Thursday 11 April 2013

Majina ya Allah Mazuri Sana

Imeandikwa na: Sheikh Rashid Ashueli.

Mwenyezi Mungu S.W.T. katuamrisha sisi Waislamu katika Kitabu Chake, Qurani Tukufu, tumuombe kwa kutumia majina Yake. Kama alivyosema katika Suratil Israa aya ya 110,
 قُلْ ادْعُوا اللَّهَ أَوْ ادْعُوا الرَّحْمَانَ أَيًّا مَا تَدْعُوا فَلَهُ الأَسْمَاءُ الْحُسْنَى…

Maana yake, “Sema: “Mwombeni Allah (Mwenyezi Mungu), au mwombeni Rahman (Mwingi wa Rehema), kwa jina lolote mnalo mwita. Kwani Yeye ana majina mazuri mazuri…”
Pia Mwenyezi Mungu S.W.T. kasema katika Suratil A`araaf aya ya 180,
 وَلِلَّهِ الأَسْمَاءُ الْحُسْنَى فَادْعُوهُ بِهَا وَذَرُوا الَّذِينَ يُلْحِدُونَ فِي أَسْمَائِهِ…

Maana yake, “Na Mwenyezi Mungu ana majina mazuri mazuri; muombeni kwayo. Na waache wale wanaoharibu utakatifu wa majina Yake…”

Na Mtume S.A.W. kasema katika Hadithi ilyopokelewa na Abu Huraira R.A.A. na iliyotolewa na Ahmad, “
‘‘إِنَّ لِلَّهِ تِسْعَةً وَتِسْعِينَ اسْمًا ، مِائَةً إِلاَّ وَاحِدًا مَنْ أَحْصَاهَا دَخَلَ الْجَنَّةَ’’

Maana yake, “Hakika Mwenyezi Mungu ana majina tisini na tisa. Majina mia isipokuwa moja. Atakayeyahifadhi (majina haya na kujua maana yake) ataingia Peponi.”
Pia Mtume S.A.W. kasema katika Hadithi ilyopokelewa na Abu Huraira R.A.A. na iliyotolewa na L-Bukhari, “
‘‘لِلَّهِ تِسْعَةٌ وَتِسْعُونَ اسْمًا ، مِائَةٌ إِلاَّ وَاحِدًا ، لا يَحْفَظُهَا أَحَدٌ إِلاَّ دَخَلَ الْجَنَّةَ’’

Maana yake, “Mwenyezi Mungu ana majina tisini na tisa. Majina mia isipokuwa moja. Hakuna atakayeyahifadhi (majina hayo na kujua maana yake) isipokuwa ataingia Peponi.”

Ingawa Mwenyezi Mungu Mtukufu katuelezea kwamba majina Yake ni tisini na tisa, lakini hata hivyo majina Yake ni zaidi kuliko hivyo. Hakuna mtu yeyote yule hapa duniani anayeyajua majina Yake yote isipokuwa Mwenyewe Muumba wa mbingu na ardhi. Na Majina haya tisini na tisa yanatafsiri sifa Zake nzuri ambazo sifa hizo hazilingani na sifa za viumbe Wake. Ndio maana Mwenyezi Mungu S.W.T. katuamrisha wakati tunapotaka kumuomba basi kwanza kabla ya kuomba dua tumuombe kwa majina hayo, halafu tuombe tunachotaka kuomba. Na wakati wa kumuomba tuwe katika tohara na moyo na kiwiliwili vimnyenyekee Mola Mtukufu, wala tusijishughulishe na mambo mengine.
Ndio maana Mtume S.A.W. kasema,
“Mwenyezi Mungu hapokei dua ya mtu yule moyo wake umeghafilika wakati anapoomba.”
Na majina hayo tisini na tisa yametajwa na Mtume S.A.W. kama yalivyokuja katika Hadithi iliyopokelewa na Abu Huraira R.A.A. na kutolewa na Ttirmidhi.
Na anayetaka kuomba dua kwanza asome,
“AUDHU BILLAAHI MINA SHAITAANI RRAJIYM. BISMI LLAAHI RRAHMAANI RRAHIYM: ALLAAHUMMA INNIY ATAWAJJAHU ILAIKA BIASMAA-IKAL HUSNAA YAA MAN HUWA, “
‘‘اللَّهُ الَّذِي لا إِلَهَ إِلاَّ هُوَ ، الرَّحْمَنُ ، الرَّحِيمُ ، الْمَلِكُ ، الْقُدُّوسُ ، السَّلامُ الْمُؤْمِنُ ، الْمُهَيْمِنُ ، الْعَزِيزُ ، الْجَبَّارُ ، الْمُتَكَبِّرُ ، الْخَالِقُ ، الْبَارِئُ ، الْمُصَوِّرُ ، الْغَفَّارُ ، الْقَهَّارُ ، الْوَهَّابُ ، الرَّزَّاقُ ، الْفَتَّاحُ ، الْعَلِيمُ ، الْقَابِضُ ، الْبَاسِطُ ، الْخَافِضُ ، الرَّافِعُ ، الْمُعِزُّ ، الْمُذِلُّ ، السَّمِيعُ ، الْبَصِيرُ ، الْحَكَمُ ، الْعَدْلُ ، اللَّطِيفُ ، الْخَبِيرُ ، الْحَلِيمُ ، الْعَظِيمُ ، الْغَفُورُ ، الشَّكُورُ ، الْعَلِيُّ ، الْكَبِيرُ ، الْحَفِيظُ ، الْمُقِيتُ ، الْحَسِيبُ ، الْجَلِيلُ ، الْكَرِيمُ ، الرَّقِيبُ ، الْمُجِيبُ ، الْوَاسِعُ الْحَكِيمُ ، الْوَدُودُ ، الْمَجِيدُ ، الْبَاعِثُ ، الشَّهِيدُ ، الْحَقُّ ، الْوَكِيلُ ، الْقَوِيُّ ، الْمَتِينُ ، الْوَلِيُّ ، الْحَمِيدُ ، الْمُحْصِي ، الْمُبْدِئُ ، الْمُعِيدُ ، الْمُحْيِي ، الْمُمِيتُ ، الْحَيُّ ، الْقَيُّومُ ، الْوَاجِدُ ، الْمَاجِدُ ، الْوَاحِدُ ، الصَّمَدُ ، الْقَادِرُ ، الْمُقْتَدِرُ ، الْمُقَدِّمُ ، الْمُؤَخِّرُ ، الأَوَّلُ ، الآخِرُ ، الظَّاهِرُ ، الْبَاطِنُ ، الْوَالِيَ ، الْمُتَعَالِي ، الْبَرُّ ، التَّوَّابُ ، الْمُنْتَقِمُ ، الْعَفُوُّ ، الرَّءُوفُ ، مَالِكُ الْمُلْكِ ذُو الْجَلالِ وَالإِكْرَامِ ، الْمُقْسِطُ ، الْجَامِعُ ، الْغَنِيُّ ، الْمُغْنِي ، الْمَانِعُ ، الضَّارُّ ، النَّافِعُ ، النُّورُ ، الْهَادِي ، الْبَدِيعُ ، الْبَاقِي ، الْوَارِثُ ، الرَّشِيدُ ، الصَّبُوْرُ’’

