Monday 21 July 2014

Dua za Mtume Muhammad s.a.w


Du’aa katika Sunnah ziko nyingi sana. Aghlabu ya du’aa za Mtume (صلى الله عليه وسلم) zilikuwa za mukhtasari wa maneno kwa maana kauli zake fupi lakini zenye maana tele na hikma kama alivyosema mwenyewe katika usimulizi ufuatao:

عَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ (رضي الله عنه) أَنَّ رَسُولَ اللَّهِ (صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ) قَالَ: "فُضِّلْتُ عَلَى الأَنْبِيَاءِ بِسِتٍّ: أُعْطِيتُ جَوَامِعَ الْكَلِمِ, وَنُصِرْتُ بِالرُّعْبِ, وَأُحِلَّتْ لِيَ الْغَنَائِمُ, وَجُعِلَتْ لِيَ الأَرْضُ طَهُورًا وَمَسْجِدًا, وَأُرْسِلْتُ إِلَى الْخَلْقِ كَافَّةً, وَخُتِمَ بِيَ النَّبِيُّونَ

Imepokewa kutoka kwa Abu Huraryah (رضي الله عنه) kwamba Mtume (صلى الله عليه وسلم) amesema: ((Nimefadhilishwa juu ya Manabii kwa mambo sita; nimepewa ‘Jawaami’al-Kalimi’[1] na nimenusuriwa kwa [kutiwa] hofu [katika nyoyo za maadui] na nimehalalishiwa ghanima[2] na nimefanyiwa ardhi kuwa kitoharishi na masjid [mahali pa kuswali], na nimetumwa kwa viumbe wote, na Manabii wamekhitimishwa kwangu))[3]

Tunazigawanya Du’aa hizo katika maudhui mbali mbali na kutokana na hali zinazomkabili Muislamu:

-Du’aa Alizokuwa Akiomba Sana Mtume (صلى الله عليه وسلم )

Kuomba kheri za dunia na Akhera

رَبَّنَا آتِنَا فِي الدُّنْيَا حَسَنَةً وَفِي الأَخِرَةِ حَسَنَةً وَقِنَا عَذَابَ النَّارِ

Rabbaana aatinaa fid-dduniya hasanatan wafil Aakhirati hasanatan wa qinaa adhaaban-naari[4]

Mola wetu, tupe katika dunia mema na katika Akhera mema na Tukinge adhabu ya Moto[5]

Kuthibitika Katika Dini Na Utiifu

‏ يَا مُقَلِّبَ الْقُلُوبِ ثَبِّتْ قَلْبِي عَلَى دِينِك

Yaa muqallibal quluwbi, thabbit qalbiy ‘alaa Diynika

Ee Mwenye kupindua nyoyo, Thibitisha moyo wangu katika Dini Yako[6]

اللَّهُمَّ مُصَرِّفَ الْقُلُوبِ صَرِّفْ قُلُوبَنَا عَلَى طَاعَتِكَ

Allaahumma Muswarrifal quluwbi, swarrif quluwbanaa ‘alaa twaa’atika

Ee Allaah, Mwenye kugeuza nyoyo, zigeuzi nyoyo zetu katika utii Wako[7]

-Du’aa Za Maombi Ya Ujumla

‏ اللَّهُمَّ إِني أسْأَلُكَ مِنْ الْخَيْرِ كُلِّهِ عَاجِلِهِ وَآجِلِهِ مَا عَلِمْتُ مِنْهُ وَمَا لَمْ أعْلَمْ، وَأعُوذُ بِكَ مِنَ الشَّرِّ كُلِّهِ عَاجِلِهِ وَآجِلِهِ مَا عَلِمْتُ مِنْهُ وَمَا لَمْ ‏‏ أعْلَمْ، اللَّهُمَّ إِنِّي أسْأَلُكَ مِنْ خَيْرِ مَا سَألَكَ عَبْدُكَ وَنَبِيُّكَ، وَأعُوذُ بِكَ مِنْ شَرِّ مَا استعَاذَ بِكَ مَنْهُ عَبْدُكَ وَنَبِيُّكَ، اللَّهُمَّ إنِّي أسْأَلُكَ الْجَنَّةَ وَمَا قَرَّبَ إلَيْهَا مِنْ قَوْلٍ أوْ عَمَلٍ وَأعُوذُ بِكَ مِنْ النَّارِ وَمَا قَرَّبَ إِلَيْهَا مِنْ قَوْلٍ أوْ عَمَلٍ، وَأسْأَلُكَ أنْ تَجْعَلَ كُلَّ قَضَاءٍ قَضَيْتَهُ لِي خَيْرًا

