَّابُ الرَّحِيمُ  
(البقرة 127 – 128)

Ewe Mola Mlezi wetu! Tutakabalie! Hakika Wewe ndiye Msikizi Mjuzi
Ewe Mola Mlezi wetu! Tujaalie tuwe ni wenye kusilimu kwako, na pia miongoni mwa vizazi vyetu wawe umma ulio silimu kwako. Na utuonyeshe njia za ibada yetu na utusamehe. Bila shaka Wewe ndiye Mwenye kusamehe Mwenye kurehemu. (Al-Baqara 127 – 128)).

رَبَّنَا آتِنَا فِي الدُّنْيَا حَسَنَةً وَفِي الآخِرَةِ حَسَنَةً وَقِنَا عَذَابَ النَّارِ (البقرة 201  )  

Mola wetu Mlezi, tupe duniani mema, na Akhera mema, na utulinde na adhabu ya Moto
(Al-Baqara 201)

رَبَّنَا أَفْرِغْ عَلَيْنَا صَبْرًا وَثَبِّتْ أَقْدَامَنَا وَانصُرْنَا عَلَى الْقَوْمِ الْكَافِرِينَ  (البقرة 250 )

Mola wetu Mlezi! Tumiminie subira, na isimamishe imara miguu yetu, na utusaidie tuwashinde watu Makafiri (Al-Baqara 250)

رَبَّنَا لاَ تُؤَاخِذْنَا إِن نَّسِينَا أَوْ أَخْطَأْنَا رَبَّنَا وَلاَ تَحْمِلْ عَلَيْنَا إِصْرًا كَمَا حَمَلْتَهُ عَلَى الَّذِينَ مِن قَبْلِنَا رَبَّنَا وَلاَ تُحَمِّلْنَا مَا لاَ طَاقَةَ لَنَا بِهِ وَاعْفُ عَنَّا وَاغْفِرْ لَنَا وَارْحَمْنَا أَنتَ مَوْلاَنَا فَانصُرْنَا عَلَى الْقَوْمِ الْكَافِرِينَ  (البقرة 286)

Mola wetu Mlezi! Usituchukulie tukisahau au tukikosea. Mola wetu Mlezi! Usitubebeshe mzigo kama ulio wabebesha wale walio kuwa kabla yetu. Mola wetu Mlezi Usitutwike tusiyo yaweza, na utusamehe, na utughufirie, na uturehemu. Wewe ndiye Mlinzi wetu. Basi tupe ushindi tuwashinde kaumu ya makafiri. (Al-Baqara 286)

رَبَّنَا لاَ تُزِغْ قُلُوبَنَا بَعْدَ إِذْ هَدَيْتَنَا وَهَبْ لَنَا مِن لَّدُنكَ رَحْمَةً إِنَّكَ أَنتَ الْوَهَّابُ  (آل عمران 8  )

Mola wetu Mlezi! Usizipotoe nyoyo zetu baada ya kwisha tuongoa, na utupe rehema itokayo kwako. Hakika Wewe ndiye Mpaji.  (Al-Imran 8)



رَبَّنَا إِنَّنَا آمَنَّا فَاغْفِرْ لَنَا ذُنُوبَنَا وَقِنَا عَذَابَ النَّارِ  (آل عمران 16)

Mola wetu Mlezi! Hakika sisi tumeamini, basi tufutie madhambi yetu, na tuepushe na adhabu ya Moto.  (Al-Imran 16)

رَبِّ هَبْ لِي مِن لَّدُنْكَ ذُرِّيَّةً طَيِّبَةً إِنَّكَ سَمِيعُ الدُّعَاء  (آل عمران 38]

Mola wangu Mlezi! Nipe kutoka kwako uzao mwema. Wewe ndiye unaye sikia maombi
(Al-Imran 38) 

رَبَّنَا آمَنَّا بِمَا أَنزَلَتْ وَاتَّبَعْنَا الرَّسُولَ فَاكْتُبْنَا مَعَ الشَّاهِدِينَِ  (آل عمران 53)

Mola wetu Mlezi! Tumeyaamini uliyo yateremsha, na tumemfuata huyu Mtume, basi tuandike pamoja na wanao shuhudia.  (Al-Imran 53)

ربَّنَا اغْفِرْ لَنَا ذُنُوبَنَا وَإِسْرَافَنَا فِي أَمْرِنَا وَثَبِّتْ أَقْدَامَنَا وانصُرْنَا عَلَى الْقَوْمِ الْكَافِرِينَِ    (آل عمران 147)    

