Saturday, 26 September 2015
Monday, 7 September 2015
Adhkaar za Jioni
Sema: Yeye Mwenyezi Mungu ni wa pekee.
Mwenyezi Mungu Mkusudiwa.
Hakuzaa wala hakuzaliwa.
Wala hana anaye fanana naye hata mmoja.
بسم الله الرحمن الرحيم
Kwa Jina La Mwenyezi Mungu Mwingi Wa Rehema Mwenye Kurehemu
Sema: Najikinga kwa Mola Mlezi wa mapambazuko,
Na shari ya alivyo viumba,
Na shari ya giza la usiku liingiapo,
Na shari ya wanao pulizia mafundoni,
Na shari ya hasidi anapo husudu.
بسم الله الرحمن الرحيم
Kwa Jina La Mwenyezi Mungu Mwingi Wa Rehema Mwenye Kurehemu
Mfalme wa wanaadamu,
Mungu wa wanaadamu,
Na shari ya wasiwasi wa Shetani, Khannas,
Anaye tia wasiwasi katika vifua vya watu,
Kutokana na majini na wanaadamu.
ya moto na adhabu ya kaburi”
ajili yako tuko hai na kwa ajili yako tutakufa na ni kwako tu marejeo.
nakiri kwa madhambi yangu, basi nakuomba unisamehe kwani hasamehe madhambi ila Wewe”
arshi yako na malaika wako, na viumbe vyako vyote kwamba Wewe ndiye Mwenyezi Mungu hapana apasae kuabudiwa kwa haki ila Wewe, hali ya kuwa peke yako huna mshirika, na kwamba Muhammad ni mja wako na ni Mtume wako”
(Utasema hivi mara nne)
Atakaye yasema haya asubuhi au jioni mara nne Mwenyezi Mungu سبحانه وتعالى atamuepusha na moto.
اللّهُـمَّ إِنّـي أَعـوذُبِكَ مِنَ الْكُـفر ، وَالفَـقْر ، وَأَعـوذُبِكَ مِنْ عَذابِ القَـبْر ، لا إلهَ إلاّ أَنْـتَ
(mara saba)
(mara tatu )
(mara tatu)
(mara mia moja)
(mara kumi, au mara moja ukisikia uvivu)
(mara mia kwa siku )
(mara tatu)
Saturday, 18 July 2015
Sita Za Shawwaal Na Swawm Nyinginezo Baada Ya Ramadhan
Muhammad Baawazir
Ndugu Waislam, baada ya kuuaga mwezi mtukufu wa Ramadhwaan, ambao umejaa fadhila nyingi na kheri zisizopatikana katika miezi kumi na moja iliyobaki, kuna umuhimu mkubwa wa kuendeleza zoezi hili la Funga baada ya mwezi huu mtukufu hususan, na kwa mwaka mzima kwa ujumla In shaa Allaah.
Swawm kwa ujumla na Swawm za Sunnah haswa ni jambo kubwa sana la ki-'Ibaadah. Na ni bora sana ieleweke ndugu zangu, kuwa Swawm si 'Ibaadah ifanyikayo katika mwezi wa Ramadhwaan pekee, bali ni jambo ambalo linalofanyika mwaka mzima katika nyakati mbalimbali kama tutakavyoona katika makala haya.
Kama ilivyo katika ‘Ibaadah ya Swalah, kuna Swalah za Sunnah au Rawaatib au Nawaafil, ambazo ndizo zitakazokuwa viraka siku ya Qiyaamah wakati zile Swalah za Fardh zitakapopelea katika Mizani. Nazo Swawm za kujitolea au za Sunnah, ndizo zitakazomuongezea mja thawabu na ujira pamoja na ile Swawm yake ya Fardh ambayo ni Ramadhwaan.
Hapa chini tutaziorodhesha Swawm za SUNNAH ambazo Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) kazipendekeza kwetu tuzitekeleze:
SWAWM YA SIKU SITA ZA MWEZI WA SHAWWAAL
Swawm hii inafuatia moja kwa moja baada ya mwezi wa Ramadhwaan na siku ya 'Iyd ul Fitr. Na Mtume(Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) anasema:
((من صام رمضان ثم أتبعه ستاً من شوال كان كصيام الدهر)) رواه مسلم و الترمذي و ابن ماجه, أبو داود وأحمد
((Atakayefunga mwezi wa Ramadhwaan, kisha akafuatia kwa kufunga siku sita za mwezi wa Shawwaal, basi atapata ujira wa aliyefunga mwaka mzima)).Imepokewa na ma-Imaam Muslim, At-Tirmidhiy, Ibn Maajah, Abu Daawuud na Ahmad.
'Ulamaa wanachambua sababu ya kulipwa mja ujira wa mwaka mzima kwa atakayefunga Ramadhwaan na siku sita hizo za Shawwaal, kwa kusema: Jambo zuri hulipwa ujira mara kumi, kwa hiyo mtu akifunga siku 30 za Ramadhwaan atapata ujira mara kumi; nazo zitakuwa 300, ukijumlisha na siku sita za Shawwaal ambazo zikilipwa mara kumi, huwa 60. Kwa hivyo 300 + 60 = 360, mtu atapata hesabu ya mwaka mzima.
Kwa mantiki hii, tunaona kuna umuhimu na ubora mkubwa wa kuifunga Swawm hii ndugu zangu.
SWAWM YA SIKU YA 'ARAFAH (Kwa wale wasio katika Hajj)
Hadiyth ifuatayo inaonyesha uzito na muhimu wa Swawm ya siku hiyo:
عنْ أَبي قتَادةَ رضِي اللَّه عَنْهُ ، قالَ:سئِل رسولُ اللَّهِ صَلّى اللهُ عَلَيْهِوسَلَّم: عَنْ صَوْمِ يوْمِ عَرَفَةَ؟ قال:يكفِّرُ السَّنَةَ المَاضِيةَ وَالبَاقِيَةَ رواه مسلمٌ
Imetoka kwa Abu Qataadah (Radhiya Allaahu 'anhu) kwamba aliulizwa Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) kuhusu Swawm ya 'Arafah akasema ((Inafuta madhambi ya mwaka uliopita na mwaka uliopo)) [Imepokewa na Muslim].
SWAWM YA SIKU TATU KATIKA KILA MWEZI 'AYAAMUL-BIYDHW'
Imesimuliwa na Abu Hurayrah (Radhiya Allaahu 'anhu) kwamba Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alisema:
((من صام ثلاثة أيام من كل شهر فذلك صوم الدهر فأنزل الله عز وجل تصديق ذلك في كتابه {من جاء بالحسنة فله عشر أمثالها} فاليوم بعشرة أيام)) رواه الترمذي قال الشيخ الألباني : صحيح
((Yeyote atakayefunga kila mwezi siku tatu,ni sawa amefunga mwaka mzima, kisha Allaah Akashusha Aayah ithibitishayo maneno ya Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) isemayo: {{Atakayetenda jambo zuri basi malipo yake ni mara kumi mfano wake}}. Siku moja kwa malipo ya siku kumi))[Imepokewa na At-Tirmidhiy na kasema Shaykh Al-Albaaniy kuwa ni Sahihi].