ALLAAHU LLADHIY LAA ILAAHA ILLA HUWA (Yeye Ndiye Mwenyezi Mungu Ambaye hapana mungu isipokuwa Yeye tu), ARRAHMAANU (Mwingi wa rehema), ARRAHIYMU (Mwenye kurehemu), AL-MALIKU (Mfalme wa milele), AL-QUDDUWSU (Mtakatifu, ametakasika na sifa zote chafu), ASSALAAMU (Mwenye kuleta amani), AL-MU-UMINU (Mtoaji wa amani), AL-MUHAYMINU (Mwenye kuyaendesha Mwenyewe mambo Yake), AL-`AZIYZU (Mshindi katika mambo Yake), AL-JABBAARU (Anayefanya analolitaka), AL-MUTAKABBIRU (Mkubwa), AL-KHAALIQU (Muumbaji), AL-BAARI-U (Mtengenezaji), AL-MUSAWWIRU (Mtia sura), AL-GHAFFAARU (Mwenye kusamehe), AL-QAHHAARU (Mwenye nguvu juu ya kila kitu), AL-WAHHAABU (Mpaji mkuu), ARRAZZAAQU (Mwenye kuruzuku), AL-FATTAAHU (Hakimu), AL-`ALIYMU (Mjuzi wa kila kitu), AL-QAABIDHU (Mwenye kunyima au kuzuia), AL-BAASITU (Mwenye kutoa), AL-KHAAFIDHU (Mfedheheshaji waovu), ARRAAFI`U (Mpandisha daraja), AL-MU`IZZU (Mtoa heshima kwa amtakaye), AL-MUDHILLU (Mnyima heshima kwa amtakaye), ASSAMIY`U (Mwenye kusikia), AL-BASIYRU (Mwenye kuona), AL-HAKAMU (Mwenye kuhukumu), AL-`ADLU (Muadilifu), AL-LLATIYFU (Mwenye kujua yaliyofichikana), AL-KHABIYRU (Mwenye kujua yaliyo dhahiri), AL-HALIYMU (Mpole), AL-`ADHIYMU (Aliye Mkuu), AL-GHAFUWRU (Mwingi wa kusamehe), ASHAKUWRU (Mwenye kushukuru), AL-`ALIYYU (Aliye juu), AL-KABIYRU (Aliye mkuu), AL-HAFIYDHU (Mwenye kuhifadhi), AL-MUQIYTU (Mlinzi), AL-HASIYBU (Mwenye kuhesabu), AL-JALIYLU (Wa hali ya juu), AL-KARIYMU (Mkarimu wa hali ya juu), ARRAQIYBU (Mchungaji), AL-MUJIYBU (Mwenye kujibu), AL-WAASI`U (Mwenye wasaa), AL-HAKIYMU (Mwenye hekima), AL-WADUWDU (Mwenye kupenda waja Wake), AL-MAJIYDU (Mwenye utukufu), AL-BAA`ITHU (Mfufuaji), ASHAHIYDU (Mwenye kushuhudia kila kitu), AL-HAQQU (Wa Haki), AL-WAKIYLU (Mtegemewa), AL-QAWIYYU (Mwenye nguvu), AL-MATIYNU (Aliye madhubuti), AL-WALIYYU (Mlinzi na Msaidizi), AL-HAMIYDU (Mwenye kusifika na kila sifa njema), AL-MUHSIYU (Mwenye kuhesabu), AL-MUBDI-U (Mwenye kuanzisha), AL-MU`IYDU (Mwenye kurejeza), AL-MUHYIYU (Mwenye kuhuisha), AL-MUMIYTU (Mwenye kufisha), AL-HAYYU (Mwenye uhai wa milele), AL-QAYYUWMU (Msimamia kila jambo), AL-WAAJIDU (Mtambuzi), AL-MAAJIDU (Wa kuheshimiwa), AL-WAAHIDU (Mmoja tu), ASSAMADU (Mwenye kukusudiwa kwa kuabudiwa), AL-QAADIRU (Mwenye uwezo wa kufanya au kutokufanya), AL-MUQTADIRU (Mwenye uwezo wa pekee juu ya kila kitu), AL-MUQADDIMU (Mwenye kutanguliza), AL-MU-AKHIRU (Mwenye kuakhirisha), AL-AWWALU (Wa Mwanzo), AL-AAKHIRU (Wa Mwisho), ADHAAHIRU (Wa Dhahiri), AL-BAATINU (Wa Siri), AL-WAALIYA (Mpanga mipango ya watu), AL-MUTA`AALI (Mtukufu Aliye juu), AL-BARRU (Mwema), ATTAWWAABU (Mwenye kupokea toba za waja Wake), AL-MUNTAQIMU (Mlipa kisasi kwa waovu), AL-`AFUWWU (Mwenye kusamehe madhambi), ARRAUFU (Mwenye huruma), MAALIKU L-MULKI DHUL JALAALI WAL IKRAAMI (Mfalme wa wafalme Mwenye utukufu na heshima), AL-MUQSITU (Mtoaji haki sawa kwa kila anayestahiki), AL-JAAMI`U (Mkusanyaji viumbe siku ya Mwisho), AL-GHANIYYU (Tajiri), AL-MUGHNIYU (Mwenye kutajirisha), AL-MAANI`U (Mwenye kuzuia viumbe visidhurike), ADHAARRU (Mwenye kudhurisha), ANNAAFI`U (Mwenye kuleta nafuu), ANNUWRU (Mwenye nuru), AL-HAADIY (Mwongozaji wa kheri), AL-BADIY`U (Mzuaji), AL-BAAQIYU (Mwenye kubakia milele), AL-WAARITHU (Mwenye kurithi kila kitu), ARRASHIYDU (Mwenye kuongoa waja kuiendea njia ya kheri), ASSABUWRU (Mwenye kusubiri).”

Wednesday 10 April 2013

Uvutaji Sigara


Uvutaji wa sigara umeenea na kushamiri dunia nzima licha ya kuwa madhara yake yapo wazi.  Baadhi ya Waislamu wametumbukia katika balaa hili na kuziathiri nyumba zao bila ya kujijua. Kuna sababu tosha zenye kuonyesha uharamu wa jambo hili kwa Muislamu.  Sigara ina athari sana katika dini, afya, mazingira, familia, rasilimali na mengineyo.
 
i.              MADHARA KATIKA DINI
 
Sigara inaathiri  ibada ya mja na inapunguza malipo ya ibada hiyo.  Kwa mfano ibada ya sala ambayo ni nguzo muhimu ya Muislamu;   Kutokana na hadithi iliyosimuliwa na wengi; Amesema Mtume Swalla Llahu Alayhi wa Ssalam
 
 “Mwenye kula Kitungu maji au thawm, basi asiukaribie Msikiti wetu na akae nyumbani”
[Bukhari na Muslim]
 
Tunaona makatazo yamekuja kutokana na harufu mbaya inayotokana na vitu hivyo amabayo huwakirihisha watu pamoja na Malaika katika nyumba za Allaah (Misikitini).
 