Mola wetu Mlezi! Tughufirie madhambi yetu na kupita kwetu kiasi katika mambo yetu, na isimamishe imara miguu yetu na utunusuru tuwashinde kaumu ya makafiri (Al-Imran 147)
 

رَبَّنَا مَا خَلَقْتَ هَذا بَاطِلاً سُبْحَانَكَ فَقِنَا عَذَابَ النَّارِ رَبَّنَا إِنَّكَ مَن تُدْخِلِ النَّارَ فَقَدْ أَخْزَيْتَهُ وَمَا لِلظَّالِمِينَ مِنْ أَنصَارٍ رَّبَّنَا إِنَّنَا سَمِعْنَا مُنَادِيًا يُنَادِي لِلإِيمَانِ أَنْ آمِنُواْ بِرَبِّكُمْ فَآمَنَّا رَبَّنَا فَاغْفِرْ لَنَا ذُنُوبَنَا وَكَفِّرْ عَنَّا سَيِّئَاتِنَا وَتَوَفَّنَا مَعَ الأبْرَارِ رَبَّنَا وَآتِنَا مَا وَعَدتَّنَا عَلَى رُسُلِكَ وَلاَ تُخْزِنَا يَوْمَ الْقِيَامَةِ إِنَّكَ لاَ تُخْلِفُ الْمِيعَاد ِ
(آل عمران 191-194)

Mola wetu Mlezi! Hukuviumba hivi bure. Subhanaka, Umetakasika! Basi tukinge na adhabu ya Moto.
Mola wetu Mlezi! Hakika unaye mtia Motoni umemhizi; na walio dhulumu hawana wasaidizi
Mola wetu Mlezi! Hakika sisi tumemsikia mwenye kuita akiitia Imani kwamba: Muaminini Mola wenu Mlezi; nasi tukaamini. Basi tusamehe madhambi yetu, na utufutie makosa yetu, na utufishe pamoja na watu wema
Mola wetu Mlezi! Na utupe uliyo tuahidi kwa Mitume wako, wala usituhizi Siku ya Kiyama. Hakika Wewe huvunji miadi
(Al-Imran 191 – 194) 

 رَبَّنَا أَخْرِجْنَا مِنْ هَـذِهِ الْقَرْيَةِ الظَّالِمِ أَهْلُهَا وَاجْعَل لَّنَا مِن لَّدُنكَ وَلِيًّا وَاجْعَل لَّنَا مِن لَّدُنكَ نَصِيرًا  (النساء:75)

Mola Mlezi wetu! Tutoe katika mji huu ambao watu wake ni madhaalimu, na tujaalie tuwe na mlinzi anaye toka kwako, na tujaalie tuwe na wa kutunusuru anaye toka kwako
(An-Nisaa 75)

رَبَّنَا آمَنَّا فَاكْتُبْنَا مَعَ الشَّاهِدِينَ   (المائدة:83)

Mola wetu Mlezi! Tumeamini. Basi tuandike pamoja na wanao shuhudia (Al-Maida  83)

رَبَّنَا ظَلَمْنَا أَنفُسَنَا وَإِن لَّمْ تَغْفِرْ لَنَا وَتَرْحَمْنَا لَنَكُونَنَّ مِنَ الْخَاسِرِينَ    (الأعراف23) 

Mola wetu Mlezi! tumejidhulumu nafsi zetu, na kama hutusamehe na kuturehemu, hakika tutakuwa katika wenye kukhasirika  (Al-A'araf 23)

رَبَّنَا لاَ تَجْعَلْنَا مَعَ الْقَوْمِ الظَّالِمِينَ    )الأعراف47)   

Mola Mlezi wetu! Usitujaalie kuwa pamoja na watu walio dhulumu (Al-A'araf 47)

رَبَّنَا افْتَحْ بَيْنَنَا وَبَيْنَ قَوْمِنَا بِالْحَقِّ وَأَنتَ خَيْرُ الْفَاتِحِينَ   (الأعراف:89)

Ewe Mola Mlezi wetu! Tuhukumie baina yetu na kaumu yetu kwa haki, nawe ndiye mbora wa wanao hukumu(Al-A'araf 89) 

رَبَّنَا أَفْرِغْ عَلَيْنَا صَبْرًا وَتَوَفَّنَا مُسْلِمِينَ    ( الأعراف 126)

Ewe Mola Mlezi wetu! Tumiminie uvumilivu na utufishe hali ni Waislamu. (Al-A'araf 126)

أَنتَ وَلِيُّنَا فَاغْفِرْ لَنَا وَارْحَمْنَا وَأَنتَ خَيْرُ الْغَافِرِينَ (الأعراف 155)         