Ukiitazama Hadiyth hii, utakuta makusudio yaliyotajwa kuwa malipo ya Funga hiyo ya siku tatu za kila mwezi, ni sawa na ya mwaka mzima, ni kuwa, ukipiga hesabu ya hizo siku tatu za kila mwezi, mara miezi kumi na mbili ya mwaka, ni sawa na siku 36. Na siku hizo 36 mara 10 ambazo ndizo malipo ya kila siku kwa mara kumi, basi utapata jumla ya siku 360 ambazo ni takriban idadi ya mwaka mzima wa Kiislam. Fadhila zilizoje na Ujira mrahisi kiasi gani wa kuuchuma ndugu watukufu.
Masiku haya matatu, Masiku Meupe ''Ayaamul-Biydhw'', yametajwa katika Hadiyth ifuatayo:
Abu Dharr Al-Ghifaariy anasimulia kuwa Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alimwambia:
((يا أبا ذر إذا صمت من الشهر ثلاثة أيام فصم ثلاث عشرة وأربع عشرة وخمس عشرة)) رواهالترمذي. قال الشيخ الألباني: حسن صحيح
((Ee Abu Dharr! Endapo utafunga siku tatu za kila mwezi, basi funga siku ya 13, ya 14, na ya 15)) (Hizi huitwa 'Ayaam ul Biydhw' Masiku Meupe kwa sababu katika masiku hayo kunakuwa kweupe zaidi kwa mwanga wa mbalamwezi). [Imepokewa na At-Tirmidhiy na kasema Shaykh Al-Albaaniy kuwa ni Sahihi].
SWAWM YA JUMATATU NA ALKHAMIYS
عن أبي هريرة رضي الله عنه قال: كان رسول الله صلى الله عليه وسلم يصوم الإثنين والخميس وعندما سئل قال: (( تُعْرَضُ الْأَعْمَالُ يَوْمَ الِاثْنَيْنِ وَالْخَمِيسِ فَأُحِبُّ أَنْ يُعْرَضَ عَمَلِي وَأَنَا صَائِمٌ })) رواه الترمذي وقال حديث حسن
Abu Hurayrah (Radhiya Allaahu 'anhu) anasimulia kuwa Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alikuwa akifunga Jumatatu na Alkhamiys. Alipoulizwa sababu ya Swawm katika siku hizo, akajibu: ((Matendo ya Wanaadam huwekwa mbele ya Allaah kila siku ya Jumatatu na Alkhamiys, nami napenda matendo yangu yawekwe mbele ya Allaah nikiwa nimefunga)). [Imepokewa At-Tirmidhiy na kasema ni Hadiyth Hasan].
SWAWM YA SIKU YA TAASU'AANA 'AASHURAA
Hizi ni Swawm za siku ya tisa na ya kumi ya mwezi wa Muharram (Mwezi wa kwanza katika kalenda ya Kiislam). Hizi ni Swawm kwa kumbukumbu na kumshukuru Allaah (Subhaanahu Wa Ta'aalaa) kwa kumuokoa Nabii Muwsaa (‘Alayhis-Salaam) pamoja na watu wake, kutokana na balaa la Fir’awn na jeshi lake.
SWAWM NYINGINEZO
Swawm katika mwezi wa Muharram zina fadhila nyingi kama Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alivyomwelezea Abu Hurayrah. pia Swawm katika mwezi wa Sha'abaan, ambapo mama wa waumini 'Aaishah (Radhiya Allaahu 'anha) anasema kuwa Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alikuwa akikithirisha sana kufunga.
NIYYAH
Swawm kama amali zingine, ni lazima kuwepo na Niyyah ndani yake. Niyyah pahala pake ni moyoni, na si kutamka, ukishapitisha uamuzi wa kufunga, basi hiyo yatosha na si kukariri maneno au kutafuta mtu akufundishe namna ya kuitamka Niyyah kwa Kiarabu au vinginevyo kama wanavyodhania baadhi ya watu.
Wa Allaahu A’lam
Monday, 6 October 2014
Faida za asali
Asali ni chakula kitamu. kinachotengenezwa na nyuki kwa kukusanya nectar kutoka kwenye mauwa.Asali inaweza kaa miaka mingi sana bila kuharibika,asilimi kubwa ya wadudu waaribifu hawawezi kukua ndani ya asali kwani inakiasi kidogo sana cha maji yaani 0.6(WATER ACTIVITY).Tone lolote la maji au mate linapoingia kwenye asali huongeza uwezakano wa kuaribika kwa asali hiyo na kufupisha maisha ya asali.Kwa ufupi naweza sema maji ni adui mkubwa wa asali.
Aina na ubora wa asali hutofautiana kutokana na aina ya nyuki walioitengeneza asali hiyo pomoja na aina ya maua ambayo nyuki wamenyonya nectar yake,rangi za asali pia hutofautiana kwa misingi hiyo hiyo.
Aina mbalimbali za asali.
Apa nchini Tanzania kuna aina kuu mbili za asali,asali ya nyuki wakubwa na asali ya nyuki wadogo.Asali ya nyuki wakubwa hupatikana kwa wingi zaidi kuliko ya nyuko wadogo,Lakini asali ya nyuki wadogo huuzwa bei ghali zaidi ya asali ya nyuki wakubwa kwani ilithibitika kwamba asali ya nyuki wadogo inatengenezwa kutoka kwenye nectar ya mauwa ambayo miti yake inausali wa dawa.Miti hiyo ni kama Mlonge,mwarubaini,rosella na mingine mingi.
Asali ni chakula kinachotumika kwa mambo mengi sana,unaweza itumia badala ya sukari kwenye vinywaji,kuipakaa kwenye mkate,na kuitumia kama kionjo kwenye vyakula mapishi mbali mbali,pia hutumika kutengeneza urembo wa aina mbalimbali kama mafuta na sabuni na vingine vingi,liakini zaidi ya yote asali hutumika kama dawa.
Ni vyema kujua kwamba asali mbichi(ambayo haijapitishwa kwenye moto)ni nzuri kuliko ile iliyopitishwa kwenye moto,Kwani pale asali inapopitishwa kwenye moto baadhi ya enzymes hufa na virutubisho vingine hupotea.Mara nyingi asali hupitishwa kwenye moto ili kuiyeyusha hasa pale inapotakiwa kuchujwa.
ASALI KAMA DAWA
Asali kama dawa inaweza kutibu matatizo mbalimbali,kumbuka tu tunaongelea asali ambayo haijachanganywa na kitu chochote.
For skin rashes, burns and abrasions.
Apply a small amount of raw honey lightly over the affected area; may cover with a dressing or a dusting of cornstarch to reduce any stickiness.
The ultimate moisturizer.
Smooth a small amount of raw honey lightly over the skin; easily remove later with splashes of cold water or comfortable warm water. Leaves skin baby soft.
As a bath and antibacterial soap.
Wash with raw honey straight from the jar and enjoy sparkling clean skin. Facial blemishes and acne caused by cosmetics or allergies will clear up quickly using a nightly treatment of RRH. A small amount needed.
For hair and scalp treatment.
Apply Really Raw Honey (with or without olive oil) to dry or damp hair about one half hour before washing–you’ll be amazed at your “crowning glory”.
For dental care and mouth sores.
Cleans teeth, mouth and dentures and stops bleeding gums. Canker sores, blisters and mouth ulcers respond to application of raw honey.
An astounding natural preservative.
Unprocessed honey found in ancient tombs was determined to be edible and was even used to preserve bodies. Keeps foods fresh and moist longer and retards spoilage.