Bila ya shaka mdomo wa mvutaji sigara una harufu mbaya zaidi  kuliko vitunguu, ima huwakera watu na Malaika kwa harufu hiyo au kukosa fadhila za sala ya jamaa msikitini kwa mwanamme.
 
i.              MADHARA KATIKA MWILI
 
Hakuna anaepinga madhara ya sigara katika mwili wa binadam.  Utafiti wa kiafya umeyaona haya na kuyaeleza kwa kina; hata imekuwa ni sheria kuweka wazi  maandishi ya tahadhari kwa kila paketi la sigara angalau watu wazinduke.
 
Ndani ya sigara hupatikana kemikali zenye sumu kama vile nicotine, arsenic, carbon monoxide na vyenginevyo ambavyo mvutaji huathirika kidogo kidogo hadi kuua sehemu muhimu za mwili wake.  Athari za zake ni kubwa na ni nyingi; husababisha cancer, TB, mshituko wa moyo, pumu, ubovu wa meno, na huwa ni  chimbuko la  maradhi mengi mengineyo.
 
Allaah Alietukuka anatuonya tusiwe wenyenye kujidhuru.  Suuratu Nnisaa’:29
 
وَلَا تَقۡتُلُوٓاْ أَنفُسَكُمۡ‌ۚ إِنَّ ٱللَّهَ كَانَ بِكُمۡ رَحِيمً۬ا

Wala msijiue, hakika Allah ni mwenye kukurehemuni

 Pia katika Suuratul Baqarah:195
 
وَلَا تُلۡقُواْ بِأَيۡدِيكُمۡ إِلَى ٱلتَّہۡلُكَةِ

Wala msjiitie kwa mikono yenu katika maangamizo
 
Na Mtume Swalla Allahu ‘Alayhi Wasallam anasema katika Hadithi:
 
" لا ضرر ولا ضرار "
 
Kusiwe na kudhuriana wala kulipa dhara.
 
 
ii.    ATHARI KWA AKILI NA MATAMANIO
 
Sigara huathiri akili ya mwanadamu kwa kiasi kikubwa.  Mvutaji mzoefu  anapoikosa  huwa vigumu kwake kufikiri kitu, kutatua tatizo au kuwa makini katika jambo mpaka aipate.  Badala kuwa mtumwa wa Mola wake, hugeuka na kuwa mateka wa sigara yake na kuifanya dhaifu akili na hisia zake.
 
Allah Subhaanahu wa Ta’ala anatueleza katika Suuratu An-Nisaa’:27
 
وَٱللَّهُ يُرِيدُ أَن يَتُوبَ عَلَيۡڪُمۡ وَيُرِيدُ ٱلَّذِينَ يَتَّبِعُونَ ٱلشَّہَوَٲتِ أَن تَمِيلُواْ مَيۡلاً عَظِيمً۬ا

Allah anataka kukukhafifishieni.  Lakini wanaofuata matamanio yao wanataka mkengeuke mkengeuko mkubwa
 
iii.           MADHARA KATIKA MALI
 
Mvutaji sigara hupoteza pesa nyingi karibu kila siku kununulia sigara isiyomletea tija yeyote bali ni kuwafaidisha hao wanaoendesha bishara hii haramu.  Kumbuka kuwa mali tunayoipata tutakuja kuulizwa kwa njia gani tumeichuma na vipi tumeitumia.
 
Katika Suurat An-nisaa’:5  Allah Subhaanahu Wata’ala anatueleza:
 
وَلَا تُؤۡتُواْ ٱلسُّفَهَآءَ أَمۡوَٲلَكُمُ ٱلَّتِى جَعَلَ ٱللَّهُ لَكُمۡ قِيَـٰمً۬اوَٱرۡزُقُوهُمۡ فِيہَا

Wala msiwape wapumbavu mali zenu ambazo Allah amezijaalia kwa maisha yenu
Pia katika Suuratul Israa:26 – 27
 
وَلَا تُبَذِّرۡ تَبۡذِيرًا  إِنَّ ٱلۡمُبَذِّرِينَ كَانُوٓاْ إِخۡوَٲنَ ٱلشَّيَـٰطِينِ‌ۖ

Wala usitawanye (mali yako) kwa ubadhirifu.  Hakika watumiao kwa ubadhirifu ni ndugu wa mashetani
 
Na kutoka kwa Mtume Swalla Allahu ‘Alayhi Wasallam anasema:
 
" إن الله ينهاكم عن قيل وقال ، وكثرة السؤال  وإضاعة المال

Hakika Allah anakukatazeni na mazungumzo yasiyokuwa na faida (huyu kasema au kimesemwa) na kukithirisha kuuliza masuali na kupoteza mali
.
Licha ya nchi za Magharibi kutoa indhaari tu katika paketi kuonesha madhara ya sigara, Maulamaa wa kiislamu takriban wote wamekubaliana kwamba sigara ni haraam. Angalia Fatwa ifuatayo kutoka katika Fataawa Islaamiyah 442/3
 
Kuvuta sigara ni haraam kwa sababu ya kuleta madhara mengi  wakati Allah Subhaanahu Wata’ala amehalalisha kwa waja wake vyote vilivyo vizuri katika vyakula na vinywa na akaharamisha vibaya vyao. Na aina zote za uvutaji ni miongoni mwa vitu vibaya  kwa sababu ya kuleta madhara na kulewesha.
 
Ni vyema kutanabahi ndugu Muislamu na kuachana na mazoea sugu na potofu ya kuvuta sigara. Mvutaji sigara huwa hajali kuvuta mbele ya wale waliomzunguka ndani ya nyumba yake, kama mkewe/mumewe, watoto na wengineo. Huwasababishia kuvuta moshi wa sumu na wale walio karibu nae. Huleta hali mbaya hasa kwa mazingira ya ndani ya nyumba na ni mfano mbaya kwa kile kinachochungwa (mke na watoto) ndani ya nyumba hiyo.
 
Ndugu yangu Muislamu , kama ni miongoni mwa wenye kuendeleza uovu huu basi rudi kwa Mola wako kwa moyo ulio mwepesi wenye kusikiliza nasaha na kukubali yale yote yanayotoka kwa Mola kwa ajili ya kuinusuru nafsi yako kwanza, kisha dini yako, kisha akili yako, kisha familia yako, kisha mali yako na kadhalika.