Allaahumma inniy as-aluka minal-khayri kullihi ‘aajilihi wa aajilihi, maa ‘alimtu minhu wamaa lam a’lam. Wa a’uwdhu Bika minash-sharri kullihi ‘aajilihi wa aajilihi maa ‘alimtu minhu wamaa lam a’lam. Allaahumma inniy as-aluka min khayri maa saalaka ‘Abduka wa Nabiyyuka, wa a’uwdhu Bika min sharri masta’aadha Bika minhu ‘Abduka wa Nabiyyuka. Allaahumma inniy as-alukal-Jannata wamaa qarraba ilayhaa min qawlin aw ‘amal, wa a’uwdhu Bika minan-nnaari wamaa qarraba ilayhaa min qawlin aw ‘amal, wa as-aluka antaj-’ala kulla qadhwaai qadhwaytahu liy khayraa

Ee Allaah, hakika mimi nakuomba kheri zote zilizokaribu na mbali nizijuazo na nisizozijua. Najikinga Kwako shari zote za karibu na za mbali nizijuazo na nisizozijua. Ee Allaah, hakika nakuomba kheri alizokuomba mja Wako na Nabii Wako, na najikinga Kwako shari alizojikinga nazo mja Wako na Nabii wako. Ee Allaah, hakiki mimi nakuomba Pepo na yanayokaribisha kwayo katika kauli au amali, na najikinga Kwako Moto na yanayokaribisha kwayo katika kauli au amali, na nakuomba Ujaalie kila majaaliwa yangu [uliyonikidhia] yawe kheri[8]

‏ اللَّهُمَّ إِنِّي أسْألُكَ الْهُدَى وَالتُّقَى وَالْعَفَافَ وَالْغِنَى

Allaahumma inniy as-alukal-hudaa wat -ttuqaa wal ‘afaafa wal ghinaa

Ee Allaah hakika mimi nakuomba uongofu na ucha-Mungu na kujichunga[9] na kutosheka[10]

Kuomba Hidaaya:

اللَّهُمَّ اهْدِنِي وَسَدِّدْنِي, اللَّهُمَّ إِنِّي أَسْأَلُكَ الْهُدَى وَالسَّدَادَ

Allaahumma-hdiniy wasaddid-niy, Allaahumma inniy as-alukal-hudaa was-ssadaad

Ee Allaah, niongoe na nionyoshe sawasawa. Ee Allaah hakika mimi nakuomba hidaaya na unyofu[11]

Kuomba hesabu ya sahali Aakhirah Na Kuwa pamoja na Mtume (صلى الله عليه وسلم ) Peponi.

اللَّهُمَّ حَاسِبْنِي حِسَابًا يَسِيرًا

Allaahumma haasibniy hisaaban -yasiyraa

Ee Allaah nihesabie hisabu iliyo sahali[12]

اللَّهُمَّ إِنِّي أَسْأَلُكَ إِيمَانًا لاَ يَرْتَدُّ, وَنَعِيمًا لاَ يَنْفَدُ, وَمُرَافَقَةَ النَّبِيِّ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ فِي أَعْلَى غُرَفِ الْجَنَّةِ جَنَّاتِ الْخُلْدِ