For healing ulcers and burns
Also many years ago, a study by Robert Bloomfield, published in the Journal of the American Medical Association, reports “Applied every 2 to 3 days under a dry dressing, honey promotes healing of ulcers and burns better than any other local application. It can also be applied to other surface wounds, including cuts and abrasions…”
Honey has anti-cancer properties.
Recent studies by Gribel and Pashinskii indicated that honey possessed moderate antitumor and pronounced anti-metastatic effects in five different strains of rat and mouse tumors. Furthermore, honey potentiated the antitumor activity of chemotherapeutic drugs such as 5-fluorouracil and cyclophosphamide. — Gribel, N.V., and Pashinskii, V.G. Antitumor properties of honey. Vopr. Onkol., 36:704-709, 1990.
C.V. Rao at the American Health Foundation in Valhalla, New York found caffeic acids in propolis are inhibitors of colon cancers in animals. Other research shows hive products have the ability to prevent and halt the spread of malignant diseases. Earlier research by M.T. Huang also published in Cancer Research found caffeic acids effective in inhibiting skin cancer tumors in mice.
Ushauri
Ni vyema ukawa na asali nyumbani kwa ajili ya matumizimbalimbali.Kwa matumizi ya asali kama dawa,nashauri asali mbichi ya nyuki wadogo.Najua ni ngumu kujua kama asali mbichi au imepitishwa kwenye moto,Hivyo nashauri utumie asali ya FANO 2010.
Asali za Fano 2010(Golden Lulu)
Asali za FANO 2010 zinapatika Thanks God supermarket,eneo la sinza madukani.nashauri asali hii kwani ndio asali ninayotumia na ninakuhakikishia kuwa ni asali mbichi,na zaidi ya yote niliwai tembelea workshop ya FANO 2010 na kuona jinsi wanavyochuja asali ,Ndio maana ninanguvu ya kushauri utumie asali hio
ONYO
Asali si nzuri kwa watoto wadogo wenye umri wa kati ya siku moja hadi miaka miwili,kwani wakati mwingine asali huwa na endospores wa bacterium clostridium botulinum.Endospores hizo zinaweza kubadilika kua aina ya bacteria wanatoa sumu.Bacteria hawa hushambulia utumbo mwembamba wa mtoto ambao haujakomaa na hivyo huweza msababishia mtoto kuumwa na hata kifo.
Akina mama msikose chupa ya asali jikoni,kwani ajali za kuungua ni kawaida jikoni na asali ni dawa nzuri sana,Ukiungua kitu cha kwanza kabisa pakaa asali nyingi kwenye eneo uliloungua..
Nimalizie kwa kusema.Asali ikichanganywa na dawa zingine za asili au viungo fulani pia huwa dawa ya magojwa mengi zaidi.Naamini makala hii imekufumbua macho na kukufanya uithamini asali
Friday, 26 September 2014
Uzushi Wa Unoadaiwa Ni Fadhila Za Siku Kumi Za Dhul-Hijjah
SWALI:
Nimepokea e-mail iliyotumwa yenye kutaja fadhila za siku kumi kila siku kuwa ni jambo fulani limetokea na kadha kama inavyoeleza hapa chini. Je hii ipo dalili au ni katika uzushi?
Siku Kumi Bora
Mwenye-ezi mungu subhanahu wataala ameapa kwa masiku bora katika quraan takatifu sura 89 aya 1-2 isemayo : Mtume Muhammad ( S.A.W.) ametusimulia vilivyotendeka na umuhimu wa siku hizi kumi bora za mfungo tatu (DhulHijja); Rasula-llah atueleza sisi ummati wake kuwa, mwenye kufunga siku hizo hupata fadhla kubwa mno,kwani kila siku ina fadhila na kheri zake:
SIKU YA KWANZA YA MFUNGO TATU Mtume (S.A.W.) asema kuwa - "Ni siku ambayo Mwenye-ezi Mungu alimsamehe Nabii Adam (A.S.) kwa makosa yake".Mwenye kufunga siku hiyo, Mwenye-ezi Mungu humsamehe madhambi yake.
SIKU YA PILI YA MFUNGO TATUMtume(S.A.W.)asema kuwa:-"Ni siku ambayo Mwenye-ezi Mungu alikubali maombi ya Nabii Yunus (A.S.) ya kumtoa katika matumbo ya samaki".Mwenye kufunga siku hiyo, ni kama aliyefanya ibada ya mwaka mzima pasi na kufanya makosa.
SIKU YA TATA MFUNGO TATU Mtume(S.A.W.)asema kuwa:-"Ni siku ambayo Mwenye-ezi Mungu aliitikia Dua ya Nabii Zakariya (A.S.) yakumpata mtoto".Mwenye kufunga siku hiyo, Mwenye-ezi Mungu huitikia dua yake.
SIKU YA NNE YA MFUNGO TATUMtume(S.A.W.)asema kuwa:-"Ni siku ambayo alizaliwa Nabii Issa(A.S.)".Mwenye kufunga siku hiyo, Mwenye-ezi Mungu humuondolea matatizo na umasikini.
SIKU YA TANO MFUNGO TATU Mtume(S.A.W.)asema kuwa:-"Ni siku alizaliwa Nabii Musa(A.S) "Mwenye kufunga siku hiyo, Mwenye-ezi Mungu humtakasa na unafiki na humuondolea adhabu za kabori.
SIKU YA SITA MFUNGO TATU Mtume (S.A.W.)asema kuwa:-Ni siku ambayo Mwenye-ezi Mungu alimfungulia Mtume wake (Muhammed (S.A.W.) )kheri".Mwenye kufunga siko hiyo, Mwenye-ezi Mungu humuangalia kwa jicho la huruma wala hapati adhabu siku ya kiyama.
SIKU YA SABA YA MFUNGO TATU Mtume asema kuwa:-"Ni siku ambayo Milango ya Jahannam(Moto)hufungwa na hayafunguliwi hadi masiku kumi yatimie".Mwenye kufunga Mwenye-ezi Mungu humfungia Milango thelathini ya mambo mazito na humfungulia Milango thelathini ya mambo mepesi.
SIKU YA NANE YA MFUNGO TATUMtume(S.A.W.)asema kuwa:-"Ni siku iitwayo Tar-wiya".Mwenye kufunga hupewa malipo ambayo hakuna ayajuwaye isipokuwa Allah SWT.
SIKU YA TISA YA MFUNGO TATUMtume(S.A.W.)asema kuwa:-"Ni siku iitwayo Arafat".Mwenye kufunga siku hiyo, hufutiwa makosa ya mwaka uliopita, na utakao kuja.
SIKU YA KUMI YA MFUNGO TATU:- Mtume(S.A.W.)asema kuwa:-"Ni siku ya kuchinja Mnyama(itakuwa Iddi Kubwa), tone la kwanza la damu litakapo tona Mwenye-ezi Mungu humsamehe dhambi zake na za jamaa zake. Na mwenye kumpa chakula Masikini au akatowa sadaka siku hiyo, Myenye-ezi Mungu atamfufua siku ya Kiyama kwa amali na mizani ya uzito, thawabu zake zitashinda uzito wa Mlima Uhud".