Tuesday 9 April 2013

Yenye kuhatarisha nyumba

Imeandikwa na:   Ummu Nassra


BISMILLAHIR-RAHMAANIR-RAHIIM

UTANGULIZI

Hakika shukrani zote ni zake Allaah Subhaanahu Wata’ala, tunaemshukuru, tunaemtegemea, kumtaka msamaha na kutubu kwake. Tunajikinga Kwake Allaah Subhaanahu Wata’ala kutokana na shari za nafsi zetu na makosa ya matendo yake. Mwenye kuongolewa na Allaah hakuna wa kumpotoa, na mwenye kumpotoa hakuna wa kumuongoa.  Rehma na Amani ziwe juu ya kipenzi chetu Muhammad SwallaAllahu ‘Alayhi wa Aalihi wa Sallam.

‘Amma Ba’ad

Nyumba ni neema kubwa ambayo mwanadamu amebarikiwa, [An-Nahl 16:80]

وَٱللَّهُ جَعَلَ لَكُم مِّنۢ بُيُوتِڪُمۡ سَكَنً۬ا

Na MwenyeziMungu amekujaalieni majumba yenu yawe maakaazi (yenu)

Kuweka mazingira sahihi ndani ya majumba ni jukumu la kila muislam mume na mke, na ni lazima mazingira hayo yaoane sambamba na sheria alizotuwekea Allah Subhanahu wa Ta’ala.   Moja kati ya njia ya kuyafikia hayo ni kuepukana na  kila aina ya uovu na uharibifu ndani ya majumba. 

Kuna sababu nyingi kwa mwenye kuamini kuwa makini katika kuijenga na kuilinda nyumba yake katika misingi mema ya kiislam.  Miongoni mwa sababu hizo ni:

1.    Kujilinda yeye pamoja na familia yake kutokana na moto wa jahannam,  na kujiweka mbali na ghadhabu zake. [At-Tahriym 66:6]


يَـٰٓأَيُّہَا ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ قُوٓاْ أَنفُسَكُمۡ وَأَهۡلِيكُمۡ نَارً۬ا وَقُودُهَا ٱلنَّاسُ وَٱلۡحِجَارَةُ


Enyi mlioamini! Jiokoeni nafsi zenu na watu wenu na moto ambao ambao kuni zake ni watu  na mawe.

2.    Kujua wajibu wake juu ya jukumu la kuchunga nyumba, na kujiweka tayari kujibu kwa kila unachokichunga.  Hadith:

Kutoka kwa Abdullah, Allah amuwie radhi, kwamba  Mtume SwallaAllahu ‘Alayhu wa Aalihi wa Ssallam amesema:

“Nyote ni wachunga na nyote mtaulizwa juu ya mlivyovichunga. Kiongozi anaewaongoza watu ni mchunga na ataulizwa juu wachungwa wake. Mwanamume ni mchunga kwa watu wake wa nyumbani na ataulizwa juu ya wachungwa wake. Na mwanamke ni mchunga kwa nyumba ya mumewe na watoto wake nae ataulizwa juu ya wachungwa wake .Mtumwa ni mchunga katika mali ya bwana wake na anawajibika juu ya mali hiyo. Hakika nyote ni wachunga na na kila mmoja wenu anawajibika juu ya wachungwa wake”   

 

                                                                                             

Imesimuliwa na Bukhari na Muslim

3.    Nyumba ni sehemu ya hifadhi kwa binaadamu, kujiweka mbali na kila aina ya ubaya na uovu ukiwa wa mnyama, binaadamu au majini, na kupata utulivu ndani yake.  Amesema Mtume SwallaAllahu ‘Alayhu wa Ssallam: 

Usalama wa mtu katika wakati wa fitnah ni kubakia nyumbani kwake.

Kilicho muhimu zaidi ni kuzingatia kuwa nyumba ni sehemu nyeti (muhimu) ya kujenga mazingira mazuri ya kiislam, kwani jamii bora hujengeka kuanzia nyumbani.   Kwa masikitiko makubwa majumba yetu mengi yamejiweka mbali na mafundisho sahihi ya kiislam. 

InshaAllaah katika makala hizi tutaweza kugusia na kutanabahisha baadhi ya vitu ambavyo huchangia kwa kiasi kikubwa kuharibika mfumo wa kiislam ndani ya majumba na jamii kwa ujumla, na kujaribu kutafuta njia muafaka kurejesha mazingira mazuri ndani ya majumba yetu.

Kuna mambo mengi ya wazi kabisa ambayo sheria yameyakataza katika Uislamu na jamii imeghafilika nayo.  Mambo hayo huchangia  kuharibika na kuhatarisha mfumo  mzima wa kiislam ndani ya majumba.  Miongoni mwa yenye kuhatarisha ni haya yafuatayo:

 

TELEVISHENI (TV) - LUNINGA.

  

Televisheni kama inavyojuilikana (TV) ni chombo ambacho hakikosekani katika kila nyumba.  Kama kitatumika vizuri chombo hicho kwa mambo ya kheri yenye kuzidisha imani, kupeleka dini mbele, kukuweka mbali na maasi na kuhifadhi dini ya mja kinaweza kuleta faida.  Na kama kitatumika vibaya kinaweza kuathiri familia kwa asilimia kubwa kabisa.

Ukweli ni kuwa kuangalia TV kuna madhara mengi na makubwa kuliko faida. Familia za kiislam zinaogelea kwa kasi kubwa bila ya kujali au kuona mabaya ya chombo hicho. 

Tuchukue mfano mdogo tu wa athari za televisheni kwa watoto kama utafiti huu mdogo uliofanyika hapa Uingereza unavyofafanua.

 

Watoto wenye kuangalia televisheni kwa zaidi ya masaa mawili kila siku wanakabiliwa na hatari ya kupatwa na ugonjwa wa athma. Uchunguzi huo umeonyesha kuwa, kuangalia televisheni kwa muda mrefu kunaleta uwezekano wa kupata athma uongezeke mara mbili kwa watoto.

Jinsi mfumo wa kupumua unavyofanya kazi wakati mtoto anapokaa tu bila kufanya chochote, hupelekea kutokea mabadiliko katika mapafu pamoja na magojwa mengine ya kupumua ikiwemo athma.

Unene wa kupita kiasi pamoja na kutokufanya mazoezi kunakosababishwa na kuangalia muda mrefu televisheni hupelekwa kutokea hali hiyo Wataalamu wamesema kuwa, kuishi maisha ya kutokuwa na harakati yoyote katika umri mdogo hupelekea kuongezeka uwezekano wa hatari ya kupata athma ukubwani.

Hivyo wamewashauri wazazi kuwashajiisha watoto wao kufuata maisha ya kawaida ya kuwa na mishughuliko na kupunguza muda wanaoutumia kuangalia TV.

Wataalamu wa Uingereza wametoa taarifa hiyo baada ya kuwafanyia uchunguzi watoto 3,000  kuanzia wale waliozaliwa mpaka walio na miaka 11.