Allaahumma inniy as-aluka iymaanan laa yartaddu, wa na’iyman laa yanfaddu, wa muraafqatan-Nabiyyi Swalla-Allaahu ‘alayhi wa sallam fiy a’-laa ghurafil-Jannah, Jannaatil-khuldi

Ee Allaah, hakika nakuomba imani isiyoritadi [isiyobadilika], na neema zisizoisha na kuambatana na Nabii Swalla-Allaahu ‘alayhi wa sallam katika vyumba vya ghorofa za juu kabisa Peponi, Pepo za kudumu milele[13]

-Kuomba Wingi Wa Iymaan, Taqwa Na Hifadhi

اللَّهُمَّ أَعِنِّي عَلَى ذِكْرِكَ وَشُكْرِكَ وَحُسْنِ عِبَادَتِكَ

Allaahumma a’inniy ‘alaa dhikrika, wa shukrika wa husni ‘ibaadatika

Ee Allaah nisaidie juu ya utajo Wako [kukudhukuru], na kukushukuru na uzuri wa ‘ibaadah Zako[14]

‏‏اللَّهُمَّ اقْسِمْ لَنَا مِنْ خَشْيَتِكَ مَا يَحُولُ بَيْنَنَا وَبَيْنَ مَعَاصِيكَ، وَمِنْ طَاعَتِكَ مَا ‏ ‏تُبَلِّغُنَا ‏بِهِ جَنَّتَكَ، وَمِنْ الْيَقِينِ مَا تُهَوِّنُ بِهِ عَلَيْنَا مُصِيبَاتِ الدُّنْيَا، وَمَتِّعْنَا بِأسْمَاعِنَا وَأبْصَارِنَا وَقُوَّتِنَا مَا أحْيَيْتَنَا, وَاجْعَلْهُ ‏الْوَارِثَ مِنَّا، وَاجْعَلْ ثَأرَنَا عَلَى مَنْ ظَلَمَنَا وَانْصُرْنَا عَلَى مَنْ عَادَانَا، ولا تَجْعَلْ مُصِيبَتَنَا فِي دِينِنَا، وَلا تَجْعَلْ الدُّنْيَا أكْبَرَ هَمِّنَا وَلا مَبْلَغَ عِلْمِنَا، وَلا تُسَلِّطْ عَلَيْنَا مَنْ لا يَرْحَمُنَا

Allaahumma-qsim-lanaa min khash-yatika maa yahuwlu baynanaa wa bayna ma’swiyk, wamin twaa’atika maa tuballighunaa bihi Jannatak, wa minal-yaqiyni maa tuhawwinu bihi ‘alaynaa muswiybaatid-duniya, wa matti’-naa biasmaa’inaa wa abswaarinaa wa quwwaatinaa maa ahyaytanaa waj-’alhul-waaritha minnaa waj-’al thaaranaa ‘alaa man dhwalamanaa wanswurnaa ‘alaa man ‘aadaana, walaa taj-’al muswiybatanaa fiy diyninaa, walaa taj-’alidduniya akbara hamminaa walaa mablagha ‘ilminaa, walaa tusallitw ‘alaynaa man-llaa yarhamunaa

Ee Allaah tugawanyie sisi hofu Yako itakayotenganisha baina yetu na baina maasi Yako, na utiifu utakaotufikisha katika Pepo Yako, na yaqini itakayotusahilishia misiba ya dunia, na tustareheshe kwa masikio yetu, na macho yetu, na nguvu zetu madamu Utatuweka hai, na yajaalie yawe ni urithi wetu na Jaalia iwe lipizo kwa anayetudhulumu, na tunusuru dhidi ya anayetufanyia uadui, na wala Usitufanyie msiba wetu ni Dini yetu, wala Usifanye dunia kuwa ndio hima yetu kubwa kabisa, na wala upeo wa elimu yetu, wala Usitusaliti kwa asiyetuhurumia[15]

1 comment:

  1. Shukran.Allah akulipeni kheri duniani na pepo akhera.

    ReplyDelete