PLEASE DO NOT FORGET TO ENLIGHTEN OTHER MUSLIMS BY FORWARDING THIS MAIL
JIBU Kutoka alhidayah
Sifa zote njema Anastahiki Allaah Aliyetukuka Mola Mlezi wa walimwengu wote, Swalah na salamu zimshukie kipenzi chetu Mtume Muhammad (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wasallam) na Swahaba zake (Radhiya Allaahu 'anhum) na watangu wema mpaka Siku ya Mwisho
Tunasikitika kwamba siku hizi fitna za kusambaza uzushi zimezidi kutokana na wepesi wa mawasiliano kupitia barua pepe (e-mail), simu za mkononi n.k. Jambo linaloshangaza ni kwamba Hadiyth zilizo Sahihi zimejaa tele lakini hizo hazisambazwi kama zinavyosambazwa za uzushi. Ni dhahiri kwamba wanaofanya hivyo ima hawajui tofauti ya mafunzo sahihi na yale potofu ima kwa uchache wa elimu, au kwa pupa tu za kutafuta thawabu kwa njia za mkato ndiko kunakowasababisha wao kueneza haya mambo yasiyo na dalili wala asili. Lakini wanaghafilika ndugu hao kutambua madhara yanayopatikana kutokana na hayo wanayoyaeneza kila mara.
Moja ya madhara makuu ni kupoteza mafundisho sahihi ya Dini yetu, na kueneza ya uongo na hivyo kutawala upotofu katika jamii ya Kiislam, Kwani kama wanavyosema wema waliotangulia, kuwa, bid’ah inavyoenea, ndio Sunnah hupotea.
Tumepekuwa vitabu mbalimbali vya Hadiyth vikubwa na mashuhuri na hakuna hata sehemu moja tuliyokuta kuna Hadiyth inayotaja Fadhila za masiku kumi ya Dhul-Hijjah kwa mtindo huo na kwa maelezo hayo! Vilevile Maulamaa waliowahi kukumbana na maelezo hayo, wamesema kuwa ni ‘Mawdhuw’ – yaani ya kutungwa na si ya kweli.
Kuna hatari vilevile ya watu kutumbukia katika maonyo na makemeo aliyoyatoa Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam):
((من كذب علي متعمدا فليتبوأ مقعده من النار)) متفق عليه
((Atakayeniongopea makusudi basi ajitayarishie makazi yake motoni)) [Al-Bukhaariy Na Muslim]
Ukiwa umeeneza mambo hayo na hali unajua kuwa si sahihi, basi tambua kuwa ushaingia katika walioelezwa ndani ya Hadiyth hiyo.
Na ikiwa una mazoea ya kueneza au kutuma kila unachopata ukidhani utapata thawabu kwa kufanya hivyo na hali huna uhakika nacho, au huna elimu ya jambo hilo kama ni sahihi au la, basi utakuwa pia una majukumu kwa kuwa Uislam umesisitiza sana elimu na umuhimu wa kuitafuta; hivyo kwanini ubakie katika ujinga na kutokufahamu unayotuma? Pia ikiwa hujui, ushaelezwa na Allaah (Subhaanahu wa Ta’ala) uulize wenye elimu na upambuzi, je, ulijaribu kufanya hayo kabla hujasambaza mambo hayo ya kutunga yenye kupotezea Waislam muda, juhudi, na hata ‘amali zao kwa kufanya yasiyo sahihi na yasiyo katika mafundisho ya Dini?
Na madhara mengine ni kwamba dhambi za mwenye kueneza uzushi huzidi kila uzushi unapozidi kusambaa na mwenye kuanza kueneza uzushi hubeba dhambi za kila mtu anayepokea na kujifunza uzushi huo:
عن أبي هريرة رضي الله عنه عن النبي صلى الله عليه وسلم أنه قال : ( من دعا إلى هدى كان له من الأجر من أجور من تبعه لا ينقص من أجورهم شيئاً ومن دعا إلى ضلالة كان عليه من الإثم مثل آثام من تبعه لا ينقص ذلك من آثامهم شيئاً) رواه مسلم
Kutoka kwa Abu Hurayrah (Radhiya Allaahu ‘anhu) kwamba Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) kasema: ((Atakayelingania kwenye uongofu atapata thawabu (ujira) wa yule atakayemfuata bila ya kupungukiwa chochote katika thawabu zao. Na atakayeelekeza katika upotofu atapata dhambi mfano wa dhambi za yule atakayefuata bila ya kupungukiwa chochote katika dhambi zao)) [Muslim]
Tumefanya utafiti mkubwa kutafuta kauli kama hizo kuhakikisha kama ipo kauli ya Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) inayotaja fadhila za siku hizo kama zilivyotajwa humu lakini hatukupata. Mojawapo ya matokeo ya utafiti ni kupata fatwa kutoka kwa Maulamaa kutoka Markaz ya Fataawa walioulizwa kuhusu ujumbe huo nao pia wamehakikisha kuwa ni uzushi usio na dalili yoyote [Markaz al-Fataawa 24 Dhul-Hijjah 1424/16-02-2004].
Tunawanasihi ndugu zetu Waislamu wasome mada muhimu katika kiungo kifuatacho ili watambue hatari ya kueneza uzushi:
Hatari Ya Kueneza Hadiyth Dhaifu Na Visa Vya Uongo
Vilevile mtu anatakiwa asome mada hii hapa chini yenye kuhusu uzushi wenye kufanana na huo:
Uzushi Unaodaiwa Kuhusu Mambo Yaliyotokea Siku Ya Ashuraa Tarehe 10
Jambo jingine muhimu tunalopenda kuwatanabahisha ni kuhusu jinsi hayo majina ya miezi ya Kiislam yanavyoitwa au yalivyozoeleka kuitwa kama tulivyoona kwenye huo ujumbe wa kutungwa kwa jina la mfungo mosi, mfungo pili, mfungo tatu n.k., hakika ni majina yaliyozoeleka lakini si sahihi kwani yanapoteza ufahamu wa majina sahihi na mpangilio wa hiyo miezi ya Kiislam.
Miezi ya Kiislam hujulikana mwezi wa kwanza kama ni Muharram lakini wao huo mwezi wa kwanza umeitwa ni mfungo nne, na mwezi wa Dhul-Hijjah ambao ni mwezi wa kumi na mbili, wao wanauita mfungo tatu! Hivyo Waislam wengi hudhani kuwa huu mwezi wa 12 wa Dhul-Hijjah tulionao sasa kuwa ni mwezi wa 3 badala ya 12. Kutoka katika mpango uliowekwa na Uislam na kufuata mipango na taratibu za kimila na kitamaduni, kunasababisha mafunzo ya Dini kutofahamika kamwe, au kusahaulika kabisa. Leo hii, Waislamu wengi Waswahili hawajui miezi ya Kiislam kwa majina yake ingawa wengi wanaijua hiyo ‘mifungo’. Huo ni ukweli wenye kusikitisha. Na wengi huita kalenda na tarehe za Kiislam kuwa ni tarehe za Kiarabu badala ya Kiislam; ilihali kuna tofauti kubwa kati ya Uislamu na Uarabu. Miezi ya Kiislam ni hiyo tuliyozungumzia hapo juu na tutaweka chini kabisa mpangilio wake wa majina ya miezi yote ya mwaka mzima. Kalenda au tarehe za kiarabu ni tofauti na za Kiislam na mtu akitaka kujua atazame magazeti ya Kiarabu ataona tofauti. Hivyo, Waislam wajizoeshe kuita tarehe za Kiislam au miezi ya Kiislam na si ya Kiarabu, maana kuna Wakristo Waarabu nao hawafuati kalenda yetu ya Kiislam.