Hasara moja ya kupoteza muda kuangalia TV inaweza kuzaa makosa mengi ndani yake.  Kuona na kusikiliza kunawavutia wengi na kuwafanya watu kutawaliwa na tabia hiyo na kutoweza kuiepuka.  Hakuna shaka kuwa jamii hasa watoto imeathirika sana na jambo hili.  TV inasababisha kwa kiasi kikubwa watoto wa Kiislamu kutumbukia katika tabia zisizo na maadili, ulevi, uzinzi, kukosa heshima, kujinasibisha na uzungu na mengi mengine maovu tunayoyaona katika jamii zetu.  Yote hayo wanayaona na kujifunza moja kwa moja kutoka kwenye TV.

Mtu huhisi kuwa anapoteza wakati tu kujistarehesha na TV, anayakata masaa na dakika kwa ajili ya chombo hicho, ni makosa!!.  TV si chombo cha starehe, bali ni chombo kinachotumika kuchochea hisia, kubadilisha muelekeo na utiifu wa mtu. Na ndiyo hali halisi ndugu yangu Muislamu kama bado hujatanabahi.


Yafaa Waislamu tuzinduke na kuziona faida chache na hasara nyingi za chombo hiki.  Kama tunaona ni neema hakika tutakuja kuulizwa namna tulivyoitumia.  [At-Takaathur 102:8]

ثُمَّ لَتُسۡـَٔلُنَّ يَوۡمَٮِٕذٍ عَنِ ٱلنَّعِيمِ

Kisha mtaulizwa siku hiyo juu ya neema mlizopewa mlizitumiaje.

Na kwa hakika hata  masikio na macho tunayoyatumia kwa chombo hicho pia tutakuwa ni wenye kuulizwa. Hivyo ni juu yetu kuchagua ni kipi cha kutizama. [Al-Israa 17:36]. 

إِنَّ ٱلسَّمۡعَ وَٱلۡبَصَرَ وَٱلۡفُؤَادَ كُلُّ أُوْلَـٰٓٮِٕكَ كَانَ عَنۡهُ مَسۡـُٔولاً

Hakika masikio na macho na moyo, hivyo vyote vitaulizwa

Tv ni kama upanga ukiutumia vizuri unaweza kuleta faida na ukiitumia vibaya unaweza kuleta madhara makubwa.  Kwa mfano mtu akiweza kuidhibiti na kuangalia kwa nadra kwa vipindi vya kheri vyenye kwenda sambamba na dini yetu inaweza kukubalika, bali ni wachache wenye kufanya hivyo.  Wengi wao wameogolea na kuangalia tu bila hata ya kujali faida na hasara zake, na hii ndio iliopelekea madhara kuwa mengi kuliko faida.



 Miongoni mwa madhara ya TV ni:

-      Kunapoteza wakati bure na kupuuza mengi ya wajibu

-      Inaeneza tamaduni za kikafiri kama ni njia moja ya kuigwa katika maisha

-      Inaeneza upotofu na uhuru kwa kupitia katika michezo, nyimbo matangazo yasiyo ya heshima ambayo hupelekea watizamaji kutumbuka na tabia hizo za kijinga.

-      Mazoea ya kuangalia TV yanaharibu akili na kuathiri afya ya mja.


Hivyo kama kuna watu wazuri wenye kumuogopa Allah  Subhaanahu Wata’ala na kuonyesha mazuri yenye faida bila ya kukiuka mipaka ya Allah, basi unaweza kuangalia na ni jambo la kupendeza kwa wengi. Ni vyema kuchunga aina gani ya vipindi tunavyoangalia ndani ya majumba yetu.

Ni wajibu wa kila mtu kueleweka wazi madhara na faida ya kifaa hichi ili tuweze kukitumia vyema ama kujiepusha nacho kabisa ikiwa tutashindwa kuweka vidhibiti katika majumba jinsi chombo hiki kitumike katika kunufaisha, kuelimisha na kuleta faida na si kuharibu, kupoteza muda na kupelekea jamii iliyozugika na hatimaye kupotoka na kupotosha wengine. 

 

 

 

UVUTAJI SIGARA

Uvutaji wa sigara umeenea na kushamiri dunia nzima licha ya kuwa madhara yake yapo wazi.  Baadhi ya Waislamu wametumbukia katika balaa hili na kuziathiri nyumba zao bila ya kujijua. Kuna sababu tosha zenye kuonyesha uharamu wa jambo hili kwa Muislamu.  Sigara ina athari sana katika dini, afya, mazingira, familia, rasilimali na mengineyo.

i.              MADHARA KATIKA DINI

Sigara inaathiri  ibada ya mja na inapunguza malipo ya ibada hiyo.  Kwa mfano ibada ya sala ambayo ni nguzo muhimu ya Muislamu;   Kutokana na hadithi iliyosimuliwa na wengi; Amesema Mtume Swalla Llahu Alayhi wa Ssalam

 “Mwenye kula Kitungu maji au thawm, basi asiukaribie Msikiti wetu na akae nyumbani”

[Bukhari na Muslim]

Tunaona makatazo yamekuja kutokana na harufu mbaya inayotokana na vitu hivyo amabayo huwakirihisha watu pamoja na Malaika katika nyumba za Allaah (Misikitini).   

Bila ya shaka mdomo wa mvutaji sigara una harufu mbaya zaidi  kuliko vitunguu, ima huwakera watu na Malaika kwa harufu hiyo au kukosa fadhila za sala ya jamaa msikitini kwa mwanamme.

 

i.              MADHARA KATIKA MWILI

Hakuna anaepinga madhara ya sigara katika mwili wa binadam.  Utafiti wa kiafya umeyaona haya na kuyaeleza kwa kina; hata imekuwa ni sheria kuweka wazi  maandishi ya tahadhari kwa kila paketi la sigara angalau watu wazinduke.

Ndani ya sigara hupatikana kemikali zenye sumu kama vile nicotine, arsenic, carbon monoxide na vyenginevyo ambavyo mvutaji huathirika kidogo kidogo hadi kuua sehemu muhimu za mwili wake.  Athari za zake ni kubwa na ni nyingi; husababisha cancer, TB, mshituko wa moyo, pumu, ubovu wa meno, na huwa ni  chimbuko la  maradhi mengi mengineyo.

Allaah Alietukuka anatuonya tusiwe wenyenye kujidhuru.  Suuratu Nnisaa’:29

وَلَا تَقۡتُلُوٓاْ أَنفُسَكُمۡ‌ۚ إِنَّ ٱللَّهَ كَانَ بِكُمۡ رَحِيمً۬ا

Wala msijiue, hakika Allah ni mwenye kukurehemuni

 Pia katika Suuratul Baqarah:195

وَلَا تُلۡقُواْ بِأَيۡدِيكُمۡ إِلَى ٱلتَّہۡلُكَةِ

Wala msjiitie kwa mikono yenu katika maangamizo

Na Mtume Swalla Allahu ‘Alayhi Wasallam anasema katika Hadithi:

" لا ضرر ولا ضرار "

Kusiwe na kudhuriana wala kulipa dhara.