Wewe ndiye Rafiki Mlinzi wetu. Basi tughufirie na uturehemu. Na Wewe ndiye mbora wa kughufiria (Al-A'araf 155)


حَسْبِيَ اللّهُ لا إِلَـهَ إِلاَّ هُوَ عَلَيْهِ تَوَكَّلْتُ وَهُوَ رَبُّ الْعَرْشِ الْعَظِيمِ   (التوبة  129) 

Mwenyezi Mungu ananitosheleza. Hapana mungu isipokuwa Yeye tu. Mimi namtegemea Yeye, na Yeye ndiye Mola Mlezi wa Kiti Kikuu cha Enzi (At-Tawba 129)

رَبَّنَا لاَ تَجْعَلْنَا فِتْنَةً لِّلْقَوْمِ الظَّالِمِينَ وَنَجِّنَا بِرَحْمَتِكَ مِنَ الْقَوْمِ الْكَافِرِينَ   (يونس85-86)

Ewe Mola wetu Mlezi! Usitufanye wenye kutiwa misukosuko na hao watu madhaalimu. 
Na utuokoe kwa rehema yako na watu makafiri  (Yunus 85 – 86 )

رَبِّ إِنِّي أَعُوذُ بِكَ أَنْ أَسْأَلَكَ مَا لَيْسَ لِي بِهِ عِلْمٌ وَإِلاَّ تَغْفِرْ لِي وَتَرْحَمْنِي أَكُن مِّنَ الْخَاسِرِينَ   (هود  74)

Ewe Mola wangu Mlezi! Mimi najikinga kwako nisikuombe nisio na ujuzi nalo. Na kama hunisamehe na ukanirehemu, nitakuwa katika walio khasiri (Hud 47)

رَبِّ اجْعَلْنِي مُقِيمَ الصَّلاَةِ وَمِن ذُرِّيَّتِي رَبَّنَا وَتَقَبَّلْ دُعَاء    (إبرهيم-40)

Mola wangu Mlezi! Nijaalie niwe mwenye kushika Sala, na katika dhuriya zangu pia. Ewe Mola wetu Mlezi, na ipokee dua yangu (Ibrahiim  40)

رَبَّنَا اغْفِرْ لِي وَلِوَالِدَيَّ وَلِلْمُؤْمِنِينَ يَوْمَ يَقُومُ الْحِسَاب   (إبرهيم41 )  

Mola wetu! Unighufirie mimi na wazazi wangu wote wawili, na Waumini, siku ya kusimama hisabu . (Ibrahiim 41)

أَنتَ وَلِيِّي فِي الدُّنُيَا وَالآخِرَةِ تَوَفَّنِي مُسْلِمًا وَأَلْحِقْنِي بِالصَّالِحِينَ  (يوسف:101)

Wewe ndiye Mlinzi wangu katika dunia na Akhera. Nifishe hali ya kuwa ni Muislamu na nichanganyishe na watendao mema (Yusuf 101)
رَّبِّ ارْحَمْهُمَا كَمَا رَبَّيَانِي صَغِيرًا( الإسراء 24 (

Mola wangu Mlezi! Warehemu kama walivyo nilea utotoni.  (Al-Israa 24)

 رَّبِّ أَدْخِلْنِي مُدْخَلَ صِدْقٍ وَأَخْرِجْنِي مُخْرَجَ صِدْقٍ وَاجْعَل لِّي مِن لَّدُنكَ سُلْطَانًا نَّصِيرًا   (الإسراء-80)  

Mola wangu Mlezi! Niingize muingizo mwema, na unitoe kutoka kwema. Na unipe nguvu zinazo toka kwako zinisaidie (Israa 80)

رَبَّنَا آتِنَا مِن لَّدُنكَ رَحْمَةً وَهَيِّئْ لَنَا مِنْ أَمْرِنَا رَشَدًا    (الكهف10) 

Mola wetu Mlezi! Tupe rehema itokayo kwako, na tutengezee uwongofu katika jambo letu. (Al-Kahf 10 ) 

رَبِّ اشْرَحْ لِي صَدْرِي  وَيَسِّرْ لِي أَمْرِي  وَاحْلُلْ عُقْدَةً مِّن لِّسَانِي يَفْقَهُوا قَوْلِي (طه 25-28)  

Ewe Mola wangu Mlezi! Nikunjulie kifua changu,
Na unifanyie nyepesi kazi yangu
Na ulifungue fundo lililo katika ulimi wangu (Taha 25 – 28)

 رَّبِّ زِدْنِي عِلْمًا    (طه 114)  

Mola wangu Mlezi! Nizidishie ilimu (Taha 114)