Miezi Ya Kiislam (Kila Muislam Ajitahidi Kuijua Na Kuihifadhi)
1- Muharram محرّم
2- Swafar صفر
3- Rabiy’u al-Awwal ربيع الأول
4- Rabiy’u ath-Thaaniy au Rabiy’u al-Aakhirربيع الآخر أو ربيع الثاني
5- Jumaada al-Uwlaa جمادى الأول
6- Jumaada ath-Thaaniy au Jumaada al-Aakhir جمادى الآخر أو جمادى الثاني
7- Rajab رجب
8- Sha’abaan شعبان
9- Ramadhaan رمضان
10- Shawwaal شوّال
11- Dhul-Qa’adah ذوالقعدة
12- Dhul-Hijjah ذوالحجة
Inasikitisha sana kuona Muislam
kahifadhi miezi yote ya kikafiri, lakini hawezi kutaja hata miezi sita ya Kiislam. Sana sana utakuta Muislam anajua ile miezi ya karibu na Ramadhaan kama Rajab, Sha’abaan na pia labda mwezi huu wa Dhul-Hijjah na wengine huujua Rabiy’ul al-Awwal kwa sababu ya kusherekea tu Mawlid na huenda asijue kuwa ni Rabiy’u al-Awwal, bali atakuwa anaujua kwa jina la kijamii ‘Mfungo sita’! Huu ndio msiba tulionao Waislam, inatubidi tuamke hivi sasa na tuzindukane na usingizi wa miaka na miaka. Na silaha pekee ya kuzindukana na hayo, ni ELIMU SAHIHI ya Dini.
Pia tunawaomba ndugu zetu kwamba wanapopata jambo lenye shaka kwanza wawe wanahakikisha kabla ya kutuma kwa wenzao kwani tutambue kuwa Muislamu inapomfikia kauli inayodaiwa kuwa ni ya Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) basi imeshakuwa ni waajib kwake kuhakikisha. Akipata dalili ya usahihi wake atume kwa wenziwe kama tunavyoamrishwa kufikisha kwa wengine japo Aayah moja na kuamrishana mema na kukatazana maovu. Lakini ikiwa hakupata dalili yake ni bora kuacha kutuma kuliko kuleta madhara ya uzushi na kuzidisha ufisadi katika dini na jamii kwa ujumla kwa kupoteza mafunzo sahihi na kueneza mafunzo ya uzushi.
Kidokezo Cha Kuweza Kutambua Hadiyth Zisizo Sahihi Au Ujumbe Wa Uongo:
Ndugu Muislam, ukitaka kugundua haraka ujumbe ulioupata kwenye barua pepe (e-mail) au ujumbe kwenye simu za mkono, kwanza kitakachokujulisha kuwa ujumbe huo una utata na sio sahihi, ni kuwa, mara nyingi maelezo yaliyomo ndani ya ujumbe huo zikiwemo zinazosemwa ni Hadiyth, utakuta hazitajwi zilipotolewa, kama ni Hadiyth utaona haisemwi nani kasimulia, nani kapokea, kitabu gani, hakuna hata Imaam wa Hadiyth (Muhaddith) aliyetajwa kwenye Hadiyth hiyo n.k. Hayo yote yanatosha kumtia mashaka mtu kuhusiana na alichokipokea. Hivyo, endapo utapokea ujumbe au Hadiyth ambayo imekuja tu na kudaiwa kasema Mtume, bila kutajwa zaidi ya hivyo… basi mrudishie aliyekutumia na muombe akueleze Hadiyth hiyo iko kwenye kitabu kipi, na nani kaisimulia na kama ni sahihi au dhaifu. Usiwe na pupa ya kueneza au kusambaza kwa wengine hadi kwanza upate uhakika 100%. Vilevile unaweza kutuandikia maswali@alhidaaya.comkuulizia masuala kama hayo na inshaAllaah tutakusaidia haraka katika masuala hayo.
Na Allaah Anajua zaidi
Monday, 8 September 2014
17 Rules of Islamic Dream Interpretations
Ibn Qutaybah ad-Dinawari رحمه الله says in his book about dream interpretations, “There is nothing in which people deal with from the different sciences that is more obscure, delicate, exalted, noble, difficult and problematic than dreams because they are a type of revelation and type of Prophethood.”
Narrated Anas bin Malik رضي الله عنهAllah’s Messenger صلى الله عليه و سلمsaid, “A good dream (that comes true) of a righteous man is one of forty-six parts of prophet hood.” [Sahih al-Bukhari]
Some scholars tried to give explanation to this ratio of 1:46. We have no way to find out that if their explanation is correct or not. Prophet hood of Prophet صلى الله عليه و سلم extended from 40 to 63 years meaning for 23 years. We know from Seerah that six months before becoming a Prophet, Messenger of Allah صلى الله عليه و سلمwas seeing dreams that would come out to be true on a very frequent basis so much so that he would see a dream one night and it would come to be true the next morning. So the ratio of 6 months to 23 years is 1:46.
1) There are 3 types of dreams: Imam at-Tirmidhi رحمه الله narrates from Muhammad Ibn Sirin رحمه الله who narrates from Abu Hurairah رضي الله تعالى عنه that Prophet صلى الله عليه وسلم said, “There are three types of dreams: 1) True Dreams 2) A dream in which a person is speaking to himself (i.e. whatever you were thinking about in the day time, you see at night) 3) A dream from shaytaan in which he wants to make you sad ”
In one hadith it is mentioned that one should stand up and pray and in another the he should not mention it to anyone.
Abu Salamah رضي الله عنه once said, “Sometimes I would see a dream that would be heavier on me than carrying a mountain. But since I heard this hadith I wouldn’t care about the bad dream I would see.”
Narrated Abu Sa‘id Al-Khudri رضي الله عنه: The Prophet صلى الله عليه و سلم said, “If anyone of you sees a dream that he likes, then it is from Allah, and he should thank Allah for it and narrate it to others; but if he sees something else, i.e., a dream that he dislikes, then it is from Satan, and he should seek refuge with Allah from its evil, and he should not mention it to anybody, for it will not harm him.” [Sahih Muslim]
Q1) A question arises, is every dream that a believer sees good?
A1) Al Muhallab رحمه الله says, “Most of the dreams of the righteous people are good dreams because sometimes a righteous person could see a dream that is meaningless but that is not very frequent because shaytaan’s control on them is very weak. And the opposite is true with other people because shaytaan has a stronger grasp over them. People are of the categories:
1) The Prophets: all of their dreams are truthful and but sometimes they need interpretation. The good dream is divided into 2 categories:
a) Direct dream: something one would see in a dream and the exact scene repeats itself in day-time when you are awake and this dream does not need interpretation.
b) A dream the comes in symbols and it needs to be interpreted.
2) The righteous: most of the time their dreams are truthful (most of them need to interpreted) and sometimes their dream are direct.
3) Rest of the people: most of their dreams are not true but some of them could be true.” [Fath al-Bari bi Sharh Sahih al-Bukhari]
2) Do not mention the dream for interpretation except to a scholar or a person who would advise you sincerely.