 

ii.            ATHARI KWA AKILI NA MATAMANIO

Sigara huathiri akili ya mwanadamu kwa kiasi kikubwa.  Mvutaji mzoefu  anapoikosa  huwa vigumu kwake kufikiri kitu, kutatua tatizo au kuwa makini katika jambo mpaka aipate.  Badala kuwa mtumwa wa Mola wake, hugeuka na kuwa mateka wa sigara yake na kuifanya dhaifu akili na hisia zake. 

Allah Subhaanahu wa Ta’ala anatueleza katika Suuratu An-Nisaa’:27

وَٱللَّهُ يُرِيدُ أَن يَتُوبَ عَلَيۡڪُمۡ وَيُرِيدُ ٱلَّذِينَ يَتَّبِعُونَ ٱلشَّہَوَٲتِ أَن تَمِيلُواْ مَيۡلاً عَظِيمً۬ا

Allah anataka kukukhafifishieni.  Lakini wanaofuata matamanio yao wanataka mkengeuke mkengeuko mkubwa

 

iii.           MADHARA KATIKA MALI

Mvutaji sigara hupoteza pesa nyingi karibu kila siku kununulia sigara isiyomletea tija yeyote bali ni kuwafaidisha hao wanaoendesha bishara hii haramu.  Kumbuka kuwa mali tunayoipata tutakuja kuulizwa kwa njia gani tumeichuma na vipi tumeitumia. 

Katika Suurat An-nisaa’:5  Allah Subhaanahu Wata’ala anatueleza:

وَلَا تُؤۡتُواْ ٱلسُّفَهَآءَ أَمۡوَٲلَكُمُ ٱلَّتِى جَعَلَ ٱللَّهُ لَكُمۡ قِيَـٰمً۬ا وَٱرۡزُقُوهُمۡ فِيہَا

Wala msiwape wapumbavu mali zenu ambazo Allah amezijaalia kwa maisha yenu

Pia katika Suuratul Israa:26 – 27

وَلَا تُبَذِّرۡ تَبۡذِيرًا  إِنَّ ٱلۡمُبَذِّرِينَ كَانُوٓاْ إِخۡوَٲنَ ٱلشَّيَـٰطِينِ‌ۖ

Wala usitawanye (mali yako) kwa ubadhirifu.  Hakika watumiao kwa ubadhirifu ni ndugu wa mashetani

 

Na kutoka kwa Mtume Swalla Allahu ‘Alayhi Wasallam anasema:

" إن الله ينهاكم عن قيل وقال ، وكثرة السؤال  وإضاعة المال

Hakika Allah anakukatazeni na mazungumzo yasiyokuwa na faida (huyu kasema au kimesemwa) na kukithirisha kuuliza masuali na kupoteza mali.

Licha ya nchi za Magharibi kutoa indhaari tu katika paketi kuonesha madhara ya sigara, Maulamaa wa kiislamu takriban wote wamekubaliana kwamba sigara ni haraam. Angalia Fatwa ifuatayo kutoka katika Fataawa Islaamiyah 442/3

Kuvuta sigara ni haraam kwa sababu ya kuleta madhara mengi  wakati Allah Subhaanahu Wata’ala amehalalisha kwa waja wake vyote vilivyo vizuri katika vyakula na vinywa na akaharamisha vibaya vyao. Na aina zote za uvutaji ni miongoni mwa vitu vibaya  kwa sababu ya kuleta madhara na kulewesha.

 

Ni vyema kutanabahi ndugu Muislamu na kuachana na mazoea sugu na potofu ya kuvuta sigara. Mvutaji sigara huwa hajali kuvuta mbele ya wale waliomzunguka ndani ya nyumba yake, kama mkewe/mumewe, watoto na wengineo. Huwasababishia kuvuta moshi wa sumu na wale walio karibu nae. Huleta hali mbaya hasa kwa mazingira ya ndani ya nyumba na ni mfano mbaya kwa kile kinachochungwa (mke na watoto) ndani ya nyumba hiyo.

Ndugu yangu Muislamu , kama ni miongoni mwa wenye kuendeleza uovu huu basi rudi kwa Mola wako kwa moyo ulio mwepesi wenye kusikiliza nasaha na kukubali yale yote yanayotoka kwa Mola kwa ajili ya kuinusuru nafsi yako kwanza, kisha dini yako, kisha akili yako, kisha familia yako, kisha mali yako na kadhalika.

 

MUZIKI NA NYIMBO


Miongoni mwa yenye kuzoeleka katika majumba yetu ni mziki. Kwa kweli mziki umeenea kila pembe ya dunia kiasi ambacho unawaumiza Waislamu wengi kimwili na kiakili bila ya kujijua. Kila mtu amekabiliana na hali ambayo humuingiza kusikiliza muziki ama kwa hiari au kwa lazima. Kuongezeka umaarufu wa muziki kunahatarisha sana majumba ya Waislamu na hatimae kutumbukia katika balaa hilo usiku na mchana

Ukweli ni kuwa muziki unaathiri sana mioyo ya Waislamu na kuishughulisha akili kwa mambo ya kipuuzi. Tunatumia muda na pesa nyingi katika kununulia CD za majimbo yasiyo na faida, zana za miziki, na hata kuwatumbukiza watoto wetu kwa vifaa (toys) mbali mbali vilivyojaa miziki; Tunajitia makosani na kuuporomoa itikadi sahihi ya Muislamu. Kuna dalili tosha katika Quraan na Sunnah zenye kuonyesha uharamu wa muziki. Katika Suurat Luqmaan aya ya 6 Allaah Subhaanahu wa Ta'ala anatueleza:

((وَمِنَ النَّاسِ مَن يَشْتَرِي لَهْوَ الْحَدِيثِ لِيُضِلَّ عَن سَبِيلِ اللَّهِ بِغَيْرِ عِلْمٍ وَيَتَّخِذَهَا هُزُوًا أُولَئِكَ لَهُمْ عَذَابٌ مُّهِينٌ))


Na miongoni mwa watu wapo wanaonunua maneno ya upuuzi, ili wawapoteze watu na njia ya Mwenyezi Mungu pasipo kujua, na wanaichukulia ni maskhara. Hao watapata adhabu ya kuwafedhehesha Maulamaa pamoja na wafasiri wengi wa Quraan wameeleza kuwa neno "Lahwal-hadith" katika aya hii inakusudiwa nyimbo na zana za miziki.