لا إِلَهَ إِلا أَنتَ سُبْحَانَكَ إِنِّي كُنتُ مِنَ الظَّالِمِينَ  (الأنبياء87) 

Hapana mungu isipo kuwa Wewe Subhanaka Uliye takasika. Hakika mimi nilikuwa miongoni mwa wenye kudhulumu (Al-Anbiyaa 87)

رَبِّ لاَ تَذَرْنِي فَرْدًا وَأَنتَ خَيْرُ الْوَارِثِينَ   (الأنبياء 89 )  

Mola wangu Mlezi! Usiniache peke yangu, na Wewe ndiye Mbora wa wanaorithi
(Al-Anbiyaa 89)

رَبِّ أَنْزِلْنِي مُنْزَلاً مُبَارَكاً وَأَنْتَ خَيْرُ الْمُنْزِلِينَ) المؤمنون 29)

Mola wangu Mlezi! Niteremshe mteremsho wenye baraka, na Wewe ni Mbora wa wateremshaji (Al-Mu'minuun 29)

رَّبِّ أَعُوذُ بِكَ مِنْ هَمَزَاتِ الشَّيَاطِينِ وَأَعُوذُ بِكَ رَبِّ أَن يَحْضُرُونِ (المؤمنون97-98) 

Mola wangu Mlezi! Najikinga kwako na wasiwasi wa mashet'aniNa najikinga kwako, Mola wangu Mlezi, wasinikaribie (Mu'minuun 97 – 98)

  رَبَّنَا آمَنَّا فَاغْفِرْ لَنَا وَارْحَمْنَا وَأَنتَ خَيْرُ الرَّاحِمِينَ    (المؤمنون  109)  

Mola wetu Mlezi! Tumeamini; basi tusamehe na uturehemu, nawe ndiwe Mbora wa wanao rehemu. (Mu'minuun 109)

رَّبِّ اغْفِرْ وَارْحَمْ وَأَنتَ خَيْرُ الرَّاحِمِينَ    (المؤمنون 118)

Mola wangu Mlezi! Samehe na urehemu nawe ni Mbora wa wanao rehemu
(Al-Mu'minuun 118)

رَبِّ هَبْ لِي حُكْماً وَأَلْحِقْنِي بِالصَّالِحِينَ   وَاجْعَلْ لِي لِسَانَ صِدْقٍ فِي الأَخِرِين 
 وَاجْعَلْنِي مِنْ وَرَثَةِ جَنَّةِ النَّعِيمِ  (الشعراء 83 – 85)

Mola wangu Mlezi! Nitunukie hukumu na uniunganishe na watendao mema . Na unijaalie nitajwe kwa wema na watu watakao kuja baadaye. Na unijaalie katika warithi wa Bustani za neema   (As-Shu'araa 83 - 85)

رَبِّ إِنِّي ظَلَمْتُ نَفْسِي فَاغْفِرْ لِي (القصص 16)

Mola wangu Mlezi! Hakika mimi nimejidhulumu nafsi yangu; basi nisamehe (AL-Qasas 16)

رَبِّ بِمَا أَنْعَمْتَ عَلَيَّ فَلَنْ أَكُونَ ظَهِيرًا لِلْمُجْرِمِينَ (القصص  17)

Mola wangu Mlezi! Kwa ulivyo nineemesha, basi mimi sitakuwa kabisa msaidizi wa wakosefu (Al-Qasas 17)

رَبِّ نَجِّنِي مِنَ الْقَوْمِ الظَّالِمِينَ ) القصص  21)

Mola wangu Mlezi! Niokoe na watu madhaalimu . (Al-Qasas 21)

رَبَّنَا اصْرِفْ عَنَّا عَذَابَ جَهَنَّمَ إِنَّ عَذَابَهَا كَانَ غَرَاماً ) الفرقان 65 )

Mola wetu Mlezi! Tuondolee adhabu ya Jahannamu. Hakika adhabu yake ikimpata mtu haimwachi (Al-Furqan 65)
  
 رَبَّنَا هَبْ لَنَا مِنْ أَزْوَاجِنَا وَذُرِّيَّاتِنَا قُرَّةَ أَعْيُنٍ وَاجْعَلْنَا لِلْمُتَّقِينَ إِمَاماً )  الفرقان 74 )

Mola wetu Mlezi! Tupe katika wake zetu na wenetu yaburudishayo macho, na utujaalie tuwe waongozi kwa wachamngu (Al-Furqan 74)