Prophet صلى الله عليه و سلم said, “You should not mention this dream to an envious person…”
There is also evidence for this in the Qur`an: (Remember) when Yûsuf (Joseph) saidto his father: “O my father! Verily, I saw (in a dream) eleven stars and the sun and the moon, I saw them prostrating themselves to me.” He (the father) said: “O my son! Relate not your vision to your brothers, lest they arrange a plot against you. Verily! Shaitân (Satan) is to man an open enemy! {Surat al-Yusuf, ayatyn 4-5}
3) Seeing Prophet صلى الله عليه و سلم:
Narrated Anas رضي الله عنه the Prophet صلى الله عليه و سلم said, “Whoever has seen me in a dream, then no doubt, he has seen me, for Satan cannot imitate my shape. [Sahih al-Bukhari]
Q2) There is an issue here, what if a person sees Prophet صلى الله عليه و سلم and he feels that it is him but his description in the dream if different than the one we know of from ahadith. So is the person in the dream Prophet صلى الله عليه و سلم?
A2) Az-Zuhri رحمه الله says that Ibn Sirin رحمه الله said, “If you see him according to his description.” An-Nawawi رحمه الله, however, has a contrary view and he says, “As long as you felt in your dream that the person you saw was Prophet صلى الله عليه و سلم then it is him even if he comes in a different form.” Ibn Taymiyyah رضي الله عنه supports the view of Ibn Sirin رحمه الله
4) A repetition of a dream is a sign of its truth. It does not matter if the same person sees the dream more than once or more than one person.
‘AbduLlah ibn ‘Umar رضي الله عنهما reported that some people were shown the Night of Qadr as being in the last seven days (of the month of Ramadan). The Prophet صلى الله عليه و سلم said, “I see that your dreams strengthen each other that Night of Qadr is in the last seven nights of Ramadhan so whoever searches for it, would search for it in the last seven days (of Ramadan).” [Sahih al-Bukhari]
Also the dream about Adhan when 2 Sahabah ضي الله عنهما saw the same dream.
5) Q3) When is the most expected time to see a righteous dream? At night or day time? Are all the times equal (whether seen at the beginning of the night or end of the day)?
A3) Ibn Sirin رحمه الله said, “Dreams of day time are equal to the dreams of night.” [Sahih Muslim]
6) Ibn Battal رحمه الله said, “Dreams are of two types: a clear evident dream like somebody would dream about himself giving dates to someone and during the day time he would give somebody dates. This type of dream doesn’t need any interpretation. Secondly, a dream that comes in symbols and this type you would understand its meaning unless you get it interpreted by a person who has knowledge and experience dream interpretation because sometimes the symbols are very delicate and sophisticated.”
Like the dream Prophet صلى الله عليه و سلم saw in which he was drinking milk from a vessel and when some of it was remaining, he gave it ‘Umar رضي الله عنه. Prophet صلى الله عليه و سلم interpreted it as knowledge. This means that Prophet صلى الله عليه و سلم absorbed the knowledge and he mentions that the milk was so much that it started flowing beneath his nails. So he had so much knowledge in him, that it started flowing from him.
7) Dreams can be about the past or the present or the future.
8) True dreams increase towards the end of times.
Ibn Sirin رحمه الله said,” I heard Abu Hurairah saying, ‘Prophet صلى الله عليه و سلم said, “When Time approaches, the dream of the believer rarely would lie.’” [Sahih al-Bukhari]
“When Time approaches…”is explained in two different opinions:
1)Al-Khattabi رحمه الله said, “The meaning of ‘When Time approaches…” is the time of night and the time of day. When the time of night approaches the length the time of day, then the dreams of the believer will be true. These are the two times when flowers open up and when fruits are ripe. The scholars of dream interpretation actually state that these are the two time when the dreams are most likely to be true.”
2)Al-Qurtubi رحمه الله says, “What is meant by this hadith, and Allah سبحانه و تعالى knows best, is the end of times and it is talking about the group of believers that will be with ‘Isa ibn Maryam عليه سلام after he kills dajjal.”
Ibn Abi Jamrah رحمه الله says,” The reason why the believer sees true dreams at the time is because the believer will be ghareeb (stranger) as was mentioned in the hadith, ‘Islam began as something strange and it will return to the way it began being strange so give glad tidings to the strangers so give glad tidings to the strangers.’”
Ibn Hajar al-‘Asqalani رحمه الله comments on all the opinions by saying, “Whenever the times are difficult for the believer, he will see dreams that are true frequently because he needs help. When the believer is alone, when the times are difficult, when you don’t find people supporting on truth, then Allah سبحانه و تعالى will inspire you to give you glad tidings through the good dreams you would see and this is to give the believers in those difficult and testing times gives the believers strength, it gives them confidence, it gives them hope so they would see a lot of dreams that would come true.”
For example the brothers who are doing Jihad feesabiliLlah see a lot of dreams that come out to be true because they are being tested by Allah سبحانه و تعالى thus He assists them.
9) Most of the times, if the dream is a glad tiding from Allah سبحانه و تعالى it would take a long for it to occur while if it is a warning it would occur swiftly.
For example Yusuf عليه سلام’s dream took a very long time for it to happen around 40 years. Some scholars say this is because Allah سبحانه و تعالى gives the believer glad tidings early on to give him confidence and hope, to inspire him in his life. While if it is a warning, you would see it and it would occur very soon so that it would be the reason of fear in your heart.
10) Dreams are glad tidings and warnings but can not be used as a source of Shari‘ah.
Ash-Shatbi رحمه الله says regarding this, “Benefit of the dream in giving the believer a glad tiding or warning not in legislation and judgement or rulings.”
11) If one sees a dream that is very long like a movie or someone is chasing you and it never ends then most likely that dream doesn’t mean anything. True dreams are short and concise.
12) The dream of a believer pleases him but it does not make him proud or over confident.
Ibn Muflih رضي الله عنه mentions in his book Adaab ash-Shar‘iyah, “Ibrahim al-Humaydi was righteous man and Imam Ahmad bin Hanbal visited him so Ibrahim told Imam Ahmad, ‘My mother has seen a dream for you where she saw this-and-that for you,’ and then he mentioned Jannah. Imam Ahmad said, ‘My brother, Sahl ibn Salamah, people used to see dreams for him similar to what you mentioned and in the end he ended up shedding blood so the dream pleases the believer, it doesn’t make him boastful.”
13) Dream interpretation is not certain but presumptive and Allah سبحانه و تعالى says in Surah Yusuf: “And he said to the one he presumed to be saved…” {ayah # 42}
Ibn Kathir رحمه الله mentions in his An-Nihayah wal Bidayah that there was a caliph (not a good one) of Ibn ‘Abbas who saw dream that he was climbing a dream with 28 steps. So he had that dream interpreted. The one who interpreted his dream told him that the meaning of this dream is, “You will rule for 28 years.” But he died six months later. He died at the age of 28 so the steps were representing his age not the time for his rule.