Mfano Ibn Mas'uud Radhiya Allahu 'anhu amesema kuhusu Aya hii "Naapa kwa Allah hii inamaanisha ni nyimbo" Pia miongoni mwa hadithi zenye kuonyesha uharamu wa ngoma na kila aina ya muziki ni hadithi mashuhuri ya Mtume Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam:
"Watakuweko watu katika Ummah wangu watakaojaribu kuhalilisha zinaa, uvaaji wa hariri, pombe na muziki. Bukhari
Ni vyema tuelewe kuwa hakuna chochote alichokikataza Allah Subhaanahu wa Taala isipokuwa kina madhara ndani yake katika ustawi wa jamii. Jua kuwa miziki tunayoichezesha majumbani yanaweza kuchochea hisia za mja, jazba pamoja na muengezeko wa mapigo ya moyo na kushughulisha akili.

Ujumbe unaopatikana katika miziki na nyimbo nyingi hasa wakati huu tulionao huenda kinyume kabisa na maadili ya Kiislamu, huamsha hisia za mapenzi, uzinzi na uhuru wa kufanya lolote bila ya kuzingatia wajibu wa mja. Umefika wakati kwa Waislamu kutanabahi na kujaribu kwa kadiri ya uwezo wetu kuepukana na balaa hili na kurejesha mandhari nzuri ndani ya majumba yetu. Tusiziuwe nyumba zetu kwa sauti za shetani (nyimbo na miziki) na kuwawekea makaazi, Ni lazima tuziuhishe nyumba zetu kuwa ni sehemu ya kumkumbukwa Allah Subhaanahu wa Taala (dhikr) kwa kila hali; kwa sala, kusoma Quraan, na vitabu vyengine vya dini pamoja na masuala mbali mbali yanayowahusu Waislamu. Hii itatupelekea kuzungukwa na Malaika, kulindwa na kupata ridhaa ya Allah Subhaanahu wa Taala.

 MCHANGANYIKO WA WANAUME NA WANAWAKE

Moja katika jambo linaloonekana ni la kawaida hasa katika majumba yetu ni michanganyiko ya wanaume na wanawake (Ikhtilaatw). Ni wajibu wa kila Muislamu kuelewa hukumu ya kisheria juu ya jambo hili. Ikhtilaatw ni kuchanganyika kwa wanawake na wanaume waliokuwa sio maharim ima kwa wingi au uchache katika sehemu moja. Hali hii imezoeleka sana majumbani mwetu, katika shughuli zetu zikiwa ni za furaha au misiba au hata siku za kawaida.

Tuelewe kuwa mijumuiko ya aina hii na kudhihirika mapambo ni kitu kilichokatazwa katika sheria kwa sababu huwa ni mzizi wa fitina na ni kichochezi cha maasia mengine kwani shaytwan huwa pamoja nao. Katika hadithi iliyosimuliwa na 'Umar, Radhiya Llahu 'Anhu inatueleza:
Kutoka kwa Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam): Hachanganyiki mwanamume na mwanamke ila shaytwaan huwa ni watatu wao. [At-Tirmidhiy]


Dini yetu imetuwekea adabu maalum; na kama kuna ulazima wa kuchanganyika majumbani, basi ni vyema kuwe na sehemu tofauti kati ya wanaume na wanawake pindi wakikujia kwao. Tunatakiwa tuwe na hadhari tunapotembelewa na mgeni, hata kama ni ndugu wa mume au mke. Mtume Swalla Llahu 'Alayhi wa Ssalaam aliwaeleza maswahaba zake na Waislamu wote kuwa: Tahadharini kuingilia majumbani mwao wanawake; Wakasema: Ewe Mjumbe wa Allaah, je, vipi kuhusu shemeji? Akasema: Shemeji ni mauti Al-Bukhaariy na Muslim]

Pia Allaah Subhanahu wa Taala anatueleza katika Suuratul Al-Ahzaab: 53
Nanyi mnapowauliza (wakeze) waulizeni nyuma ya pazia. Kufanya hivyo kunasafisha nyoyo zenu za zao. Ni jukumu letu kama ni wazazi kuzielewa sheria hizi na kuzidi kuzipamba nyumba zetu katika mandhari nzuri ya kiislam. Hii itasaidia hata na vizazi vyetu kuinukia kwa maadili na tabia njema na kujua mipaka yao. Na kama itatokea kwa mwanamme au mwanamke kutembea au kutembelewa na kukutana na mwenyeji wa jinsia tofauti basi na tumuogope Allaah na kujihifadhi kwa kadiri ya uwezo wetu, bila ya kurefusha mazungumzo.

Allaah Alietukuka Anatufahamisha katika Suuratu Nnuur:30-31

Wambie waumini wanaume wainamishe macho yao (wasitazame yaliyokatazwa) na wazilinde tupu zao hili ni takaso kwao; bila ya shaka Allaah anazo habari za wanayoyafanya. Na wambie waumini wanawake wainamishe macho yao na wazilinde tupu zao, wala wasidhihirishe viungo vyao isipokuwa vinavyodhihirika.


 MAMBO YA KUZINGATIA HASA KWA KINA MAMA

Miongoni mwa mambo yenye kuporomoa Uislamu katika majumba ya Waislamu ni udhaifu wa baadhi ya kinamama kuupuuza au kutoyatambua mafunzo muhimu yanayowahusu ambayo dini yetu yameyaweka wazi. Miongoni mwa hayo ni haya yafuatayo:

i.              Kudhihirisha kwa Mapambo:

Kawaida, wanawake huwa na mvuto wa kimaumbile. Hivyo Uislamu umeweka sheria maalum juu ya kuhifadhi maumbile hayo, heshima, staha pamoja na hadhi zao. Suurat Al-Ahzab: 59 Allaah Subhaanahu Wata’ala Anatueleza:


يَـٰٓأَيُّہَا ٱلنَّبِىُّ قُل لِّأَزۡوَٲجِكَ وَبَنَاتِكَ وَنِسَآءِ ٱلۡمُؤۡمِنِينَ يُدۡنِينَ عَلَيۡہِنَّ مِن جَلَـٰبِيبِهِنَّۚ ذَٲلِكَ أَدۡنَىٰٓ أَن يُعۡرَفۡنَ فَلَا يُؤۡذَيۡنَۗ

Ewe Mtume! Waambie wake zako na binti zako na wanawake wa Kiislamu wajiteremshie uzuri shungi zao, kufanya hivyo kutapelekea wepesi wajuulikane (kuwa ni watu wa heshima) ili wasiudhiwe

.

Ni mazoea ya wanawake wengi wanapotaka kutoka au kupata wageni majumbani mwao hudhihirisha mapambo yao yakiwemo maumbile yao kwa nguo za wazi au za kubana, manukato pamoja na mapambo mengine.  Hali hii inaweza kusababisha vishawishi vingi, fitina na mtafaruku katika familia.  Ni lazima tuwe waangalifu ni nani waliotuzunguka hasa wale wasiotakikana kuona mapambo hayo (wasiokuwa mahrim).  Suuratu Nnuur: 31 Allaah Subhaanahu Wata’ala Anatuhimiza.