رَبِّ أَوْزِعْنِي أَنْ أَشْكُرَ نِعْمَتَكَ الَّتِي أَنْعَمْتَ عَلَيَّ وَعَلَى وَالِدَيَّ وَأَنْ أَعْمَلَ صَالِحاً تَرْضَاهُ وَأَدْخِلْنِي بِرَحْمَتِكَ فِي عِبَادِكَ الصَّالِحِينَ ) النمل  19)

Ee Mola wangu Mlezi! Nizindue niishukuru neema yako uliyo nineemesha mimi na wazazi wangu, na nipate kutenda mema uyapendayo, na uniingize kwa rehema yako katika waja wako wema (An-Naml 19) 

وَأُفَوِّضُ أَمْرِي إِلَى اللَّهِ إِنَّ اللَّهَ بَصِيرٌ بِالْعِبَادِ  (غافر 44)

Nami namkabidhi Mwenyezi Mungu mambo yangu. Hakika Mwenyezi Mungu anawaona waja wake.(Ghafir 44)

رَبِّ أَوْزِعْنِي أَنْ أَشْكُرَ نِعْمَتَكَ الَّتِي أَنْعَمْتَ عَلَيَّ وَعَلَى وَالِدَيَّ وَأَنْ أَعْمَلَ صَالِحًا تَرْضَاهُ وَأَصْلِحْ لِي فِي ذُرِّيَّتِي إِنِّي تُبْتُ إِلَيْكَ وَإِنِّي مِنْ الْمُسْلِمِينَ  (الأحقاف  15)

Mola wangu Mlezi! Niwezeshe nishukuru neema zako ulizo nineemesha mimi na wazazi wangu, na nitende mema unayo yapenda. Na unitengenezee dhuriya zangu. Hakika mimi nimetubu kwako, na mimi ni miongoni mwa Waislamu. (Al-Ahqaaf 15)

رَبَّنَا اكْشِفْ عَنَّا الْعَذَابَ إِنَّا مُؤْمِنُونَ   )الدخان  12  (  

Mola wetu Mlezi! Tuondolee adhabu hii. Hakika tutaamini  
(Ad-Dhukhan 12)

 رَبَّنَا اغْفِرْ لَنَا وَلِإِخْوَانِنَا الَّذِينَ سَبَقُونَا بِالإِيمَانِ وَلاَ تَجْعَلْ فِي قُلُوبِنَا غِلًّا لِّلَّذِينَ آمَنُوا رَبَّنَا إِنَّكَ رَؤُوفٌ رَّحِيمٌ    (الحشر:(10

Mola wetu Mlezi! Tughufirie sisi na ndugu zetu walio tutangulia kwa Imani, wala usijaalie ndani ya nyoyo zetu undani kwa walio amini. Mola wetu Mlezi! Hakika Wewe ni Mpole na Mwenye kurehemu. (Al-Hashr  10)

 
 رَّبَّنَا عَلَيْكَ تَوَكَّلْنَا وَإِلَيْكَ أَنَبْنَا وَإِلَيْكَ الْمَصِيرُ  
 رَبَّنَا لاَ تَجْعَلْنَا فِتْنَةً لِّلَّذِينَ كَفَرُوا وَاغْفِرْ لَنَا رَبَّنَا إِنَّكَ أَنتَ الْعَزِيزُ الْحَكِيمُ (الممتحنة:4- (5

Mola wetu Mlezi! Juu yako tumetegemea, na kwako tumeelekea, na kwako ndio marejeo.
Mola wetu Mlezi! Usitufanyie mtihani kwa walio kufuru. Na tusamehe, Mola wetu Mlezi. Hakika Wewe ndiye Mwenye nguvu, Mwenye hikima . (Al-Mumttahina 4 -5 )

 
 رَبَّنَا أَتْمِمْ لَنَا نُورَنَا وَاغْفِرْ لَنَا إِنَّكَ عَلَى كُلِّ شَيْءٍ قَدِيرٌ  (التحريم: 8   (
 
Mola wetu Mlezi! Tutimilizie nuru yetu, na utughufirie! Hakika Wewe ni Mwenye uweza juu ya kila kitu .(At-Tahriim 8)

 
 رَبِّ اغْفِرْ لِي وَلِوَالِدَيَّ وَلِمَن دَخَلَ بَيْتِيَ مُؤْمِنًا وَلِلْمُؤْمِنِينَ وَالْمُؤْمِنَاتِ وَلَا تَزِدِ الظَّالِمِينَ إِلَّا تَبَارًا) نوح:28)

Mola wangu Mlezi! Nighufirie mimi na wazazi wangu, na kila aliye ingia nyumbani mwangu kuwa ni mwenye kuamini, na Waumini wote wanaume, na Waumini wanawake. Na wala usiwazidishie walio dhulumu ila kupotea.  (Nuuh 28)