There was a woman who dreamt that her daughter would break three banners (flag carried in war time). So she went to Ibn Sirin رحمه الله and he interpreted that dream saying, “If her dream is true, it means that she would marry three noble men all of them would be killed.” When her daughter grew up, she married Yazid ibn al-Muhallab who was a great leader in ‘Iraq and he was killed. Later on, she married ‘Amr ibn Yazid at-Taymi and he was killed. Her third marriage was with al-Hasan ibn ‘Uthman ibn ‘Abdur Rahman ibn ‘Awf رحمه الله, the grandson of the Sahabi ‘Abdur Rahman bin ‘Awf. She had an argument with him and she told him, “In the Name of Allah, you would be killed.” He asked her the reason and she told him about her dream. He said, “Alright, I am going to divorce you since you think I am going to be killed now!” Finally, she married al-‘Abbas ibn ‘AbdiLlah ibn Harith ibn Nawfal ibn Harith ibn ‘Abdul Muttalib and he was killed.
One man saw in a dream, during the plague, that caskets were coming out of his house and the number of them was equal to the number of his family. So, he interpreted the dream that his entire family would be killed in the plague. And the dream started to manifest itself. His family were dying one after the other and all the bodies were coming out of his house exactly how he saw in his dream until he was the last member of his family left so he was pretty sure that he would be killed by the plague because his dream was, until now, true. But a thief came into his house and was struck by the plague, he fell ill in his house, he died and he was the last body to leave the house and not the person who saw the dream.
14) It is haram and a great sin to claim that one has a seen a dream whilst he has not seen it or to lie in it.
Narrated ‘AbduLlah ibn ‘Abbas رضي الله عنه that the Prophet صلى الله عليه و سلم said, “Whoever claims to have seen a dream that he has not seen, would be told to tie between two hairs on the Day of Judgement.”
15) A dream could be seen by a person but it could be for someone else.
Al Hakim and ‘AbduLlah Ibn Mubarak narrate that someone saw a dream for Abu Jahl that he became a Muslims and pledged allegiance to Prophet صلى الله عليه و سلم. But this never happened. So this dream was for his son, ‘Ikrimah رضي الله عنه who became a Muslim and pledged allegiance to Prophet صلى الله عليه و سلم later on.
A dream was seen for Usayd bin Abil ‘Aas that he became the governor of Makkah and he never did but his son ‘Attab became the governor of Makkah.
16) Same symbol in a dream could mean different things for different people
For example: A man came to Ibn Sirin رحمه الله and told him that he had seen himself in a dream giving Adhan. Ibn Sirin رحمه الله replied, “You will make Hajj.” Another man came with the same dream and Ibn Sirin رحمه الله replied, “You are a thief!” Ibn Sirin رحمه الله was asked the reason of him giving different interpretations of the same dream to different people and he said, “Because I saw in the first man’s face righteousness and Allah سبحانه و تعالى says in the Qur`an that Ibrahim عليه سلام made adhan calling people to Hajj so I interpreted this mean that this person would make Hajj. Whilst I saw evil on the face of the other man and Allah سبحانه و تعالى says in Surah Yusuf, ‘then a crier cried: ‘O you (in) the caravan! Surely, you are thieves!’ so I interpreted it to mean that this person is a thief.’”
17) Prophet صلى الله عليه و سلم said, “A dream is hanging on the leg of a bird (and in another narration on the wing of the bird) as soon as it is interpreted, it happens as it was interpreted.” So some scholars say that if you take your dream to a scholar, it would happen as it is interpreted by him so that’s why you must take it to a person who has knowledge about dream interpretation and or a person who would give you a sincere advice and not to the person who is envious so if the dream is interpreted it would happen as he interpreted.
However,
there is a difference of opinion regarding this issue.
And Allah سبحانه و تعالى knows best.
Source: Islam best Religion website.
Friday, 1 August 2014
SIKU YA IJUMA NA HUKMU ZAKE
Siku ya Ijumaa, ni siku bora kabisa iliyotokewa na jua. Katika siku hii Mwenyezimngu Alimuumba Adam,na Kiyama kitasimama siku ya ijuma, na ni siku ya Idi kwa Waislamu. Kwa hivyo, yameamrishwa baadhi ya mambo katika siku, miongoni mwao: hutuba ya Ijumaa,kuoga, kujitia manukato, kwenda Ijumaa kwa kuvaa vazi zuri zaidi napambo zuri zaidi, kwenda Ijumaa mapema, kukaa karibu na imamu na kuutayarisha moyo kusikiliza mawaidha na utajo wa Mwenyezi Mungu.
Utangulizi
Enyi watu, Mcheni Mwenyezi Mungu (Subhaanahu wa Taala). Na mjuwe ya kuwa hakika Mwenyezi Mungu (Subhaanahu wa Taala) huumba atakavyo na huchagua atakavyo. Amesema Mwenyezi Mungu (Subhaanahu wa Taala):
قال تعالى: {وَرَبُّكَ يَخْلُقُ مَا يَشَاءُ وَيَخْتَارُ مَا كَانَ لَهُمُ الْخِيَرَةُ } [القصص: 68]
{{ Na Mola wako huumba atakavyo na huchagua atakavyo, hawana viumbe hiari}}.. Na Mwenyezi Mungu (Subhaanahu wa Taala) ndie anaye jua hekima kwa kila kitu anacho kichagua miongoni mwa viumbe vyake. Mwenyezi Mungu (Subhaanahu wa Taala) huchagua Mitume miongoni mwa Malaika na watu. Na Mwenyezi Mungu (Subhaanahu wa Taala) ameufadhilsha Mji wa Makka kushinda sehemu nyingine. Na akauchagua Mji wa Madina kuwa ni mji aliohamia Mtume (Swalla Llahu ‘alayhi wasallam) na Masahaba. Kisha akauchagua Baytul Maqdis akajalia ni sehemu ya Mitume wengi ambayo Mwenyezi Mungu (Subhaanahu wa Taala) ametuelezea habari zao katika Qur’an Tukufu. Na Mwenyezi Mungu (Subhaanahu wa Taala) amefadhilisha baadhi ya Miezi kuliko mingine na Usiku na Mchana. Akachagua Miezi mine Mitukufu (Dhul-qa’ada, Dhul-hijja, Muharam na Rajab). Na bora wa masiku ni siku ya Ijumaa. Kwa hivyo, mtukuzeni Allah (Subhaanahu wa Taala) na kumsifu na kumsalia Mtume Muhammad (Swalla Llahu ‘alayhi wasallam).
Hukumu ya Swala ya Ijumaa
Swala ya Ijumaa ni miongoni mwa swala muhimu za faradhi. Na sharia imetia mkazo zaidi na kusisitiza kutekelezwa swala ya ijumaa kwa jamaa. Na malipo yake ni makubwa zaidi.
Fadhila za siku ya Ijumaa:
1. Kupata Thawabu na Malipo kwa kila hatua ya kwenda Msikitini sawa na Mtu aliyesimama kuswali na kufunga Mwaka mzima. Amesema Mtume (Swalla Llahu ‘alayhi wasallam) : [ Mwenye kuoga na kujisafisha, kisha akaenda Msikitini na mapema na akamkurubia Khatibu na akasikiliza kwa utulivu. Mwenyezi Mungu (Subhaanahu wa Taala) atamlipa kwa kila hatua malipo sawa na Mtu aliyesimama kuswali na kufunga Mwaka mzima] (Imepokewa na Ahmed).