 

وَقُل لِّلۡمُؤۡمِنَـٰتِ يَغۡضُضۡنَ مِنۡ أَبۡصَـٰرِهِنَّ وَيَحۡفَظۡنَ فُرُوجَهُنَّ وَلَا يُبۡدِينَ زِينَتَهُنَّ إِلَّا مَا ظَهَرَ مِنۡهَا‌ۖ

Na waambie waumini wanawake wainamishe macho yao na wazilinde tupu zao, wala wasidhihirishe  viungo vyao isipokuwa vinavyodhihirika.

Kujistiri kwa hijabu ya ki shari’ah kunapelekea kupata ridhaa ya Allaah Subhaanahu Wata’ala na kutii amri Yake, kujitakasa pamoja na kuheshimika na wengine.

 

i.              Kutoka toka bila ya sababu maalum

Wanawake wa Kiislamu hawajakatazwa kutoka nje ima kwa, kufanya kazi, kutembelea wazee, marafiki au katika shughuli za kijamii, ikiwa hakuna kipingamizi chochote cha shari’ah kitachowazuia. Muhimu ni kuchunga na kuielewa mipaka iliyowekwa katika dini.  Hata hivyo kutulia majumbani ni bora zaidi kwao na kutawaepusha na mambo mengi. 

Ulimwengu tulionao, kina mama wengi imekuwa ni adimu kutulia majumbani mwao, hii hupelekea familia kukosa utulivu, kizazi kukosa malezi na maadili mema kutokana na wazazi huwa hawana muda wa kutosha na watoto wao. Allaah Subhaanahu Wata’ala Anatufahamisha katika Suuratul Ahzaab: 33

وقَرۡنَ فِى بُيُوتِكُنَّ وَلَا تَبَرَّجۡنَ تَبَرُّجَ ٱلۡجَـٰهِلِيَّةِ ٱلۡأُولَىٰۖ

Na kaeni majumbani mwenu, wala msionyeshe mapambo yenu kama walivyokuwa wakionyesha wanawake wa zama za ujahili (ujinga)

 

Hivyo ni lazima kwa kinamama kuzingatia ni sababu gani zitakazowatoa ndani ya majumba yao, kuwe na mtizamo na upeo wa hali ya juu kabla ya kuamua kutoka. Na ikibidi kutoka basi azingatie mipaka ya Allaah Subhaanahu Wata’ala, kusiwe na aina yoyote ya mapambo kama vipodozi, manukato, udi na mengineyo. Awe amejihifadhi vizuri kwa mujibu wa shari’ah. Kufanya hivyo kutahifadhi utu wao, dini yao pamoja na kizazi chao kwa ujumla.

 

HITIMISHO

Ni wajibu wa Waislamu kudumisha mafunzo mazuri tuliyoekewa wazi katika dini yetu. Jamii bora huanza majumbani. Ni vyema kwa wasimamizi wa majumba kusaidiana na kushirikiana pamoja katika kulinda na kuhifadhi mazingira mazuri kwa kumuogopa Allaah Subhaanahu Wata’al. Ni juu yetu kuwa waangalifu wa kile tunachokikuza - watoto, kwani wao husoma kutoka kwetu. 

Ni jukumu la kila mmoja wetu kusoma na kujifunza kitu gani Allaah Subhaanahu Wata’ala Anapendezeshwa nacho na kipi Amekikataza hasa ndani ya majumba yetu ili tuishi hali ya kuwa Allaah Subhaanahu Wata’ala Ameturidhia. Tuzipambe nyumba zetu kwa misingi ya Kiislamu ili zitofautike na zile zisizo za Kiislamu. Huu ni ukumbusho kwa wenye kukumbuka.

Tumuombe Allaah Atuongoze katika haki na kuifuata, tuijuwe batili na kuiacha, Atupe tawfiyq, Atulinde na Kutuweka katika msimamo ulio sawa. Aamiyn

 

 








Wednesday 3 April 2013

Swalatul-Istikhara

(Swala ya kuomba ushauri kutoka kwa Allah)



Dua ya Swalatul-Istikhara

Amesema Jaabir Bin Abdillah رضى الله عنه “alikuwa Mtume wa Mwenyezi Mungu akitufundisha Swala ya Istikhara kama vile anavyotufunza sura ya Qur’an. Anasema
رضى الله عنه

 ‘Akikusudia mmoja wenu kufanya jambo, aswali rakaa mbili zisizo za faradhi, kisha aseme:


اللّهُـمَّ إِنِّـي أَسْتَخيـرُكَ بِعِاْـمِك، وَأسْتَقْـدِرُك
َ بِقُـدْرَتِـك، وَأَسْـألُـكَ مِنْ فَضْـلِكَ العَظـيم، فَإِنَّـكَ تَقْـدِرُ وَلا أَقْـدِر، وَتَـعْلَـمُ وَلا أَعْلَـم، وَأَنْـتَ عَلاّمُ الغُـيوب، اللّهُـمَّ إِنْ كُنْـتَ تَعْـلَمُ أَنَّ هـذا الأمْـرَ (وَيُسَـمِّي حاجته) خَـيْرٌ لي في دينـي وَمَعـاشي وَعاقِـبَةِ أَمْـري، ( عَاجِلِهِ و آجِلِه) فَاقْـدُرْهُ لي وَيَسِّـرْهُ لي ثـمَّ بارِكْ لي فيـه، وَإِنْ كُنْـتَ تَعْـلَمُ أَنَّ هـذا الأمْـرَ شَـرٌ لي في دينـي وَمَعـاشي وَعاقِـبَةِ أَمْـري، ( عَاجِلِهِ و آجِلِه) فَاصْرِفْـهُ عَنّيِ وَاصْرِفْني عَنْـهُ وَاقْـدُرْ ليَ الخَـيْرَ حَيْـثُ كانَ ثُـمَّ أَرْضِـني بِِـه .



Ewe Mwenyezi Mungu hakika mimi nakutaka ushauri (muelekezo) kwa ujuzi Wako, na nakuomba uniwezeshe kwa uwezo Wako, na nakuomba fadhila Zako kubwa, hakika Wewe unaweza, nami siwezi, nawe unajua nami sijui, nawe nimjuzi wa yale yaliyofichikana. Ewe Mwenyezi Mungu iwapo jambo hili kutokana na ujuzi wako (utalitaja jambo lako) lina kheri na mimi katika dini yangu na maisha yangu na mwisho wa jambo langu (karibu na mbali ) basi nakuomba uniwezeshe nilipate, na unifanyie wepesi, kisha unibariki, na iwapo unajua kwamba jambo hili ni shari kangu katika dini yangu namaisha yangu na mwisho wa jambo langu (karibu na mbali) basi liepushe na mimi naminiepushe nalo, na nipangie jambo jengine lenye kheri nami popote lilipo, kisha niridhishe kwalo”