2- Kusamehewa Madhambi yake ya wiki mzima pamoja na siku tatu za ziada. Amesema Mtume (Swalla Llahu ‘alayhi wasallam) : [ Mwenye kutawadha vizuri, kisha akaja Msikitini na akamsikiliza Khatibu na kunyamaza. Anasemehewa Madhambi yake ya wiki mzima pamoja na siku tatu]. Imepokewa na Muslim.
3- Kukubaliwa dua katika siku hii tukufu. Amesema Mtume (Swalla Llahu ‘alayhi wasallam) : [Hakika katika Siku ya Ijumaa kuna wakati, haafikiwi Muislamu na wakati huo hali akiwa anamuomba Allah, ila Mwenyezi Mungi humkubalia Dua yake].
Adabu na Sunna za Siku ya Ijumaa:
- Kuoga na kujisafisha na kupaka manukato mazuri pamoja na kuondosha harufu mbaya mwilini.. Amesema Mtume (Swalla Llahu ‘alayhi wasallam) : [Mwenye kuoga siku ya Ijumaa, kisha akaenda Msikitini na mapema. Mfano wake ni kama mtu aliyetowa sadaka ya Ngamia].
- Kwenda Msikitini mapema na kumkurubia khatibu. Amesema Mtume (Swalla Llahu ‘alayhi wasallam) : [Nedeni mkasali sala ya Ijumaa, na mkae karibu na khatibu].
- Kujishughulisha kwa Kumtaja Allah, kusoma Qur’an, kuomba msamaha, kuomba dua kwa wingi na kumsalia Mtume Muhammad (Swalla Llahu ‘alayhi wasallam).
- Kumsilikiza Khatibu kwa utulivu, bila ya kujishughulisha na mambo mengine.Asema Mtume (Swalla Llahu ‘alayhi wasallam) : [Mwenye kutawadha vizuri, kisha akaja Msikitini na akamsikiliza Khatibu na kunyamaza. Anasemehewa Madhambi yake ya wiki mzima pamoja na siku tatu]. Imepokewa na Muslim.
Mambo yalio katazwa katika swala ya Ijumaa:
- Kuja Msikitini kuchelewa na kukata safu kwa kuruka watu, kwa lengo la kutaka kukaa safu ya mbele. Siku moja Mtume (Swalla Llahu ‘alayhi wasallam) alimuona mtu akikata safu na kuruka watu; Akamuambia kaa chini kwa hakika umewaudhi watu na umefanya maasi makubwa.
- Kuwashawishi waja wa Mwenyezi Mungu, kwa kusoma Qur’an kwa sauti kubwa, au kufanya Dhikri kwa sauti ya juu. Mtume (Swalla Llahu ‘alayhi wasallam) aliwakataza Masahaba kusoma kwa sauti ya juu, na akawambia; Asisome mmoja wenu Qura’n kwa sauti ya juu kuliko mwingine.
- Kuzungumza wakati wa Khatibu anatoa khutbah ya Ijumaa. Amesema Mtume (Swalla Llahu ‘alayhi wasallam) : [Ukimuambia mwenzako nyamaza na Khatibu akiwa anazungumza, kwa hakika umeharibu swala ya Ijumaa].
Khatari ya kuacha kuswali swala ya Ijumaa
Mtume Muhammad amesisitiza na kutilia mkazo juu la suala la kutekeleza swala ya Ijumaa. Na akawatahadharisha Waislamu wanaoacha kutekeleza swala hii. Adhabu kubwa watakayo pata watu hao hapa duniani ni nyoyo zao kuwa ngumu na kupigwa muhuri wa kughafilika. Amesema Mtume (Swalla Llahu ‘alayhi wasallam): [ Hawataendelea watu kuacha swala ya Ijumaa, mpaka Mwenyezi Mungu apige muhuri nyoyo zao, kisha watakuwa niwenye kuishi katika mughafala].
Ndugu Waislamu, tujihadhari sana na kuacha swala ya Ijumaa, kwasababu adhabu yake ni nzito sana. Moyo ukiwa mgumu, basi mwanadamu anakuwa sawa na myama, hajali lolote wala chochote. Utamuona hamuogopi Mwenyezi Mungu, kwa kufanya maasi usiku na mchana.
Tunamuomba Allah (Subhaanahu wa Taala) athibitishe nyoyo zetu juu ya twaa yake, na atulinde na machafu yote.
KHUTBA YA PILI
Ndugu Waislamu, katika Mafundisho ya Mtume Muhammad (Swalla Llahu ‘alayhi wasallam) ni kuitukuza siku hii ya Ijumaa, kwani hii ni siku tukufu ilio chaguliwa na Mwenyezi Mungu (Subhaanahu wa Taala) na kupatiwa Umma huu wa mwisho.
Mtume Muhammad (Swalla Llahu ‘alayhi wasallam) alikhusisha baadhi ya vitendo katika siku ya Ijumaa:
- Kusoma Surat Sijdah na Surat Insaan katika swala ya Al-Fajiri. Imepokewa na Abu Hureirah – Radhi za Allah ziwe juu yake- { Alikuwa Mtume akisoma katika swala ya Al-Fajri siku ya Ijumaa (Surat Sijdah) katika rakaa ya kwanza. Na katika rakaa ya pili (Surat Insaan) } Muslim.
- Kusoma Surat Al-Kahfi. Amesema Mtume (Swalla Llahu ‘alayhi wasallam): {Mwenye kusoma Surat Al-Kahfi siku ya Ijumaa, Mwenyezi Mungu anampa mwangaza baina ya Ijumaa mpaka Ijumaa nyingine}. Al-Bayhaqi na Haakim.
- Kuzidisha kwa wingi kumsalia Mtume Muhammad (Swalla Llahu ‘alayhi wasallam). Amesema Ibnu-Qayyim: “Mtume wa Mwenyezi Mungu ni Bwana wa viumbe vyote, na siku ya Ijumaa ni bwana wa siku zote. Kumswalia Mtume siku hii ina malipo mengi kushinda siku nyingine”.
- Kuzidisha kumuomba Allah (Subhaanahu wa Taala) katika siku hii. Kwasababu kuna wakati wa kukubaliwa dua ya Muislamu. Amesema Mtume (Swalla Llahu ‘alayhi wasallam) : [Hakika katika Siku ya Ijumaa kuna wakati, haafikiwi Muislamu na wakati huo hali akiwa anamuomba Allah, ila Mwenyezi Mungu humkubalia Dua yake].
Mwisho
Ndugu katika Imani, kama tulivyo sikia umuhimu wa siku ya Ijumaa, na namna sheria ilivyo tilia mkazo siku hii. Na vilivile malipo na thawaabu nyingi kwa Yule atakae tekeleza ibada kwa masharti yake na nguzo zake. Ni jukumu letu kufanya bidii kwa kufanya ibada mbali mabali kama alivyo tufundisha Mtume (Swalla Llahu ‘alayhi wasallam), ili tuweze kupata malipo na thawabu nyingi kutoka kwa Allah (Subhaanahu wa Taala). Enyi Waislamu, Tushindaneni kufuata Sunna na Mafundisho ya Mtume (Swalla Llahu ‘alayhi wasallam) katika siku hii kuu.
Mwenyezi Mungu atujaalie miongoni mwa waja wake wema na atupe uwezo wa kufuata Sunna za Mtume (Swalla Llahu ‘alayhi wasallam). Tunamuomba Allah atukubalie ibada zetu na atupe mwisho mwema tukiondoka duniani.